Dreamlinerz
Member
- Jun 17, 2019
- 62
- 77
- Thread starter
-
- #21
Uzuri wa hizo ukihitaji unaipata hata ukiitaka saa 8 usiku unapata,sio hizi gari nyingine.Toyota kama crown,mark X,brevis bado bei spare zake ni mziki.
Ndio maana carina Ti Yangu naipenda Sana Kwenye spare hainiumizi kichwa sana
Yes mkuu hata mm nilikuwa na Carina ti yaani spare zake huumizi kichwa.
Sasa hivi nikipata pesa nataka ninunue rav 4 nione Kama itakuwa vzr kwenye gharama za spares.
Napenda Rav 4 J nasikia ndio ngumuInategemea RAV 4 ya mwaka gani kama hizi za 2006 kwenda mbele spare bei ni zile zile tu mkuu...
Embu ona sasa,tofauti ya laki nzima!Huyu jamaa nimemkubali sana, nilikuwa natafuta spare ya nissan bluebird hapa dar naambiwa 360,000 ila nilipomcheki yeye kaniagizia nje nadhani nairobi kwa 140,000 ndani ya siku mbili mzigo nikaupata na sasa nadunda mtaani.
Kweli kabisaTatizo ukizoea hizi gari kuziacha nayo ngumu.
Tatizo wakiwa na garage za ntaani huwa hawapo. Unamoatia gari anawapa vijanaUnajua hao dealers possibility ya kua wana garage za mtaani ni kubwa sana huwezi jua unaweza ukawa unapata hata spea kwa bei ya punguzo fulani
Ni competitor wa Toyota Alphad......Nissan Elgrande imekaaje wakuu. Naona bei imepoa na chombo kina space ya kutosha
Daah. Maana natafuta gari ya juu Kwa bajeti ya 11m (gharama zote)Ni competitor wa Toyota Alphad......
Spea ni ghali kidoogo
Daah. Maana natafuta gari ya juu Kwa bajeti ya 11m (gharama zote)
NATAFUTA MLANGO STARLET WA ABIRIA KUSHOTO NYUMAKama kichwa cha habari kinavyojieleza,sisi wamiliki wa magari ambayo ni brand tofauti na TOYOTA tunapata changamoto nyingi sana ambazo zinapelekea wengine kushindwa kuyahudumia magari yao na mwisho kuachana nayo au kuyatelekeza kwenye magereji au kuyauza kwa bei ya HASARA kitu kinachopelekea magari haya kuonekana hayafai na watu wengi kusita na kuogopa kuyanunua.
Sasa basi Uzi huu ukawe msaada wa kupeana habari,taarifa,na huduma ambazo zitapelekea kusaidia kupunguza adha ya kuhudumia magari yetu kuanzia kwenye upatikanaji wa spare parts kwa bei reasonable na mafundi wenye ujuzi wa kuzielewa hizi gari.
Mimi binafsi nimeshakutana na changamoto nyingi kwa kumiliki ka gari kangu kadogo aina ya VW POLO,nimevumilia matatizo mengi ya mafundi na bei kubwa za spare tangu nimeanza kukamiliki lakini kilichonitokea juzi juzi hapa ndicho kilichopelekea mimi kuleta huu mjadala humu jukwaani ili tuweze kusaidiana na mwishowe magari haya yaonekane ya kawaida na isiwe adhabu kuyamiliki.
Gari yangu ilikuwa na tatizo la fuel pump la muda mrefu kidogo baada ya kuwekewa mafuta machafu,kwahiyo ilikuwa na tatizo la kuchangaya,ilikuwa naweza kusimama kwenye mataa taa zikiruhusu gari inakosa nguvu ya kwenda kabisa kiasi kwamba magari ya nyuma yangu yananipigia honi,fundi akaniambia hiyo itakuwa tatizo ni fuel pump,ikabidi niingie mtandaoni nikakutana na jamaa anauza spare za magari mbalimbali sitamtaja humu basi fuel pump bila housing yake ilinitoka 250,000/= pamoja na kubembeleza nipunguziwe bei haikusaidia ilinibidi ninunue tu kwasababu gari ndio ninayoitumia kwa mizunguko yangu mjini lakini iliniuma sana kwasababu najua online aliexpress fuel pump hiyo isingezidi 70,000 mpaka kuipata lakini ingenibidi nisubiri wiki tatu au zaidi na hiyo ndio ilikuwa changamoto
Na hiyo sio mara ya kwanza kununua spare kwa bei mbaya kuizidi hii,changamoto ni nyingi sana kwahiyo wale wamiliki wenzangu wa magari haya adimu,mafundi,wauzaji spare tukutane hapa tuelezee changamoto tunazokutana nazo ili tuweze kuona ni namna gani tunaweza kusaidiana.
Nawasilisha.
Pole mkuu sasa umeiuza nini au umepata suluhisho la spea zake.Mkuu ulikuwa sahihi ukiona mtu anajibu pumba kwahuu uzi uliouleta ujuwe huyo anamiliki baiskel achana naye mimi nimemiliki mazda imenitesa kwenye spea najuta kwenye Toyota kifaa cha 125000 mazda utapata kwa 400,000 wakati huo spea nishida kuzipata, kwa ushauli mfuko ukituna gari yakununua ni Toyota
Hiyo ni bei ya kawaida mkuu. Hasa ukinunua OEM parts. Mie nimenunua ya Toyota Tsh 120,000. Sema za Toyota mara nyingi kuna kuwa na copies nyingi mtaani ndio maana zinaonekana cheap.Namiliki Nissan FUGA timing belt tu ilikatika ikanitoka 110,000
Timing belt ya Nidsan hiyo mbona ni bei ya kawaida saana....na isitoshe nissan spea zao nyingi si magumashi...hapo ni mkataba.Namiliki Nissan FUGA timing belt tu ilikatika ikanitoka 110,000
Kamata Noah new model chibu kwa 10.5 m only!Daah. Maana natafuta gari ya juu Kwa bajeti ya 11m (gharama zote)
Kuna jamaa anaitwa kindimu anapatikana kurasini mivinjeni ndo Fundi hatari wa mabenzi na VW na hizi BMW au mini CooperKwa wenye Benz huwa naona kuna mtundu wa gari hizo huku Kijichi 'kwa mabenzi'
Sawa mkuu. Nasubiria ofa za BeFoward mwisho wa mwaka. SBT wana products za ovyo sanaKamata Noah new model chibu kwa 10.5 m only!