Wana JF, mwenye moyo wa kunikopesha laki nne nimepata dharura

Ndugu watu tunatofautiana.
Haupo serious.
Yani unaweka nyumba bond?
Hata ninayo pesa sikukopeshi.

Laki nna nikupe afu uweke nyumba.
Ili ukishindwa kulipa nikiuza hio nyumba uanze kulia lia na familia yako.

Kama huweZi kujieleza vizuri unadhani nani atakusaidia
 
Haupo serious.
Yani unaweka nyumba bond?
Hata ninayo pesa sikukopeshi.

Laki nna nikupe afu uweke nyumba.
Ili ukishindwa kulipa nikiuza hio nyumba uanze kulia lia na familia yako.

Kama huweZi kujieleza vizuri unadhani nani atakusaidia
Samahani kama hujalielewa vizuri hilo, nimesema kua tutakavokua tumekubaliana hata nyumba niko radhi kuweka dhamana, inamaana kwamba kama utakua hujaridhika na dhamana ninazotarajia kuweka, kulingana na shida nilionayo niko radhi kuweka hata nyumba ndugu yangu, samahani kama hukunielewa vizuri.
 
Mrejesho, nimekomaa mpaka nimepata laki mbili namshukuru Mungu, ila bado nina upungufu wa laki mbili wadau naombeni msaada wenu wa hali na mali ili niweze kutatua hili tatizo, nimebanwa kwakweli sina jinsi.
 
Njia pekee ya kupata hiyo hela ni kugawa labda 100k au 50k na kukopa kwa watu wako wa karibu maana kutoa 400k kwa pamoja risk ni kubwa mno hata kama mtu anayo
 
Njia pekee ya kupata hiyo hela ni kugawa labda 100k au 50k na kukopa kwa watu wako wa karibu maana kutoa 400k kwa pamoja risk ni kubwa mno hata kama mtu anayo
Mkuu nimekopa kwa style hio ndo maana nimefanikiwa kupata laki mbili, hizo nimezipata juzi, sasa naomba wadau wa JF mnisaidie hio laki mbili iliobaki, maana sasa kwa ndugu jamaa na marafiki hapo ndo walipoishia kunisaidia, naombeni msaada wenu Kwakweli nimebanwa mwenzenu silali.
 
Njia pekee ya kupata hiyo hela ni kugawa labda 100k au 50k na kukopa kwa watu wako wa karibu maana kutoa 400k kwa pamoja risk ni kubwa mno hata kama mtu anayo
Ujue mpaka nimepata hio hela, wameniazima kwa mtindo huu, mmoja kaniazima 100k, mwingine 50k na mwingine 50k ndo ikawa imepatikana laki mbili, lakini sasa nina upungufu wa laki mbili naombeni msaada wenu jamani wa hali na mali.
 
Labda niseme tu kua kwa jinsi nilivobanwa niko radhi kwa makubaliano yoyote jamani naombeni msaada wenu.
 
Nenda kwenye taasisi ndogo ndogo za kukopesha fedha (microfinance institutions) such as BRAC, FINCA, PRIDE and the like
 
Kikubwa zaidi ni kumshukuru Mungu kwa kila jambo, jamani wadau naombeni msaada wenu wa hali na mali, mniazime hio lakimbili iliobaki ili niweze kutatua tatizo nililo nalo, kama nilivoazimwa huku kwa majirani, marafiki na ndugu, kwa mtindo huo huo nawaomba mnisaidie atakaekua na laki au hamsini ili mradi nikamilishe hio pesa iliobaki.
 
Mi ningekuazima lakini watu mmebadilika sana maana hata wengine waliokuja kwangu sasa nimeamua kujitolea tu kwamba sina mpango wa kudai tena.
Na vile vile Tanga na nilipo mimi ni vitu viwili tofauti maana sina hata ndugu huko kwamba atakuja kuchukua dhamana ya kitu chochote.
Kwakweli nilikoma, nilisema sitokuja kukopesha tena kwa tabia za waliotangulia.
 
Mkuu pole, lakini usijefikiri wote tupo hivo, kwa Tanga mi nipo Korogwe mjini waweza angalia namna ya kunisitiri mkuu.
 
Laki nne hii au unamaanisha 400,000 hii...!!!kama n hizo zote na ikatokea umekopeshwa kweli naomba kwa herufi kubwa uje utupe mrejesho wa kifo chako.[emoji36][emoji36]
 
Laki nne hii au unamaanisha 400,000 hii...!!!kama n hizo zote na ikatokea umekopeshwa kweli naomba kwa herufi kubwa uje utupe mrejesho wa kifo chako.[emoji36][emoji36]
Mkuu usijali nimefafanua vizuri hapo juu, kua nimeshapata laki mbili kwa kukopeshwa kidogo kidogo, iliobaki sasa hivi ni laki mbili, naomba wadau wenye kuguswa mniazime hio iliobaki, si lazima mtu aniazime yote ila yoyote ile itakayopatikana mwenye hamsini au laki au kiasi chochote kile ili mi niweze kujazia kwenye iliobaki ili kutatua tatizo langu, natanguliza shukurani zangu kwenu.
 
Utapata mkuu, jf wema wapo sana
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…