Uchaguzi 2020 Wana-CHADEMA mnapoenda kumpitisha mgombea Urais, tuleteeni mgombea ambaye ni Chaguo la Wananchi

Uchaguzi 2020 Wana-CHADEMA mnapoenda kumpitisha mgombea Urais, tuleteeni mgombea ambaye ni Chaguo la Wananchi

Joined
May 16, 2020
Posts
41
Reaction score
59
Ndugu wanamabadiliko wenzangu mlioko ndani ya vikao vya maamuzi CHADEMA chonde chonde mnapoenda kwenye kwenye kura za kuteua mgombea wa urais tafadhalini kazi moja tu mlionayo fitina na figisu zenu ziwekeni pembeni tuleteeni mgombea ambae ni chaguo la wananchi na siyo chaguo lenu binafisi

Chaguo la wananchi si mwingine bali ni Tundu Antipasi Lissu. Huyu ndiye kete pekee anaekubalika na wananchi wote bila kujali vyama vyao kabila zao dini zao rika zao lakini pia ni mtu pekee mwenye uwezo wa kukabiliana na Magufuli. Nyalandu ni presidential material lakini hakubaliki na hana jina kwa wananchi kama mwamba Lissu

Mkijichangana mkaleta jina tofauti na hilo mjue chama chenu mtakuwa mmekipoteza mazima kwenye uwanja wa siasa. Pamoja na figisu za utitiri wa kesi za kubambikiwa alizonazo mwamba Lissu bado yeye ndo chaguo la wananchi na kwa uwezo wake na weledi alionao wa taaluma yake binafisi sioni kama kuna kesi ya kumsumbua hapo.

Na serikali kupitia tume ya uchaguzi wakijichanganya kuondoa jina lake hapo ndo utakuwa mwanzo wa mabadiliko tunayoyalilia siku zote. Hapo ndo tutajua nini maana ya nguvu ya umma.

Narudia kuwaomba wajumbe wa vikao vya uteuzi tuleteeni chaguo letu Lissu. Lissu ndo mpango mzima wa mungu ni zawadi yetu watanzania mungu ana makusudi makubwa na yeye tumruhusu atimize mapenzi yake kupitia mja wake.

Mara ya kwanza kutimiza mapenzi yake ni pale alipomnusuru na kifo baada ya kushindiriwa utitiri wa risasi za moto zaidi 32 huku nusu yake zikicharanga mwili wake bila mafanikio ya kumuua.

Mara hii mungu ameamua kutimiza mapenzi yake dhidi yake kwa kumfanya awe rais wa watanzania. Tafadhali msifanye makosa. Kila la kheri katika vikao vyenu macho na matumaini ya wapenda mabadiliko yako kwenu muwe na dominika njema.

Ndimi mpenda mabadiliko obhwitabhwandebha@gmail.com
 
WamekusikiA mkuu . Siasa inakitu kama kiu ya maji. Kiu uanza pole pole na mwishowe huwa juu.Uvunaji wa wanachama katika Chama chochote huku a mda bada ya mda!!I mean Political Royalty !!mtu pekee aliejenga na ataendelea kujenga royalty ni Lissu. Lissu amebeba kundi kubwa la vijana ambao wengi wao ni wasomi ama waelewa kuliko kundi lingne.
Chonde chonde CDM tendeeeni haki wananchi kwa kuwapa chaguo lenye kukata kiu yao!!
 
Mataanio yako umeyaita ya Watanzania? Watanzania wanataka JPM tubasi. Wengine hata wasipo gombea.
 
Back
Top Bottom