Mindyou
JF-Expert Member
- Sep 2, 2024
- 1,869
- 4,877
Wanabodi,
Wanawake visiwani Zanzibar wenye sifa wametakiwa kushiriki kikamilifu katika kujiandikisha kwenye daftari la kudumu la mpiga kura katika zoezi ambalo linatarajiwa kufanyika Febuari Mosi hadi Machi 17, Mwaka huu
Wito huo umetolewa na Mkurugenzi Idara ya Wanawake na Watoto Sitti Abbas Mwinyi katika mkutano maalum ulioandaliwa na Taasisi ya Binti wa Leo ukibeba ajenda mahususi ya kuwahamasisha wanawake kushiriki katika zoezi hilo
Amesema baadhi ya wanawake wengi wanashindwa kujitokeza katika kushiriki kwenye zoezi la uandikishaji hivyo amewataka kuhakikisha wanatekeleza haki yao ya msingi ya Demokrasia
Mwenyekiti wa Taasisi ya Binti wa Leo Nahida Abdalla amesema kujiandikisha kwa wanawake wenye sifa ni takwa la kikatiba ili kutekeleza haki yao ya msingi ya kuchagua na kuchaguliwa katika Uchaguzi Mkuu ambao unatarajiwa kufanyika Mwezi Oktoba Mwaka huu
Source: Wasafi FM
Wanawake visiwani Zanzibar wenye sifa wametakiwa kushiriki kikamilifu katika kujiandikisha kwenye daftari la kudumu la mpiga kura katika zoezi ambalo linatarajiwa kufanyika Febuari Mosi hadi Machi 17, Mwaka huu
Wito huo umetolewa na Mkurugenzi Idara ya Wanawake na Watoto Sitti Abbas Mwinyi katika mkutano maalum ulioandaliwa na Taasisi ya Binti wa Leo ukibeba ajenda mahususi ya kuwahamasisha wanawake kushiriki katika zoezi hilo
Amesema baadhi ya wanawake wengi wanashindwa kujitokeza katika kushiriki kwenye zoezi la uandikishaji hivyo amewataka kuhakikisha wanatekeleza haki yao ya msingi ya Demokrasia
Mwenyekiti wa Taasisi ya Binti wa Leo Nahida Abdalla amesema kujiandikisha kwa wanawake wenye sifa ni takwa la kikatiba ili kutekeleza haki yao ya msingi ya kuchagua na kuchaguliwa katika Uchaguzi Mkuu ambao unatarajiwa kufanyika Mwezi Oktoba Mwaka huu
Source: Wasafi FM