pingli-nywee
JF-Expert Member
- Sep 16, 2015
- 11,923
- 13,350
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
safi kabisa
Kweli kabisa, ni kiashiria kizuri kwamba kuna mengi mazuri yanayoendelea kwenye sekta ya elimu Kenya. Hawa ni wanafunzi kutoka shule ambayo sio maarufu sana kule vijijini. Ila wamefanikiwa kutumia vitu vya kawaida kwenye mazingara yao, kwa gharama ya shilingi mia tu, kubuni kifaa ambacho kitabadilisha maisha ya walemavu wengi. Hiki kifaa chao cha Essameter ni 'callibrated' na kina alarm, ambayo inalia 'target' ikifikiwa. Kando na kutumika kwenye maisha ya kawaida, majaji wa mashindano hayo wanasema kifaa hicho kitaboresha elimu mashuleni kwa walemavu(vipofu na viziwi) kwasababu kinaweza kikatumika kufunza pia, sanasana kwenye hesabu.Hongera zao, elimu ya Kenya inazidi kupaa.
Kenyans are very ambitious at a personal level.That has what has kept us going even when every odd is against us.Sana. Hawa wanafunzi ni wabunifu kupindukia na wameiwakilisha nchi yao ya Kenya vilivyo. International Science and Engineering Fair(ISEF) ni mashindano ya kimataifa ya kisayansi yanayowashirikisha wanafunzi 1,800 kutoka nchi 75 duniani! Wadhamini wa mashindano hayo ya kila mwaka ni U.N., kupitia shirika lao la U.N. Science and Cultural Organisation na ndio mashindano makubwa kabisa ya kisayansi kwa wanafunzi wa shule za upili duniani. Hiki kifaa chao 'Essameter' ambacho jina lake limeunganisha majina yao Esther na Salome ndio walishinda nacho kwenye 56th Kenya National Science & Engineering Fair 2019. Wakenya waliofuzu kwa mashindano hayo ya kimataifa yaliyokuwa kule U.S.A mwaka huu ni wanafunzi kumi kutoka shule tatu nchini.![]()