GoldDhahabu
JF-Expert Member
- Apr 29, 2023
- 7,189
- 10,375
Huu ni utafiti usio rasmi! Yeyote mwenye mashaka aingie "field" kujiridhisha.
Watanganyika hawautaki kwa sababu hawakushirikishwa. Rais wao wa wakati huo alijiamulia mwenyewe bila kujali matakwa ya wananchi wengi.
Wazanzibar ndiyo kabisa, hawataki hata kuusikia. Nao kama wangeshirikishwa inawezekana wasingeukubali.
Kwa ufupi, ni viongozi wa Tanganyika na Zanzibar ndiyo walioungana na si nchi zao wala watu wao! Ndiyo maana imeshindikana kuuzika Uzanzibar na Utanganyika.
Mitazamo ya sasa kwa kada tofauti kuhusiana na Muungano:
1. Watanganyika: Serikali moja, au Serikali tatu, au kila mmoja abaki na nchi yake
2. Wazanzibar: Serikali tatu au Muungano uvunjwe
3. Watawala Watanganyika: Serikali mbili, ikishindikana, basi Serikali moja.
4. Watawala wa Zanzibar: Serikali tatu au Muungano uvunjwe.
5. Wasomi: Serikali tatu.
6. CHADEMA, ACT WAZALENDO, CUF, NCCR MAGEUZI na vyama vingine vya upinzani: Serikali tatu
7. CCM: Serikali mbili au moja na si vinginevyo
Kwa sura hiyo, ni wazi kuwa Watanganyika na Wazanzibar hawautaki muundo wa Muungano wa sasa wa Serikali mbili. Ili Muungano uendelee kudumu, sharti hitaji la wengi lizingatiwe: Serikali tatu.
PIA SOMA
- Muungano wa Tanganyika na Zanzibar: Una faida gani na kwa manufaa ya nani?
Watanganyika hawautaki kwa sababu hawakushirikishwa. Rais wao wa wakati huo alijiamulia mwenyewe bila kujali matakwa ya wananchi wengi.
Wazanzibar ndiyo kabisa, hawataki hata kuusikia. Nao kama wangeshirikishwa inawezekana wasingeukubali.
Kwa ufupi, ni viongozi wa Tanganyika na Zanzibar ndiyo walioungana na si nchi zao wala watu wao! Ndiyo maana imeshindikana kuuzika Uzanzibar na Utanganyika.
Mitazamo ya sasa kwa kada tofauti kuhusiana na Muungano:
1. Watanganyika: Serikali moja, au Serikali tatu, au kila mmoja abaki na nchi yake
2. Wazanzibar: Serikali tatu au Muungano uvunjwe
3. Watawala Watanganyika: Serikali mbili, ikishindikana, basi Serikali moja.
4. Watawala wa Zanzibar: Serikali tatu au Muungano uvunjwe.
5. Wasomi: Serikali tatu.
6. CHADEMA, ACT WAZALENDO, CUF, NCCR MAGEUZI na vyama vingine vya upinzani: Serikali tatu
7. CCM: Serikali mbili au moja na si vinginevyo
Kwa sura hiyo, ni wazi kuwa Watanganyika na Wazanzibar hawautaki muundo wa Muungano wa sasa wa Serikali mbili. Ili Muungano uendelee kudumu, sharti hitaji la wengi lizingatiwe: Serikali tatu.
PIA SOMA
- Muungano wa Tanganyika na Zanzibar: Una faida gani na kwa manufaa ya nani?