Wana Simba SC tutaje wachezaji tunaoona hawatufai msimu ujao

Umeua mkuu tena sana.. Ila kwa nini center Midfieder tusichukue wawili(2) wa kigeni ??
Wa kumsaidia Kapombe awe mzawa.. na huyu MAEMBE wa wapi na nafasi gani anacheza?
Nakubaliana na ushauri wako Kapombe asaidiwe na beki mzawa labda Kimenya wa Prison au mwingine mkali, tulete professionals defensive midfielder wawili. Sorry nilikosea sio Vitalis Maembe Bali Vitalis Mayanga wa ndanda ambaye tayari tunamkataba naye.
 
Apo kwa mzamiru umepotea
 
Simba ni sehemu salama ya kuua vipaji vya wachezaji! Daah yaan jembe kama Mbonde ndio lishapotea! Kwasi, Mo, Salamba, Mlipili ..........Then mbabaishaji kama Manula eti anacheza!
 
Usajili ujao utahusisha sana wachezaji kutoka nnje, ndio maana nasema kama kuna wazawa watabaki, inabidi wapambane kwelikweli

Simba tutahitaji beki namba tatu kutoka nnje mkali

Tutahitaji mabeki wawili wa kati kutoka nnje wakali

Tutahitaji mawinga wawili wakali kutoka nnje

Tutahitaji pia mshambuliaji mmoja mkali kutoka nnje

Hii ni kama tunalitaka kweli kombe la ligi ya mabingwa Africa
 
Simba ni sehemu salama ya kuua vipaji vya wachezaji! Daah yaan jembe kama Mbonde ndio lishapotea! Kwasi, Mo, Salamba, Mlipili ..........Then mbabaishaji kama Manula eti anacheza!
Kiwango mzee, kumbuka mbonde ni majeraha, hao wengine viwango vyao sio vya kucheza simba ya maendeleo
 
Simba ni sehemu salama ya kuua vipaji vya wachezaji! Daah yaan jembe kama Mbonde ndio lishapotea! Kwasi, Mo, Salamba, Mlipili ..........Then mbabaishaji kama Manula eti anacheza!
Timu sehemu salama ya kucheza mpira tanzania ni ipi???...wakina samatta kwani walipitia ombaomba fc??
 
Mashabiki wa soka Tanzania ndio upeo wetu aisee..hapo watu wanatoa mapemdekezo as if wanachangiaga pesa za usajili..unakuta jitu lipo hapa na hata kuchangia timu kwa kuingia uwanjani haliwezi..Nazi kutoa mapendekezo..unakuta hata wengine hawanunui jezi orijino hawanunui..

Alafu hizi ni story za abunuasi aisee..kocha ndie mwenye wachezaji ...atatoa mapendekzo yatafanyiwa kazi...
 
Kiwango mzee, kumbuka mbonde ni majeraha, hao wengine viwango vyao sio vya kucheza simba ya maendeleo
Tamaa mmezidi mkuu! Kwasi na Salamba tuliwataka, kwa kuwa mna mawe mkawadaka! Mmeshauwa vipaji vyao sasa hamuwataki!
 
Mzamiru yupo vizuri ila ndemla sina uhakika nae sana....simba inahitaji marekebisho sehemu chache but marekebisho yawe makubwa sana ya wachezaji wakubwa wa kimataifa....sehemu ya ulinzi na kiungo zipewe kipaumbele
Kabisa mkuu
 
Simba ni sehemu salama ya kuua vipaji vya wachezaji! Daah yaan jembe kama Mbonde ndio lishapotea! Kwasi, Mo, Salamba, Mlipili ..........Then mbabaishaji kama Manula eti anacheza!
Mkuu Manula akija yanga atacheza nafasi ya Fei toto?
Usipopambana kupata namba unapotea.. Simba sio timu ya mama yao eti wacheze kiholela tu.
 
Hakuna ubishi kocha ndio mwamuzi.. haya ni maoni yetu mashabiki wala sio sheria.
Waliopo bongo wanajadili ya Liverpool a/u Man u utawaambiaje??
Uwanjani tunaingi na Jezi tunanunua.. tulia kama hayakuhusu
 
Mkuu Manula akija yanga atacheza nafasi ya Fei toto?
Usipopambana kupata namba unapotea.. Simba sio timu ya mama yao eti wacheze kiholela tu.
Mkuu mwambie kweli simba inaua vipaji ndo mana iliua mpaka cha samatta ndo mana amefika alipo leo
 
Tamaa mmezidi mkuu! Kwasi na Salamba tuliwataka, kwa kuwa mna mawe mkawadaka! Mmeshauwa vipaji vyao sasa hamuwataki!
Kumbe mliwataka waje kucheza ndondo au ridhaa?.. Mbona hawajazeeka chukueni , kwani BOBAN + NGASA wamekuja kufua kiwango jangwani.?
 
Kumbe mliwataka waje kucheza ndondo au ridhaa?.. Mbona hawajazeeka chukueni , kwani BOBAN + NGASA wamekuja kufua kiwango jangwani.?
Mkuu ukiangalia kwa makini Ngasa na Boban ni kama tumeinua viwango vyao ukilinganisha na walivyokuwa kabla ya kujiunga Yanga msimu uliopita!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…