Wanahabari Tanzania mmepewa Uhuru, mnakwama wapi?

Wanahabari Tanzania mmepewa Uhuru, mnakwama wapi?

voicer

JF-Expert Member
Joined
Jul 13, 2020
Posts
5,545
Reaction score
11,935
Mmekuwa mkiililia serikali hususan awamu ya tano, iliyopita.

Kwamba ilikandamiza na kuuminya Uhuru wa kuongea na kutoa maoni nchini. Ikiwemo kuminya Uhuru wa vyombo vya habari nchini Tanzania. Sasa ni awamu ya sita chini ya Samia Suluhu Hassan. Ameifungua nchi kimataifa.

Pia amewapa Uhuru wenu pamoja na kuwarudishia waziri wenu mpendwa. Kwenye wizara ile ile mliyokuwa nae mkiulilia Uhuru pamoja. Amekutana na nyinyi na mmewekeana "MOU"

Lakini tukiangalia Kwenye Media Press nchini na kinachoendelea kwa sasa hatuoni tofauti kivitendo. Mambo ni yaleyale kama ilivyokuwa huko tulikotoka. Mlipaswa kuelewa jinsi ya kufanya kazi ya uanahabari katika kipindi hiki. Ili kwenda sambamba na ukuaji mkubwa tena wa kasi waTeknolojia ya mawasiliano Duniani.

Sasa hivi kwa asilimia kubwa Duniani na Tanzania ikiwemo. Watu wengi ni rahisi kujua ni nini kinaendelea popote pale Duniani kutokana na uwepo wa teknolojia ya Simu janja zao. Na inakuwa ni rahisi mtu yeyote kuripoti habari ya tukio kutokea saa hiyo hiyo linapotokea. Kabla hata halijafika kwenye vyombo vya habari.mfano kupitia humu JamiiForums

Waandishi wa habari wa nchi hii. Ili kuiokoa sekta yenu isijifie taratibu kama tunavyoonabikizidi kudorola kwa sasa. Mfano
Kupitia soko linaloyumba la magazeti huko mitaani. Mnapaswa kuacha kulialia sambamba na wanasiasa badala yake mwende mbele zaidi kiuandishi na utafiti wa habari.

Mbadili mfumo wenu wa utendaji kazi.muache mtindo wa kuishia kuripoti matukio na kuishia hapo. Mwende far beyond na kuleta habari za uchunguzi na zenye weledi wa kina sababu nyinyi mmesomea kazi hiyo. Tofauti na sisi tunaoishia kuripoti kile ambacho macho yetu yameona.

Mje na habari zenye muendelezo wa matukio kwa kina na zenye kuihabarisha na kuielimisha jamii yetu. Pale mnapopata nafasi za kufanya mahojiano na viongozi waandamizi nchini.

Wawe wa kiserikali au kisiasa, msiishie kujipendekeza kwa kutanguliza uheshimiwa wao mbele. Bali muuweke pembeni na
muuvae uanahabari wenye weledi kwa kuuliza maswali yenye tija na yanayoihusu na kuigusa jamii kuhusiana na mada husika itakayokuwa mezani. Tena kwa weledi zaidi. Jaribuni kuiga wenzenu wa mashirika ya nje.

Badala ya kushinda mkitafuta udaku na press release zenye kuandamana na bahasha zenye posho. Kisha mkaishia kutuletea habari zilizolalia upande wa watoa Bahasha wazuri. Mwende kwenye jamii huko ndani na kutuletea habari halisi zenye jicho la mwanahabari msomi. Pia muwe mnafanya muendelezo wake.

Mfano!
mliandika na kuripoti tukio la vijana watano waliopotea katika mazingira tata jijini Dar es Salaam mwezi wa December 26/2021.
Baadae hakuna mrejesho wa kilichoendelea mpaka sasa. Ingawa sakata hilo halijapatiwa ufumbuzi mpaka sasa.

Lakini Media zetu hakuna hata moja ambayo imechukua one step ahead na kurudi kwenye zile familia, au kurudi kwenye vyombo husika ili kuwajulisha wananchi na hivyo kuwaondolea taharuki husika kwa kupata mrejesho.

Badala yake mko kawaida mkiendelea kutuletea habari fupifupi tena zingine zenye lugha za kihuni kwa jamii kama. Akinukisha.
Kimenuka hiko kitu. Balaa jingine...

Na mara nyingi maudhui ya habari hayaakisi au kuendana na vichwa vya habari husika.

Nawauliza wanahabari mnakwama wapi?

commonmwananchi
10101
 
Ukweli mchungu kwa sasa habari hazina mvuto, si magazetini hata kwenye luninga. Huu uandishi wa kuripoti matukio tu ni janga. Nina miaka kadhaa sifatilii habari za kwenye media kama magazeti na tv,Kwa sababu naamini nitakutana na upuuzi uleule kila siku: Waziri kasema hivi, serikali imejenga, polisi yaua majambazi nk.
 
Wana habari wamekuwa ni chawa wa waheshimiwa usitegemee jipya kutoka kwao. Walilia kwa magufuli kuwa anaminya sekta ya habari ukweli ni kuwa magu alikuwa hatoi bahasha ya kaki kwao.
 
Ukweli mchungu kwa sasa habari hazina mvuto, si magazetini hata kwenye luninga. Huu uandishi wa kuripoti matukio tu ni janga. Nina miaka kadhaa sifatilii habari za kwenye media kama magazeti na tv, kwa sababu naamini nitakutana na upuuzi uleule kila siku:Waziri kasema hivi, serikali imejenga, polisi yaua majambazi nk.
Huko kwenye luninga ndio tatizo kubwa.

Wao ni kuripoti matukio ya uzinduzi, ajali, migogoro ya ardhi basi.

Kisha wanahamia Bongo flavour mchana kutwa.

Hakuna habari za kina za kuigusa jamii wala nini!
 
Wana habari wamekuwa ni chawa wa waheshimiwa usitegemee jipya kutoka kwao.walilia kwa magufuli kuwa anaminya sekta ya habari ukweli ni kuwa magu alikuwa hatoi bahasha ya kaki kwao.
Hilo pia ni tatizo ila hapo wameingia mtegoni kwa kukubali wanasiasa kuwagawa pande mbili.
 
UHURU WA KUONGEA NA ULE WA VYOMBO VY HABARI UPO

ILA

TUNA MASHAKA NA UHURU WA MSEMAJI AU MWANDISHI HUYO BAADA YA KUTOA YALIYOMO MOYONI MWAKE
 
Waandishi wa habari wa sasa taaluma ni zero.. Unakuta wanaanza habari na kuanza kutoa sifa kwa viongozi wa serikali bila sababu ya msingi..

Utackia.. "Tumpigie makofi mama amejenga zahanti nyingi " badala waingie field kuona gzo zahanati zina vifaa vya kutosha na madactari na nurses kama wapo...

Wenywe wapo wanasifia majengo tu
 
nadhani hili zigo tuwatwishe Jukwaa la wahariri (Tanzania Editorial Forum) wasiwe wepesi wepesi hivi,kupenda kusifia tu.wakubai kupokea na kuchapisha habari,kwa misingi ya habari
 
UHURU WA KUONGEA NA ULE WA VYOMBO VY HABARI UPO

ILA

TUNA MASHAKA NA UHURU WA MSEMAJI AU MWANDISHI HUYO BAADA YA KUTOA YALIYOMO MOYONI MWAKE
Hatutaki ya moyoni mwake tunataka habari za kichunguzi. Ayo ya moyoni ampe mkewe au mumewe.

Wanahabari wasasa wanaandika hisia zao na matamanio yao
 
UHURU WA KUONGEA NA ULE WA VYOMBO VY HABARI UPO

ILA

TUNA MASHAKA NA UHURU WA MSEMAJI AU MWANDISHI HUYO BAADA YA KUTOA YALIYOMO MOYONI MWAKE
Mbona hatuoni hata mmoja anayethubutu ili tujuwe kama ni uhuru bandia?
 
Waandishi wa habari wa sasa taaluma ni zero.. Unakuta wanaanza habari na kuanza kutoa sifa kwa viongozi wa serikali bila sababu ya msingi..

Utackia.. "Tumpigie makofi mama amejenga zahanti nyingi " badala waingie field kuona gzo zahanati zina vifaa vya kutosha na madactari na nurses kama wapo...

Wenywe wapo wanasifia majengo tu
Nadhani woote wameingia kwenye kutafuta teuzi.
 
UHURU WA KUONGEA NA ULE WA VYOMBO VY HABARI UPO

ILA

TUNA MASHAKA NA UHURU WA MSEMAJI AU MWANDISHI HUYO BAADA YA KUTOA YALIYOMO MOYONI MWAKE
Iddi Amini alishawaambia waandishi wa habari wa Uganda you have freedom of expression in this country but your safety is not guranteed..Yaani mko huru kutoa mawazo yenu nchi hii lakini usalama wenu sio garantii
 
nadhani hili zigo tuwatwishe Jukwaa la wahariri (Tanzania Editorial Forum) wasiwe wepesi wepesi hivi,kupenda kusifia tu.wakubai kupokea na kuchapisha habari,kwa misingi ya habari
Tatizo ni kwamba wale jukwaa la wahariri,wamesahau wajibu wao na sasa wameigeuza ile kuwa NGO kimaslahi binafsi zaidi.
 
Hatutaki ya moyoni mwake tunataka habari za kichunguzi. Ayo ya moyoni ampe mkewe au mumewe.

Wanahabari wasasa wanaandika hisia zao na matamanio yao
Huo ndio uhalisia wake mkuu.
Wanawaza maslahi kuliko wajibu wao.
 
Kitu ambacho naweza kuwatetea na baadaye kuwasema hawa jamaa zetu ni hivi; kwanza walio kwenye tasnia husika kila mtu ana njaa kali sana.

So ni vigumu mwandishi akasimamia ukweli anaojua ndiyo wenyewe alafu nafsi inamwambia angalia nyumbani umeacha 1500/-, alafu ending of the month salary ni 300kl, so alipo atakua ukweli ila anapambania bahasha ya kaki.

Mazingira yetu ya uandishi ni magumu mno, ukizingatia hata hao jw huwa wanaitwa kwenye vikao na wakubwa kwenda kupewa semina nk.

Kwenye habari za uchunguzi na developing story hapo unatafuta kiyama chako, kuna mifano halisi hapo nyuma, paskali na wenzake walikuwa na kipindi hot cha kiti moto kilifia wapi, ambapo itv walikopi na kuja kipindi chao nao sijui kilifia wapi, mpaka leo kuna ripoti ya leo but hakina msisimko.

Pasipo kujipendejeza huli mkuu, kila mtu anataka mkate, ukifanya kazi kibabe as strong story, developing story, investigation story nk labda upate bampa media za nje na usigundulike asee!, Kwa sasa hapa bongo ukitaka kuvuna pesa habari za udaku ohoo, utajiri huu hapa, angalia yule binti wa ng'ambo anavyovuna pesa.
 
Mbona hatuoni hata mmoja anayethubutu ili tujuwe kama ni uhuru bandia?
HATA WEWE UNAWEZA KUJARIBU MKUU, TENA UZURI KUNA PLATFORMS NYINGI SANA, SEMA USIKIKE TUONE KITAKACHOKUTOKEA UWE MFANO
 
Back
Top Bottom