Wanairaimba: Dkt. Mwigulu hatununuliagi hata pombe

Wanairaimba: Dkt. Mwigulu hatununuliagi hata pombe

Lyambalyetu

JF-Expert Member
Joined
Apr 6, 2021
Posts
278
Reaction score
255
Baada ya kuwa Mwanza kwa takriban miezi mitatu, juma lililopita nikarejea na kuamua kukusanya ndengu Jimbo la Iramba na hivyo kunilazimu kutembelea vijiji ambavyo wanalima ndengu.

Ndengu ni mojawapo ya zao tunalolima sana Iramba, ukiacha alzeti na zamani vitunguu.

Katika pitapita zangu huko na kuulizia wajihi na umuhimu wa Mbunge wetu wa sasa Dr. Mwigulu. Kwa sasa anatajwa kwa kutokuwa na tabia ya ukarimu kama watangulizi wake akina Shango na Kiula.

Juma Kilimba amabye kwa sasa ni Mwenyekiti wa CCM Mkoa alikuwa ni mtaalamu wa kuhonga lakini hakuwa mkarimu na ndiyo maana ilipofika 2010 alishindwa kiurahis sana na Dk. Mwigulu.

WanaIramba wanadai Mzee Shango alikuwa akiwakuta kwenye klabu anakaa nao na anawanunulia pombe yote pale kwenye Klabu wanainywa wanafurahi na wanaendelea na maisha yao.

Shango na Mzee kiula ndiyo tabia zao zilikuwa zinalandana ingawa Shango alikuwa mkarimu kwa watu wa namna zote.

Upande wa Mwigulu wanadai anajidai sana. Akifika msibani anabaki kwenye gari mpaka aongozwe kushuka na Mlinzi/Msaidizi wake. Kula hivyo hivyo mpaka Mlinzi wake atangulie kula ndiyo naye ale.

Dkt. Mwigulu hatoi fedha kiholela na inaonesha anadaharau sana maisha yao - wakiwa wanakunywa pombe Klabuni anapita tu na ligari lake na kuna wakati aliwahi kuwatimulia vumbi. Wao wanadai kama hanywi angeshuka tu basi anagalau awasalimie na kuwanunulia pombe awaache waendelee kwa furaha zao.

Shango hakuwa mnywaji lakini alikuwa anachukua jagi anazuga kama naye kanywa kwa kuweka mdomoni ilimradi tu achanganyike nao. Sasa Dk. Mwigulu kama yupo hivyo je akija kuwa Rais si ndiyo atakuwa anaishia Singida mjini.
 
Wanafahamu kazi, majukumu na wajibu wa mbunge?
Wanafukiri kugawa pesa kiholela na kununulia watu pemba ni sehemu ya majukumu ya mbunge?
 
Kati ya Shango na Mwigulu nani amewaletea maendeleo zaidi Iramba?
 
Kati ya Shango na Mwigulu nani amewaletea maendeleo zaidi Iramba?
Maendeleo ya WanaIramba yaliletwa na WanaIramba wenyewe. Serikali imechangia kdg sana. Hamna MwanaIramba aliyeachana na nyumba ya tembe alijengewa nyumba ya bati na Mwigulu!
 
Wanafahamu kazi, majukumu na wajibu wa mbunge?
Wanafukiri kugawa pesa kiholela na kununulia watu pemba ni sehemu ya majukumu ya mbunge?
Hebu elezea kidogo kazi na wajibu huo?
 
Huu ni ujinga, na hao wapumbavu wanao omba pombe badala ya mambo muhimu kwa maendeleo ya maisha yao.
Wala hamna ujinga hapo. Kama mjini wanaimba bia tamu kwa nini vijijini isiwe "pombe tamu"? Mambo muhimu kwa maendeleo yao ni yapi sasa - kwani Dr. Mwigulu ana wajibu wa kutujengea nyumba au kutulimia mashamba?
 
Hapahitaji darubini Kali kujua kua mwigulu Ni mtu wa majivuno na kujiskia Sana[emoji3525]
 
Wanafahamu kazi, majukumu na wajibu wa mbunge?
Wanafukiri kugawa pesa kiholela na kununulia watu pemba ni sehemu ya majukumu ya mbunge?
usiwahukumu. hayo yote mwigulu aliyafanya wakati wa kampeni. ukipanda mbegu lazima uitunze.
 
Wanairamba 🏃‍♀️🏃‍♀️🏃‍♀️🏃‍♀️🏃‍♀️

Ifike mahala waanze kutaka kupewa vitu vinavyodumu na vitakavyowaboreshea maisha
 
Mleta mada nimekuelewa umetaka kutueleza hali halisi ya Mwigulu,ni mtu mwenye majivuno,asiejua alipotoka na anaependa kunyenyekewa.Huo ni ushamba binadmu lazima uwe na kumbu kumbu ulipotoka.
 
Hawana la kumfanya Tume ya uchaguzi itamtetea
 
Kwa hiyo mleta mada unataka kusema kuwa Wana Iramba ni walevi Sana. Kumbe zile tabia za dada zenu zinaanzia kwenye tamaduni zenu aisee. Mnapenda Sana Kitonga. Eti mtu ashuke kwenye gari awanunulie pombe😂. Kweli nchi ngumu hii.
 
Tuimbe wote.

Tumeipenda wenyewe, chaguo letu wenyewe nawavimbe wapasuke, watajijua wenyewe.
 
Back
Top Bottom