Wamiliki wa Jengo lililopo mtaa wa Msimbazi na Agrey Kariakoo wameamua kuchukua hatua la kulibomoa

Wamiliki wa Jengo lililopo mtaa wa Msimbazi na Agrey Kariakoo wameamua kuchukua hatua la kulibomoa

Mkalukungone mwamba

JF-Expert Member
Joined
Aug 29, 2022
Posts
862
Reaction score
1,755
Kiukweli nawapongeza wamiliki wa jengo hili kuona umuhimu wa kuliboboa jengo ambalo ni la muda mrefu tena limeshaanza kuonyesha ishara mbaya.

Bila shaka wamejifunza pakubwa baada ya kuporomoka kwa jengo la kariakoo na kusababisha vifo kadhaa vya watanzania na hata biashara zao kuharibika.
===================
Wamiliki wa Jengo lililopo mtaa wa Msimbazi na Agrey Kariakoo wameamua kuchukua hatua ya kulishusha/ kulibomoa Jengo lao kwa hiyari yao baada ya kuona jengo hilo limekua chakavu na ni hatarishi kwa matumizi kabla halijadondoka na kuleta athari.

Pia, Soma: Live Updates Kuporomoka kwa Ghorofa Kariakoo Nov 16: Watu 7 wengine waokolewa

Warda Adallah Mohammed ambaye ni mmoja wa wasimamizi wa Jengo hilo akizungumza na wahandishi wa habari jioni ya leo amesema kuwa uamuzi huo ulifanyika baada ya kulifanyia utafiti jengo hilo na wataalamu kugundua kuwa linatakiwa kuangushwa na halifai kwa matumizi kwani lina zaidi ya miaka 90 toka kujengwa kwake.

 
na hayo mengine yote yaliyovunjwa na kujemgwa upya kabla ya tukio ka maafa ya kuanguka ghorofa, sababu ilikuwa ipi?
 
Huyo mama mjanja, upo uwezekano wa jengo kuwa na bima.

Wamejipanga.
 
Liache kuanguka miaka yote hiyo karibia karne moja ndio lije lianguke sasa kwa kuwa limechakaa? Aseme tu ameamua kulibomoa na kujenga jingine jipya la kisasa zaidi. Basi kwa mtazamo huo kuna haja ya kubomoa majengo yote machakavu yenye umri huo kwa dhana hiyo.
 
Huyo mama mjanja, upo uwezekano wa jengo kuwa na bima.

Wamejipanga.

Bila hata bima. Kiwanja tu kitupu kariakoo ni rasilimali kubwa.

Wawekezaji kibao wapo tayari kukujengea ukiwa na kiwanja kariakoo. Kisha mnagawana idadi ya fremu. Kila mtu anakula kodi.

Jengo wanavunja kisha wanajenga upya. Kama hawana hela za kujenga upya wanamtafuta investor anawajengea. Kodi wanakula kama kawaida
 
Sasa ukitaka awe lofa lofa kama wewe?!!!
Comment kwanza kuhusu ubora au ubaya wa hatua hiyo.......tujifunze kuwa positive jamani, dah!!!!
Yaani hawa wana mawazo kama ya mdogo wake na huyo mama ambaye alileta polisi kuzuia kuvunjwa kwa jengo. Watanzania wengine wanachojali ni pesa tu kuliko usalama
 
Back
Top Bottom