Wanandoa wasisitizwa kupima ukimwi

Wanandoa wasisitizwa kupima ukimwi

Rutashubanyuma

JF-Expert Member
Joined
Sep 24, 2010
Posts
219,468
Reaction score
911,184
Wanandoa wasisitizwa kupima ukimwi


Na David John

SERIKALI ya Marekani kupitia Shirika lake la Misaada (USAID) kwa kushirikiana na shirika lisilokuwa la kiserikali nchini Engender Health kupitia mradi wa
Champion wamezindua programu mpya kwa wanandoa kujenga tabia ya kupima UKIMWI na kupanga uzazi ili kujenga familia iliyo bora.

Akizungumza Dar es salaam wakati wa uzinduzi wa programu hiyo jana, Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Bi. Blandina Nyoni alisema kuwa virusi vya Ukimwi (VVU) na Ukimwi ni moja ya matatizo makubwa kwa Tanzania na hii inatokana na kutokuwa na tabia ya kupima mara kwa mara na wanandoa kutokuwa na uaminifu katika mahusiano yao ndani ya nyumba.

"Kupitia Valentine Day (Siku ya wapendanao) nawaasa Watanzania hasa wanandoa kukaa pamoja kupanga malengo yao na kuwa waaminifu katika ndoa na kujenga tabia ya kupima mara kwa mara na kushirikishana katika maamuzi mbalimbali ndani ya nyumba," alisema.

Pia alisema katika utafiti uliofanywa kuhusiana na Ukimwi pamoja na malaria mwaka 2007 na 2008 ilionyesha asilimia 6.6 kwa wanawake walio katika ndoa wameathiriwa na tatizo wakati kwa wanaume ni asilimia 4.6.

Mwakilishi kutoka Marekani, Bi. Jens Schules alisema nchi yake kwa kutambua jitihada za serikali ya Tanzania wanaunga mkono na kusaidia katika kupambana na Ukimwi pamoja na malaria kupitia mradi wa Champion, na kuwataka Watanzania kutumia siku ya wapendanao kukaa pamoja kupanga mambo mbalimbali ya kimaendeleo ikiwa pamoja na uzazi ili kujenga familia iliyo bora.
 
Ukweli usiopingika ni kuwa kabla wapenzi hawajaamua kuoana wengi utakuta walikuwa ni mafundi kwa kiguu kwa njia: Kumega au wamegaji wazuri...............................na wengineo magwiji wa kuwamegea wengineo........................hivyo wengi wetu bila ya kukusudia utakuta wapo kwenye mtandao wa VVU ..................................hivyo wazo hili limekuja wakati mwafaka..........................na kwa kuongezea tuhimize sheria ya wachumba kupimwa kupimwa kabla ya kufunga ndoa.........................
 
Ukweli usiopingika ni kuwa kabla wapenzi hawajaamua kuoana wengi utakuta walikuwa ni mafundi kwa kiguu kwa njia: Kumega au wamegaji wazuri...............................na wengineo magwiji wa kuwamegea wengineo........................hivyo wengi wetu bila ya kukusudia utakuta wapo kwenye mtandao wa VVU ..................................hivyo wazo hili limekuja wakati mwafaka..........................na kwa kuongezea tuhimize sheria ya wachumba kupimwa kupimwa kabla ya kufunga ndoa.........................

Watu hawataona kwa mwendo huu
 
Haya tunawashukuru kwa hamasa tutajitahidi ila hiyo mara kwa mara sijui ndio ngapi sasa...
 
Back
Top Bottom