Pre GE2025 Wanahabari tutendeeni haki Wananchi wa Iramba Magharibi, mbona kero zetu hamjaziripoti?

Pre GE2025 Wanahabari tutendeeni haki Wananchi wa Iramba Magharibi, mbona kero zetu hamjaziripoti?

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Mliogwa

Member
Joined
Jun 6, 2024
Posts
37
Reaction score
37
Hivi karibuni Mbunge wetu wa Iramba Magharibi na Waziri wa Fedha Dk. Mwigulu Lameck Nchemba alikuja kujiandikisha kwenye Daftari la Kupiga Kura kwa ajili ya uchaguzi mdogo wa Serikali za Mitaa katika Kituo cha Ofisi ya Mtendaji wa Kijiji cha Misigiri kilichopo Kata ya Ulemo wilayani Iramba, Mkoani Singida.

Baada ya kujiandikisha wananchi tuliokusanyika pale tulitoa malalamiko yetu juu ya changamoto mbalimbali ambazo Mbunge wetu hajatatua. Vyombo vya habari vilikuwepo pale tulizungumza kwa uchungu juu ya huyu mbunge wetu ambaye ametusahau kimaendeleo.

Cha kusikitisha HAKUNA MWANAHABARI HATA MMOJA ALIYETOA MALALAMIKO YETU KWENYE VYOMBO VYA HABARI. Habari iliyotoka ni ya mbunge kujiandikisha tu kana kwamba hakuna lingine lililotokea.

Kwa hali hii tutakuwa na uhakika gani wa taarifa zitakazo kuwa zinatolewa kwetu? Hadi sasa tunaamini kuwa wanachotaka wanasiasa ndicho kinacholetwa kwetu na sio uhalisia wa yanayotokea.

INASIKITISHA SANA.

============== ========================

Snapinsta.app_463143969_434903172566222_1550900090723303312_n_1080.jpg

Snapinsta.app_463331487_953737620122004_3791433003037282687_n_1080.jpg

 
Hivi karibuni mbunge wetu wa Iramba Magharibi na waziri wa Fedha Dk. Mwigulu Lameck Nchemba alikuja kujiandikisha kwenye daftari la kupiga kura kwa ajili ya uchaguzi mdogo wa Serikali za Mitaa.
Baada ya kujiandikisha wananchi tuliokusanyika pale tulitoa malalamiko yetu juu ya changamoto mbalimbali ambazo mbunge wetu hajatatua. Vyombo vya habari vilikuwepo pale tulizungumza kwa uchungu juu ya huyu mbunge wetu ambaye ametusahau kimaendeleo.
Cha kusikitisha HAKUNA MWANAHABARI HATA MMOJA ALIYETOA MALALAMIKO YETU KWENYE VYOMBO VYA HABARI. Habari iliyotoka ni ya mbunge kujiandikisha tu kana kwamba hakuna lingine lililotokea.
Kwa hali hii tutakuwa na uhakika gani wa taarifa zitakazo kuwa zinatolewa kwetu? Hadi sasa tunaamini kuwa wanachotaka wanasiasa ndicho kinacholetwa kwetu na sio uhalisia wa yanayotokea.
INASIKITISHA SANA.
Unataka wakose Udc na teuzi nyingine?
 
Ni mwandishi gani wa singida atakayeandika negative kwa mbunge huyo anayeonekana ni mtemi na hakuna wa kumng'oa jimboni mwake? Mwigulu ndio mwanasiasa mwenye nguvu mkoani singida na tanzania kwa ujumla. Labda atokee mwandishi mwenye itikadi za upinzani ndiyo ataweza kuandika negative za mwigulu jimboni kwake
 
Hivi karibuni mbunge wetu wa Iramba Magharibi na Waziri wa Fedha Dk. Mwigulu Lameck Nchemba alikuja kujiandikisha kwenye daftari la kupiga kura kwa ajili ya uchaguzi mdogo wa Serikali za Mitaa.

Baada ya kujiandikisha wananchi tuliokusanyika pale tulitoa malalamiko yetu juu ya changamoto mbalimbali ambazo Mbunge wetu hajatatua. Vyombo vya habari vilikuwepo pale tulizungumza kwa uchungu juu ya huyu mbunge wetu ambaye ametusahau kimaendeleo.

Cha kusikitisha HAKUNA MWANAHABARI HATA MMOJA ALIYETOA MALALAMIKO YETU KWENYE VYOMBO VYA HABARI. Habari iliyotoka ni ya mbunge kujiandikisha tu kana kwamba hakuna lingine lililotokea.

Kwa hali hii tutakuwa na uhakika gani wa taarifa zitakazo kuwa zinatolewa kwetu? Hadi sasa tunaamini kuwa wanachotaka wanasiasa ndicho kinacholetwa kwetu na sio uhalisia wa yanayotokea.

INASIKITISHA SANA.
Waandishi Wana njaa na ni machawa sana! Alishawapa bahaha Ili wasiandike! Halafu huyu mbunge wenu ni Mpuuzi sana!
 
Kama Waandishi wenyewe wa habari hawana hata Mikataba ya kazi, Wala Mishahara ya kueleweka ndiyo watakuwa na ubavu wa kuandika mabaya ya Waziri wa Fedha, ambaye ndiyo mkusanyaji na mlipaji wa Idara zote za Serikali?

Hapo akiwapa bahasha ya shilingi 200,000 Kwa Kila mmoja hakuna atakayefungua mdomo wake kuripoti negative ya Waziri

Nchi ngumu sana hii
 
Back
Top Bottom