Wanachimba Michanga wanahatarisha Maisha yetu Kisarawe Two (Kigamboni), hawataki kusitisha mchakato huo

Wanachimba Michanga wanahatarisha Maisha yetu Kisarawe Two (Kigamboni), hawataki kusitisha mchakato huo

BigTall

JF-Expert Member
Joined
Mar 9, 2022
Posts
525
Reaction score
1,257
WhatsApp Image 2024-08-07 at 19.47.28_f1564b96.jpg
Uchimbaji huo wa mchanga umekuwa ukifanyika kwa zaidi ya miaka minne sasa, tumeripoti kwenye Mamlaka mbalimbali lakini bado wahusika wamekuwa wakiendelea na hivyo kuweka nyumba zetu kwenye hatari ya kubomoka hasa kipindi cha mvua.

Uchumbaji wa michanga maeneo ya Mwaninga, Chekeni, Kisarawe II, Mwasonga, Kigamboni umekuwa ukisababisha zile sehemu zilizochimbwa kuwa kama visima na hivyo vyombo vya usafiri kushindwa kupita, hali hiyo inatupa changamoto kubwa kupata huduma.

Eneo letu hili ni la makazi ya Watu lakini sasa hivi limegeuka kuwa eneo la kuchimba michanga.

Tutukienda kuwasilisha malalamiko yetu kwa Viongozi wa Serikali za mtaa hakuna msaada wa maana, miundombinu umeharibika imekuwa ni sehemu ya Wachimba Mchanga.
WhatsApp Image 2024-08-07 at 19.47.28_96f9a7e5.jpg


Tulienda kwa Mkuu wa Wilaya tukaonana na Msaidizi wake tukamuelezea kinachoendelea lakini huu ni zaidi ya mwezi wa pili sasa hakuna mrejesho wowote kutoka kwake.

Inapotokea kuna wagonjwa wa dharura au Wajawazito wanapopata shida ni mtihani kupata msaada, hada Bodaboda wenyewe wanaogopa kuja kutuchua kutokana na njia kutokuwa rafiki.

Ukitembea kidogo mitaa ya huku kujikuta umezama kwenye dimbwi la maji ni jambo ambalo linatikea mara kwa mara.

Wakati wa mvua Wanafunzi wamekuwa wakilazimika kukaa nyumbani kwa zaidi ya miezi kwa kuwa njia zinajaa maji inakuwa ni hatari kupita.
 
Back
Top Bottom