mpiganiahaki
Senior Member
- Apr 28, 2011
- 170
- 67
Wanafunzi wa UDOM kitivo cha Teknolojia ya mawasiliano na Elimu Angavu(College of Informatics&Virtual Education) tunaendelea na mgomo wa kutoingia darasani ili kushinikiza Utawala kuwarudisha wenzetu 27 waliosimamishwa masomo kurudishwa chuoni.
Msimamo huu ulianza tokea Alhamis ya wiki iliyopita baada ya wanafunzi wenzetu wapatao 10 kusimamishwa masomo kwa madai kuwa ndio waliokuwa vinara wa maandamano tuliyofanya jana yake Jumatano hadi Ofisi ya W/Mkuu kuhitaji kutimiziwa mahitaji yetu ya muda mrefu,ambayo W/Mkuu Pinda aliahidi kututimizia alipokuja chuoni kwetu Tar.15 Jan. 2011.
Sisi wana-informatics dai letu kuu lilikuwa kupatiwa mahitaji yetu muhimu ya kitivo(Special Facult Requirement),dai ambalo halijawahi kutimizwa toka kuanzishwa kwa college hii mwaka 2007.
Ndipo Jumatano ya wiki iliyopita wanafunzi wote wa college hii tukaamua kuandamana hadi Ofisi ya W/Mkuu iliyoko Dodoma Mjini ili kufaham hatma ya madai yetu.Tulipofika ofisini kwake tulipewa majibu ambayo tuliridhika nayo kuwa madai yetu bado yanashughulikiwa na hadi kufikia tar. 6 May 2011 madai yetu yatakuwa yameshashughulikiwa.
Cha kushangaza siku iliyofuata ambayo ilikuwa Alhamis,yalibandikwa majina ya wanafunzi 10 ambao walihitajika utawala na walipofika walipewa barua za kuwasimamisha masomo kwa muda usiojulikana kwa madai kuwa ndio vinara wa maandamano tuliyofanya jana yake J'5 na walitolewa nje ya chuo kwa ulinzi mkali wa Polisi.
Siku hiyo hiyo wanafunzi wa college hii tuliandamana hadi utawala tukishinikizwa wenzetu warudishwe na pia tukaweka azimio la kutoingia darasani hadi hapo wenzetu 10 watakapo rudishwa chuoni.
Msimamo huo wa kutoingia darasani ndipo ukaanza leo Jumatano tar.27 kutokana na mfululizo wa sikukuu toka siku tuliyoweka azimio la kutoingia madarasani.
Katika hali iliyotushangaza wengi,leo Jumatano wakati tukiwa katika mgomo wa kutoingia madarsani,tukaletewa tena list ya wanafunzi wengine 17 ambao utawala imewaona kuwa ndio vinara wa migomo na kuwakabidhi barua za kuwasimamisha masomo;
Hivyo kufanya idadi ya waliosimamishwa masomo kufikia 27.
Napenda kusema kwa niaba ya wana-informatics wenzangu kuwa,tunaipenda na kuitakia mema sana college yetu ,chuo chetu na Nchi yetu kwa ujumla.Lakini njia hii utawala wanayotumia haitakwenda kusaidi kabisa, bali inakwenda kusababisha matatizo makubwa zaidi na zaidi.
Naomba kuweka wazi jambo hili,College yetu ya Iformatics ndiyo College pekee ya UDOM ambayo ilikuwa haijawahi kufanya maandamano yoyote wala mgomo wowote toka ianzishwe na hii inatokana na viongozi wetu ambao walikuwa wakitupa matumaini na kutuongezea moyo wa subira,hivyo kutufanya kuendelea kuwa wavumilivu.
Ila sisi kama wana-informatics tunajiuliza toka college nyingine zifanye maandamano&migomo hatujawahi kusikia kuna hata mwanafunzi mmoja kasimamishwa masomo,lakini sisi tuliofanya peaceful demonstration kwa mara ya kwanza wenzetu 27 wanasimamishwa masomo katika college ya wanafunzi 1200!
Pia wana JF najiuliza, semester iliyopita wahadhiri wa UDOM walifanya mgomo wa kutofundisha kwa muda wa wiki moja wakati walipokuwa wanapigania maslahi yao, lakini hakuna aliyefukuzwa wala kusimamishwa kazi.
Iwaje sisi wana-informatics tunaopigania maslahi yetu,ambayo utawala umeshindwa kuyafuatilia tangu kuanzishwa kwa college hii mwaka 2007,wenzentu wasimamishwe masomo?
Tunasema hatutaacha kuedelea na mgomo wetu wa kutoingia darasani na hatutishiwi na staili ya utawala kutusimamisha masomo, na kama hawawezi kuwarudisha wenzetu wote 27 basi tufukuzeni wote!
Mwisho, wana-informatics tunatoa wito kwa college nyingine zote za UDOM kama Education, Social Science, Humanity na nyinginezo kutuunga mkono katika mgomo huu ili kuweza kuishinda dhuluma hii tunayofanyiwa na utawala.
Msimamo huu ulianza tokea Alhamis ya wiki iliyopita baada ya wanafunzi wenzetu wapatao 10 kusimamishwa masomo kwa madai kuwa ndio waliokuwa vinara wa maandamano tuliyofanya jana yake Jumatano hadi Ofisi ya W/Mkuu kuhitaji kutimiziwa mahitaji yetu ya muda mrefu,ambayo W/Mkuu Pinda aliahidi kututimizia alipokuja chuoni kwetu Tar.15 Jan. 2011.
Sisi wana-informatics dai letu kuu lilikuwa kupatiwa mahitaji yetu muhimu ya kitivo(Special Facult Requirement),dai ambalo halijawahi kutimizwa toka kuanzishwa kwa college hii mwaka 2007.
Ndipo Jumatano ya wiki iliyopita wanafunzi wote wa college hii tukaamua kuandamana hadi Ofisi ya W/Mkuu iliyoko Dodoma Mjini ili kufaham hatma ya madai yetu.Tulipofika ofisini kwake tulipewa majibu ambayo tuliridhika nayo kuwa madai yetu bado yanashughulikiwa na hadi kufikia tar. 6 May 2011 madai yetu yatakuwa yameshashughulikiwa.
Cha kushangaza siku iliyofuata ambayo ilikuwa Alhamis,yalibandikwa majina ya wanafunzi 10 ambao walihitajika utawala na walipofika walipewa barua za kuwasimamisha masomo kwa muda usiojulikana kwa madai kuwa ndio vinara wa maandamano tuliyofanya jana yake J'5 na walitolewa nje ya chuo kwa ulinzi mkali wa Polisi.
Siku hiyo hiyo wanafunzi wa college hii tuliandamana hadi utawala tukishinikizwa wenzetu warudishwe na pia tukaweka azimio la kutoingia darasani hadi hapo wenzetu 10 watakapo rudishwa chuoni.
Msimamo huo wa kutoingia darasani ndipo ukaanza leo Jumatano tar.27 kutokana na mfululizo wa sikukuu toka siku tuliyoweka azimio la kutoingia madarasani.
Katika hali iliyotushangaza wengi,leo Jumatano wakati tukiwa katika mgomo wa kutoingia madarsani,tukaletewa tena list ya wanafunzi wengine 17 ambao utawala imewaona kuwa ndio vinara wa migomo na kuwakabidhi barua za kuwasimamisha masomo;
Hivyo kufanya idadi ya waliosimamishwa masomo kufikia 27.
Napenda kusema kwa niaba ya wana-informatics wenzangu kuwa,tunaipenda na kuitakia mema sana college yetu ,chuo chetu na Nchi yetu kwa ujumla.Lakini njia hii utawala wanayotumia haitakwenda kusaidi kabisa, bali inakwenda kusababisha matatizo makubwa zaidi na zaidi.
Naomba kuweka wazi jambo hili,College yetu ya Iformatics ndiyo College pekee ya UDOM ambayo ilikuwa haijawahi kufanya maandamano yoyote wala mgomo wowote toka ianzishwe na hii inatokana na viongozi wetu ambao walikuwa wakitupa matumaini na kutuongezea moyo wa subira,hivyo kutufanya kuendelea kuwa wavumilivu.
Ila sisi kama wana-informatics tunajiuliza toka college nyingine zifanye maandamano&migomo hatujawahi kusikia kuna hata mwanafunzi mmoja kasimamishwa masomo,lakini sisi tuliofanya peaceful demonstration kwa mara ya kwanza wenzetu 27 wanasimamishwa masomo katika college ya wanafunzi 1200!
Pia wana JF najiuliza, semester iliyopita wahadhiri wa UDOM walifanya mgomo wa kutofundisha kwa muda wa wiki moja wakati walipokuwa wanapigania maslahi yao, lakini hakuna aliyefukuzwa wala kusimamishwa kazi.
Iwaje sisi wana-informatics tunaopigania maslahi yetu,ambayo utawala umeshindwa kuyafuatilia tangu kuanzishwa kwa college hii mwaka 2007,wenzentu wasimamishwe masomo?
Tunasema hatutaacha kuedelea na mgomo wetu wa kutoingia darasani na hatutishiwi na staili ya utawala kutusimamisha masomo, na kama hawawezi kuwarudisha wenzetu wote 27 basi tufukuzeni wote!
Mwisho, wana-informatics tunatoa wito kwa college nyingine zote za UDOM kama Education, Social Science, Humanity na nyinginezo kutuunga mkono katika mgomo huu ili kuweza kuishinda dhuluma hii tunayofanyiwa na utawala.