LGE2024 Wananchi wa Hai wadai wamefurahia elimu waliyopata kuhusu masuala ya Upigaji Kura

LGE2024 Wananchi wa Hai wadai wamefurahia elimu waliyopata kuhusu masuala ya Upigaji Kura

Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024

Suley2019

JF-Expert Member
Joined
Oct 7, 2019
Posts
2,203
Reaction score
5,610
WAKATI vyama vya siasa vinavyoshiriki uchaguzi wa serikali za mitaa, vijiji na vitongoji vikihitimisha kampeni zake leo, kupisha uchaguzi wa viongozi hao Novemba 27, wananchi wa kwa Sadala, Wilaya ya Hai, mkoani Kilimanjaro, wameeleza kufurahishwa kwao na namna walivyojengewa uwezo na ujasiri wa kushughulika na viongozi wasiowajibika.

Katika mkutano wa utoaji elimu ya mpiga kura, uliofanywa leo na Shirika lisilo la kiserikali la TUSONGE CDO, baadhi ya wakazi wa kwa Sadala wamesema hamasa hiyo imewafungua macho.

Mfanyabiashara wa Soko la Kwa Sadala, Allan Masacky, amesema elimu hiyo imewasaidia kujua ni kwa namna gani watamalizana na wagombea wenye uchu wa madaraka na wanaotafuta uongozi kwa njia ya rushwa.

“Hii hamasa inayofanywa na TUSONGE kuwaamsha wananchi kuchagua viongozi bora na kushiriki mikutano ya kampeni ni nzuri, kwa sababu hatuwezi kuchagua viongozi mzigo wala wala rushwa wanaoshawishi wananchi kuwachagua kwa kuwapa fedha.
 
Back
Top Bottom