A
Anonymous
Guest
Wananchi wa maeneo ya Mwakaleli halmashauri ya Busokelo wilaya ya Rungwe mkoani Mbeya kwa miaka mingi tumeahidiwa kujengewa barabara kwa kiwango cha lami lakini haitekelezwi.
Ujenzi wa Barabara ya Katumba-Mwakaleli-Lupaso mpaka leo haujaanza licha ya kwamba serikali kupitia Mkuu wa wilaya ya Rungwe mwaka jana April 30, 2024 iliitisha mkutano wa hadhara na kumkabidhi Mkandarasi wa kichina barabara hiyo yenye urefu wa km 35.6
Mpaka leo Mkandarasi haonekani wala hakuna mtambo wowote ulioletwa eneo la mradi.
Ni miezi nane sasa tangu mkataba usainiwe ukimya umetawala licha ya wananchi kubomoa nyumba ili kupisha mradi huo.
Mbunge wa jimbo Atupele Mwakibete Hana akiulizwa anakosa majibu.
Ubovu wa miundombinu ya barabara hii inakwamisha maendeleo ya kiuchumi ya wananchi wa maeneo haya ambao ni wazalishaji wakubwa wa mazao ya kilimo na ufugaji Kama viazi, maziwa, Mahindi, chai na mazao ya misitu.
Tunaomba serikali itusaidie ili Mkandarasi aanze kazi ya ujenzi barabara ikamilike kwa wakati.
Ujenzi wa Barabara ya Katumba-Mwakaleli-Lupaso mpaka leo haujaanza licha ya kwamba serikali kupitia Mkuu wa wilaya ya Rungwe mwaka jana April 30, 2024 iliitisha mkutano wa hadhara na kumkabidhi Mkandarasi wa kichina barabara hiyo yenye urefu wa km 35.6
Mpaka leo Mkandarasi haonekani wala hakuna mtambo wowote ulioletwa eneo la mradi.
Ni miezi nane sasa tangu mkataba usainiwe ukimya umetawala licha ya wananchi kubomoa nyumba ili kupisha mradi huo.
Mbunge wa jimbo Atupele Mwakibete Hana akiulizwa anakosa majibu.
Ubovu wa miundombinu ya barabara hii inakwamisha maendeleo ya kiuchumi ya wananchi wa maeneo haya ambao ni wazalishaji wakubwa wa mazao ya kilimo na ufugaji Kama viazi, maziwa, Mahindi, chai na mazao ya misitu.
Tunaomba serikali itusaidie ili Mkandarasi aanze kazi ya ujenzi barabara ikamilike kwa wakati.