Kweli Mtwara tumeondokana na zama zile za kusafiri siku mbili hadi tatu, siku hizi Masasi unafika saa 9 au 8.45 mchana. Tunashukuru sana kwa hilo. Ila kuna kero kubwa sana inatusumbua abiria waendao Mkoa huo, kulipia bag suala hili kwa kweli linakera sana sana sana, abiria yeyote akisafiri jamani ni lazima achukue bag, sasa inakuwaje ulipe nauli, halafu ulipie tena na bag? hivi hii ni biashara ya madereva na makondakta au ni ya wamiliki wa mabasi hayo? Na je, wamiliki wa mabasi wanalijua suala hili? hivi ukasalimie nyumbani usichukue hata zawadi? na ukichukua zawadi uwaze nauli, gharama ya zawadi, gharama ya bag!!! tutafika kweli?
Kinachonishangaza zaidi, ukisafiri kwenda mikoa mingine kama Arusha, Dodoma, Tanga na kwingineko hukuti mambo kama haya, hata uchukue bag kubwa kiasi gani hilipi, sasa kwanini taratibu wa usafiri zinatofautiana na mikoa mingine? utaratibu huu ulianzishwa na nani? SUMATRA jamani chonde tusaidieni Mtwara tumechoka kulipia mabag kwa kweli, ni bora watuambie nauli sh 30,000/= lakini nikiwa na bag nisilipe kuliko kulipa nauli sh 25,000/= bag na zawadi zingine sh. 20,000/= inchosha sana na mimi nimechoka na hali hii, vyombo husika vifuatilie suala hili
Kinachonishangaza zaidi, ukisafiri kwenda mikoa mingine kama Arusha, Dodoma, Tanga na kwingineko hukuti mambo kama haya, hata uchukue bag kubwa kiasi gani hilipi, sasa kwanini taratibu wa usafiri zinatofautiana na mikoa mingine? utaratibu huu ulianzishwa na nani? SUMATRA jamani chonde tusaidieni Mtwara tumechoka kulipia mabag kwa kweli, ni bora watuambie nauli sh 30,000/= lakini nikiwa na bag nisilipe kuliko kulipa nauli sh 25,000/= bag na zawadi zingine sh. 20,000/= inchosha sana na mimi nimechoka na hali hii, vyombo husika vifuatilie suala hili