#COVID19 Wananchi wanaendelea na majukumu yao, ugonjwa wa COVID-19 kama kiini macho

#COVID19 Wananchi wanaendelea na majukumu yao, ugonjwa wa COVID-19 kama kiini macho

RWANDES

JF-Expert Member
Joined
Jun 12, 2019
Posts
1,788
Reaction score
4,401
Nimetembelea sehemu nyingi za starehe na maeneo mengi ya biashara watu wamejazana na wengine kutovaa barakoa mbaya zaidi wengine walikuwa wakibishana Yanga na Simba jinsi Manara alivyotoka Simba na kuongea na media walikuwa wakitemeana mate hata hawana habari na ugonjwa huo, nilijaribu kuingilia mjadala wao nikagusia kuhusu ugonjwa wa Corona nilichojibiwa nilishangaa sana

Waliniambia Corona haiwezi walipia kodi za majengo wala haiwezi kulipa ada za watoto.

Mbaya zaidi wamesema ni ugonjwa kama magonjwa mengine ukikupata ukifariki ni wewe na maisha yanaendelea!

Nimegusia kuhusu chanjo ya Corona wameniambia hiyo anaijua mkuu wa nchi mbaya zaidi wanasema huwezi kuchanja uendelee kuvaa barakoa kwa hiyo wanasema Mungu ndiye atakayeamua hatima ya gonjwa hili kuondoka nchini

Ndugu zangu katika hali hii Wizara ya Afya bado ina kazi kubwa kuwaelimisha watu ugonjwa huu umekuwa ugonjwa wa HIV maana watu wanashauri kama hujapima na mwenza wako vaa suti lakini waliowengi hawafanyi hivo.

Wananchi wamesema watavaa Barakoa wakienda ofisi za umma maana huko ndio kuna maelekezo lukuki kumbi za starehe hakuna maelekezo hayo
 
Ni lazima waione Corona kiini macho mtu unasema Corona iko kibao wakati yeye mtaani kwake hajawahi ugua au kuuguza au kuzika mtu mwenye corona halafu unataka aelewe kuwa corona ipo tele? lazima apinge
 
Nimesafiri kutoka Dar es Salaam hadi Mwanza, lakini kwenye bus tuliokuwa tumevaa barakoa ni wachache sana na hakuna tangazo lolole lililotolewa na wahudumu wa bus abiria kuchukua tahadhari.

Hata askari wa usalama barabarani, pamoja na kwamba walitusimamisha mara kwa mara, hawakuingia ndani kuwahimiza abira kuchukua tahadhari, bali walikuwa bega kwa bega na dereva au konda.

Tusipokuwa pamoja katika janga hili tutaanguka, tena vibaya sana!
 
Hapo kwenye kiini macho.

Mpaka sasa vifo vinavyotangazwa kila siku tangu dunia iumbwe ni hii COVID 19. magonjwa mengine hayaui? kwa nini kutangaza vifo vya ugonjwa mmoja? je, takwimu zinazotolewa na hao watu wa magharibi ni za kweli?

Chanjo ni hiari.
 
watu hawataki kusikia ugonjwa huo na hawana mda nao ! Wanasema maelekezo yapo ofisi za umma wanasema mbona wafanyakaz haohao wanaonekana kwenye kumbi za starehe bila barakoa na wanaruka na kukanyagana
 
Tunazikana mitaani kwa kuhisi kafa kwa korona?
Serikali ingeweka mfumo wakuweka wazi mtu akiugua au kufa ifahamike ni Corona au kisukari.

Huko ushetu hawasemi nini kilimuondoa marehemu,wamebaki kuaga nje yakilichomo
 
Hayajakukuta unaweza kusema utakalo then ubinafsi kwa wafrika sio Jambo la ajabu kama tatizo halijafika kwake....Kuna rafiki zangu wengi wamepoteza wazazi wao kwa mpigo baba na Mama unaweza kuvaa viatu vya maumivu wanayopata......kiburi cha ujana kisikupe jeuri
 
Serikali ilivyokaa kimya juu ya corona ikifanya watu wafanye conclusion zao
 
Haya mambo kama hayajakukuta unaweza kuongea utumbo wa kila aina. Watu kama nyie inabidi angalau mtu mmoja wa karibu yako apitiwe labda utapata akili kidogo. Hapa ninapoandika mwenzetu yupo kwemye machine ya kumsaidia kupumua halafu kuna wapumbavu mnafanya mzaha.
 
Hayajakukuta unaweza kusema utakalo then ubinafsi kwa wafrika sio Jambo la ajabu kama tatizo halijafika kwake....Kuna rafiki zangu wengi wamepoteza wazazi wao kwa mpigo baba na Mama unaweza kuvaa viatu vya maumivu wanayopata......kiburi cha ujana kisikupe jeuri

Tatizo ni wafanyakazi wa huduma za afya (Madaktari na Wauguzi) wamekumbwa na kasumba ya UVIKO-19 wakati magonjwa mengine ni tishio kwa afya na uhai wa watu.

Nina mifano ya watu kadhaa waliopoteza maisha hospitalinu wakisubiri majibu ya UVIKO-19 baada ya kudhaniwa wameambukizwa. Matokeo ya majibu yakaja hasi wakati wamekwisha kata roho.

Yawezekana wazazi wa rafiki zako nao wakawa "victims" wa tatizo kutokupewa huduma stahiki kwa dhana kuwa wameambukizwa
 
Haya mambo kama hayajakukuta unaweza kuongea utumbo wa kila aina. Watu kama nyie inabidi angalau mtu mmoja wa karibu yako apitiwe labda utapata akili kidogo. Hapa ninapoandika mwenzetu yupo kwemye machine ya kumsaidia kupumua halafu kuna wapumbavu mnafanya mzaha.
Wanaumwa magonjwa mengine mnasingizia corona,corona mafua tu.

Ukienda hospitalini hukosi wagonjwa wanaopumulia gas.machine za kupumulia zipo toka enzi hizo hazijaanza kufanya kazi baada ya corona kwanini kila mtu akiwa kwenye machine muone ana corona?
Magonjwa ya kusumbua kupumua yapo mengi na yote yakizidi machine ndio hua kazi yake
 
Haya mambo ya chanjo bado watu hawajayaelewa.
Na itakuwa taabu sn kuelewa chanjo kwa sasa.

Hata wazee wa zamani wa kiafrica walipoletewa utamaduni wa kujisaidia kwenye vyoo ilikuwa shida tupu, tena, ugomvi ulikuwa mkubwa sn zaidi ya hili la chanjo. Walishazoea kujisaidia maporini.

Na hili la chanjo linahitaji muda watu wajitafakari
 
Ni jambo la kuomba mungu kama hujaipata corona mzee hapa,nmepigwa nayo siku 3 nilikuwa niko ndani tu kuoumua shda kifua ndo usiseme hapa navyoongea siskii harufu yoyote wala ladha
 
ni jambo la kuomba mungu kama hujaipata corona mzee hapa,nmepigwa nayo siku 3 nilikuwa niko ndani tu kuoumua shda kifua ndo usiseme hapa navyoongea siskii harufu yoyote wala ladha
Pole sana mkuu
 
Nimetembelea sehemu nyingi za starehe na maeneo mengi ya biashara watu wamejazana na wengine kutovaa barakoa mbaya zaidi wengine walikuwa wakibishana Yanga na Simba jinsi Manara alivyotoka Simba na kuongea na media walikuwa wakitemeana mate hata hawana habari na ugonjwa huo, nilijaribu kuingilia mjadala wao nikagusia kuhusu ugonjwa wa Corona nilichojibiwa nilishangaa sana

Waliniambia Corona haiwezi walipia kodi za majengo wala haiwezi kulipa ada za watoto.

Mbaya zaidi wamesema ni ugonjwa kama magonjwa mengine ukikupata ukifariki ni wewe na maisha yanaendelea!

Nimegusia kuhusu chanjo ya Corona wameniambia hiyo anaijua mkuu wa nchi mbaya zaidi wanasema huwezi kuchanja uendelee kuvaa barakoa kwa hiyo wanasema Mungu ndiye atakayeamua hatima ya gonjwa hili kuondoka nchini

Ndugu zangu katika hali hii Wizara ya Afya bado ina kazi kubwa kuwaelimisha watu ugonjwa huu umekuwa ugonjwa wa HIV maana watu wanashauri kama hujapima na mwenza wako vaa suti lakini waliowengi hawafanyi hivo.

Wananchi wamesema watavaa Barakoa wakienda ofisi za umma maana huko ndio kuna maelekezo lukuki kumbi za starehe hakuna maelekezo hayo
Nawapongeza SANA wananchi wenzangu wote tulio na hekima ya namna hii. Ugonjwa wa korona ni uongo, danganya toto na mradi wa globalists uliojaa hila na upuzi mtupu.
 
Back
Top Bottom