Wanachuo kibao walala nje ya studio za S2kizzy ili warekodi wimbo

Wanachuo kibao walala nje ya studio za S2kizzy ili warekodi wimbo

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Hakuna ubishi kuwa S2kizzy aka Zombie ndiye producer mkali sana hivi sasa na amefanikiwa kwa kiasi kikubwa kuachia hit songs tu na kujijengea heshima ndani na nje ya Bongo.

Hivi karibuni S2Kizzy alitangaza ku-record wimbo bure kwa wanafunzi wa chuo, na habari hii ilivutia umati mkubwa. Jana, wanafunzi wengi walijitokeza na kulala nje ya studio hizo za Pluto ili kupata fursa hiyo ya kipekee.
Hali ilikuwa ya kusisimua, huku vijana wakisubiri kwa hamu kuweza kuingia na kurekodi sauti zao. Wanafunzi hao walionyesha ari na juhudi kubwa, wakiwa na ndoto ya kufanya muziki na kuonyesha vipaji vyao.
Angalia ilivyokuwa: wahusika walipiga picha, wakisherehekea pamoja, na kila mmoja akijaribu kujiandaa kwa ajili ya kurekodi. Hii ni fursa ambayo wengi hawakuweza kuikosa, na inadhihirisha jinsi muziki unavyoweza kuwa daraja kwa vijana wa kisasa.

Soma: Hakuna ubishi, S2kizzy ni producer bora kuzidi mkongwe Master Jay
 
Ukisikia kizazi cha wakata mauno ndy hicho sasa kila kijana anataka kuwa msanii sahv

Ova
 
Hao wote walitakiwa wakapambane huko mashambani na viwandani,lakini kama mazingira na miundombinu ikiwepo .... sasa vijana kwa asilimia kubwa wakitaka kuwa wasanii hapo kuna shida

Ova
 
Back
Top Bottom