Wanafunzi wa VETA wafanya ukarabati Muhimbili, Prof. Mkenda apongeza uwezo wao

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda, amesema wanafunzi wa VETA, ambao leo Machi 15, 2025, wamefanya ukarabati kwenye wodi ya watoto ya Hospitali ya Taifa Muhimbili, ikiwemo kupaka rangi, wamekuja kuonesha uwezo wao kutokana na yale wanayojifunza VETA.

"Sisi tunafurahi kwamba wenzetu wa VETA, katika Maadhimisho ya Miaka 30 tangu VETA ianzishwe, wamejipanga kuonesha shughuli ambazo wanaowafundisha wanaweza kufanya. Mojawapo ni kupaka rangi katika maeneo mbalimbali, ambapo sehemu kubwa ni hii (Muhimbili), lakini najua watafanya na Iringa, Tabora, kwenye mashule, zahanati na hospitali," amesema Prof. Mkenda.

"Wanafunzi hawa wanaposoma VETA wanafundishwa vitu vingi, mojawapo ni ujenzi pamoja na kupaka rangi, kwa hiyo wamekuja kuonesha uwezo wao," ameongeza.

Pia, Soma: Waziri Mkuu Majaliwa: Wenye degree kasomeni ufundi VETA mjiajiri

Prof. Mkenda ameyasema hayo wakati wa hafla ya ukarabati wa wodi ya watoto katika Hospitali ya Taifa Muhimbili, uliofanywa na wanafunzi wa VETA kuelekea Maadhimisho ya Miaka 30 tangu kuanzishwa kwake.

Chanzo: TBC Digital
 
Kwahiyo hao waliosoma degree na hawana ajira waende Veta mtawapa hizo tenda?
 
 

Attachments

  • Snapinsta.app_483423170_1071770781641908_3545649834984004154_n_1080.jpg
    126.7 KB · Views: 1
Prof. Adolf Mkenda, Kwenye familia yake,wangapi wapo au wamepitia VETA?
 
Sasa wa darasa la saba anaenda Veta wa form four anaenda veta wa form six anaenda veta wa degree anaenda veta,........sasa tusome nini ili tusiende veta?
U-secretatary kama chura kiziwi,utaikwepa VETA
 
Mwaka huu hatutaki propaganda tena.
Nionyeshwe mtoto wa DAS, RSO, DSO, RPO, RPC, RAS, DC, RC, Mbunge, Waziri ambaye anahangahika huko VETA ili ajikwamue na ukosefu wa ajira au ili akaajiriwe na wachina.
 
Tuendelee kuhimiza wenye degree wakaongeze elimu veta. πŸ˜€πŸ˜€πŸ˜€πŸ˜€πŸ˜€πŸ˜€
 
VETA inakaribisha wenye degree,wezi,mafisadi,makahaba,wavaa kobazi,walokole na mawaziri kuongeza ujuzi mnavyo vifanyia kazi.
kama wewejambazi ukiingia VETA utazidi kupata ujuzi mzuri zaidi
 
I
Sasa wa darasa la saba anaenda Veta wa form four anaenda veta wa form six anaenda veta wa degree anaenda veta,........sasa tusome nini ili tusiende veta?
naonyesha mfumo wa elimu ea Tanzania ni WA ovyo..Inatakiwa CCM na serikali zake ziwajibike kwa kuwapatia Watanzania elimu za nadhalia vyuo vikuuu
 
Sasa wa darasa la saba anaenda Veta wa form four anaenda veta wa form six anaenda veta wa degree anaenda veta,........sasa tusome nini ili tusiende veta?
Kuna kisa kimmoja mtoto mmoja wa kike kuanzia vidudu kasoma boarding school hadi A level hajawahi kupika,kaenda chuoni hadi Masters degree hajui kupika. Alipokuja kuolewa ndipo alijua umuhimu wa kujua mapishi.alijiunga na VETA kujifunza mapishi vinginevyo mume wake alitaka kumpa dispatch letter.
VETA ni maisha na kuna wakati haikwepeki.
 
Nonsense
 
Huyu Prof Mkenda ni sehemu ya tatizo, pengine na yeye angepelekwa VETA angekuwa na "ujuzi" wa kuongoza hii wizara
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…