Wana Yanga mlifurahi miaka minne ya Malinzi sasa ni zamu yetu Simba kufurahi miaka minne ijayo

Kama ni hivi balaa...
 
Mezani FC kwan hao viongozi wataingia uwanjani na vitambi vyao kucheza? Hamuwezi kuweka rekod mpaka TFF yote iwe Simba?
 
Ninachokiona hapa nikutaka kuwaharibia pace hawa viongozi wapya waliochaguliwa. Wakati huohuo huyu shabiki uchwara akitaka kuficha madhaifu ya simba kwa kujidanganya makusudi kabisa kwa kuhamisha lawama kwa watu wengine. Nimalize kwa kuuliza, je CAF na FIFA nazo zina usimba na uyanga au rufaa haikufika huko?
 
Umemsahau Bi. Hindu ni Simba toka enzi ya Sunderland
 
Umesema kweli kabisa , kama watu wao waligombea ili kuipa Simba ubingwa watasubiri sana.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Umesema kweli kabisa , kama watu wao waligombea ili kuipa Simba ubingwa watasubiri sana.

Sent using Jamii Forums mobile app
Kama kweli hao waliotajwa kuongoza TFF wote ni wanachama/wapenzi wa Simba, na kama kweli huo ulkuwa ni mkakati mahsusi wa Simba, basi wategemee anguko endelevu takatifu. Kwa nini? Mzazi ambaye ni mwalimu wa mwanafunzi wake mwenyewe darasani, anayemwonyesha maswala a mtihani na kumpa majibu yake ili afaulu, huishia kumgeuza mwanafunzi huyo kuwa kihiyo, huku wenzake wanaohngaika kwa uwezo na nguvu zao wakiendelea kuelimika inavyostahili hata kama hawabebi nafasi ya kwanza darasani. Wanapoingia darasa au shule nyengine ambayo mwalimu-baba hana mamlaka nayo, wanafunzi wa aina hiyo hugeuka ghafla kutoka wa mfano kuwa ni kituko.
Aidha, hoja chelema za wanaodai Yanga inabebwa zinaanzia pale Yanga inapoanzia ama Simba inapoishia. Huanzia pale Yanga inapoanzia kwa fowadi yake kutoziwilika kwa mbinu za kawaida, hivyo marefa kutoa adhabu za penalti. Sasa ina maana kwa viongozi hawa nje ya uwanja maana yake ni kwamba Yanga hawatapewa penalti ndani ya uwanja? Huanzia pale Simba inapoishia kufungwa ndani ya uwanja na kukata rufaa bila ya kufuata taratibu, hivyo kushindwa rufaa yao. Sasa ina maana kwa viongozi hawa nje ya uwanja Simba haitafungwa ndani ya uwanja, na hata ikifungwa wataipa ushindi hata taratibu zikiendelea kutofuatwa?
Nitafutahi wakifanya hivyo maana angalau uhakika wa kutochukua ubingwa unazidi kuwa mkubwa, hata kama hautachukuliwa na Yanga. Si kwa sababu ya udhaifu bali ya championship-fatigue, ile hali ya timu kukosa morali ya kupigania ubingwa kwa sababu ya mazowea ya kuuchukua muda mrefu mfululizo.
 
Naomba viongozi wetu wasiwe na ile tabia ya Malinzi itamaliza soka letu tu, nakubali kuna mapenzi na team lakini yasifikie kile kiwango cha malinzi ni ujinga ule na sio mapenzi na team.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…