Wanaopenda Ugomvi Kwenye Daladala Mara Nyingi Wana Msongo Wa Mawazo

Wanaopenda Ugomvi Kwenye Daladala Mara Nyingi Wana Msongo Wa Mawazo

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
2,780
Reaction score
6,607
DSC01065.JPG
Salama wadau, kuna mambo ambayo binafsi naona hayapo sawa, inawezekana tunayachukulia poa lakini ukiyatazama kwa undani ni wazi kuna kitu hakipo sawa katika maisha ya Wabongo wengi.

Tangu zamani inajulikana ndani ya daladala ni sehemu ya vituko vingi, kuna matukio mengi kwa kuwa asilimia kubwa wanaotumia ni wale wenzangu na mimi wenye ipato cha chini na kipato cha kati.

Nasema hivyo kuwa kuwa ni watu wachache sana ambao wana kipato cha juu wanatumia usafiri huo, japo inapotokea kwa asilimia ndogo.

Hiyo inatokana na hadha zilizopo katika usafiri huo wa umma, kwanza ni wa shida hasa mida ya asubuhi na jioni ambapo kunakuwa na mzunguko mkubwa wa watu wengi kutoka na kurejea nyumbani au kwenda vibaruani.

Ugomvi, lugha kali, dharau, kubanana, kuibiana, kutomasana, kupapasana, lugha za kukera, ni baadhi ya mambo ambayo sisi wapanda daladala, mwendokasi, Bajaj tunakutana nayo.

Ndiyo maana wanasema ukitaka kupata au kuona vituko vingi wewe banda daladala au mwendokasi hasa mida niliyotaja jioni au asubuhi.

Changamoto niliyoiona ni kuwa kuna watu wengi sijui ni stress au tabia zimebadilika, au maisha magumu au ni nini hasa! Kuna ugomvi mwingi unatokea bila sababu za msingi na unaweza kukwepeka lakini bado inatokea.

Wiki iliyopita nikiwa kituoni, ilikuja daladala watu wakiwa wengi, wakaanza kugombania, mbaba mmoja (miaka 35-40) akaweka begi lake kwenye siti yeye akiwa nje.

Alipoenda kugombania akafanikiwa kuingia, kufika kwenye ile siti akamkuta mdada amekaa, akaanza kulumbana naye atoke mdada akagoma, wakati hayo yakitokea kulikuwa bado kuna siti kama sita hivi zipo wazi nyuma ya hiyo siti wanayoigombania.

Sasa bahati nzuri gari ikawa haijajaa kumbe abiria wengi hawakuwa wakienda ‘route’ hiyo, hivyo siti zikawa nyingi, lakini yule ‘mwamba’ akakomaa na dada wa watu mpaka wakaanza kuvutana, ikawa mbinde kwelikweli.

Jamaa anamvuta mdada wa watu kama ile siti ni mali yake vile, wakati nyuma kuna siti kibao zipo wazi, tuliokuwa pembeni tukajiuliza huku mwamba ni stress au ameweka nini kwenye hiyo siti.

Niishie hapo siku mbili baadaye likatokea tukio kama hilo katika daladala nyingine nikilishuhudiA.

Juzi kati tena nikiwa kwenye basi la kwenda mkoani ikatokea sekeseke kama hilo, jamaa kakaa kwenye siti ambayo siyo namba ya tiketi yake, akaja mwenye siti yake ambaye ni mdada, mzee baba akagoma kutoka.

Yaani inachekesha lakini inashangaza, ilibidi wahudumu wa basi watumie nguvu kubwa kumtaka jamaa aondoke kwenye siti, akawa anagoma, ikabidi wafikie hatua ya kutishia kumshusha kwenye basi kwa kuwa ndio kwanza lilikuwa kituoni likijiandaa kutoka, ndipo akakubali kishingo upande.

Sasa hivyo ni mifano michache tu, njua hata wewe unayo mingine mingi, hivi najiuliza, sisi Watanzania ni nini hasa kinatusumbua kichwani, ni stress za maisha au basi tu watu wameamua kujitoa akili?

Naamini wengi mmekutana na matukio ya aina hii au mengine yanayoonesha wazi vichwa vya Wabongo vipo lesi.

========================

MWANASAIKOLOJIA ASEMA WANA MSONGO WA MAWAZO

Mwanasaikolojia Sylvia Sostenes ambaye pia ni Mwenyekiti wa Taasisi ya Thamani Yangu Initiative inayotoa huduma za kisaikolojia kutoka Ubungo Jijini Dar es Salaam anazungumzia sababu za kutokea mivutano katika usafiri wa umma:

“Imekuwa ni kawaida kutoka matukio hayo hasa katika miaka ya hivi karibuni, asilimia kubwa hiyo inatokea kwa kuwa wahusika wana matatizo ya kisaikolojia.

“Wapo wanaofanya hivyo kwa kuwa wanakuwa wameshindwa kumaliza tofauti zao za walipotoka, hivyo wanakwenda kulipuka sehemu ambzo wanazimudu, na sehemu hizo wanajua ugomvi hautakuwa wa watu wawili.

“Wanajua akifanya ugomvi kwenye umma atapata sapoti ya watu au watu kuingilia na hautakuwa mkubwa.

“Unakuta mtu ameambiwa sogea kidogo au amechelewa kukupa nauli, mtu anakuja juu kwa kuwa ana hasira zake ambazo alishindwa kuzitoa huko alikotoka.

“Hali hii siyo tu kwenye usafiri, bali sehemu nyingi zenye msongamano wa watu kama sokoni, shuleni, hospitali na kwingineko.

“Nashauri wanaokuwa na msongo wa mawazo au wenye kawaida ya kufanya hivyo ni vema mtu akajifunza kutafuta utatuzi wa matatizo yake na siyo kutegemea kutoa msongo wake wa mawazo kwenye maeneo ya watu wengi.”
 
Daladala sio kila anayependa Hana hela ya kununua babywalker
 
Dunia ni msongamano wa watu wenye akili tofauti na penye wengi pana wengi......jitahidi kwa kadri ya uwezo wako kuepukana na malumbano na maugomvi ya kipuuzi sehemu yoyote........

 
Nakumbuka ilikuwa 2016 hivi mitaa ya tabata asubuhi nawahi town. Nimepanda daladala inayotoka town nakwenda kugeuza nayo kimanga sababu ya wingi wa watu ile asubuhi nisikose siti na kupuka mikanyagano na mibabano isiyo ya lazima.

Maeneo ya mawenzi akapanda bi dada fulani wa umri wa kama 34+ hivi. Konda anapiga debe akiwaambia abiria kuwa siti zipo watu wanashuka mwisho kimanga. Asilojua ni kuwa wale ambao walikuwa wakiingia walikuwa wanawaomba siti wanaoshuka wawape msaada kabla gari haijajaa na mtifuano wa kugombea siti haujaanza.

Tukafika kimanga mwisho abiria kadhaa waliosimama wakashuka wengine walibaki maana walikuwa wamekosa siti ila wanaenda town. Bi dada alikuwa miongoni mwao.

Safari ya kwenda town ikaanza konda anakusanya nauli. Alipomfikia bi dada kuliwaka moto. [emoji23][emoji23][emoji23]

Bi dada alikuwa na hasira anaongea kama amepandisha mashetani anamuuliza konda kama alijua hakuna siti kwann aliwaambia wapande na daladala kibao tunapishana nazo zinaenda kimanga na ni tupu zinafanya kushindana kuita abiria. Konda akawa anamjibu kwa kumkera tu kuwa kama anaona issue sana ashuke akawa anataka mrudishia nauli ila pungufu ya ile aliyotoa. Maana daladala zinatoza nauli ya kugeuza na gari hata kama umepanda kituo kimoja tu kabla ya kufika mwisho.

Bi dada akazidi kumind. Yaani hadi machozi yanamlenga usoni jinsi alivyofura kwa hasira.

Sasa kwa wakati huo gari zima wakawa wananong'ona na baadhi wanamsema konda kuwa ni kweli kamkosea huyo dada. Basi kwa busara ya kiutu uzima, kwakuwa yule dada alikuwa amesimama usawa wa siti ya nyuma ya siti niliyokuwapo nikaona nifanye utu. So nikaongea na jamaa pembeni yangu kuwa namwita huyo dada aje kukaa siti nilipokuwa hapo dirishani asisogee ili huyo dada aje kukaa hapo siti ya dirishani.

Basi jamaa akamwita bidada me nikamwambia njoo ukae dada jamaa amekukwaza sana. Bila kujibu akawa ananitazama yale macho ya kustaajabu kuwa unashuka nikamwambia aje akaanza kusogea na jamaa akakaa kiubavu bi dada akaja akapita kuketi. Me nikasimama.

Kuna kitu nilihisi cha tofauti siku ile ndani ya nafsi na ndio maana huwa nawapa watu hii story mara kwa mara. Yule dada alikaa naona akasahau maumivu yake ghafla maana siku yake naona tokea alipotoka haikuwa nzuri.

Muda huo huo kabla hata hatujaenda mbali nikasikia mtu siti ya mbele nyuma ya siti ya dreva (daladala ni coaster mayai) ananiita kuniambia nikaketi pale alipo. Alikuwa anashuka kituo cha alfarouq. Abiria walishaelewa mchezo maana waliona matukio yote haya na wao wakawa waungwana kunipisha nikaketi pale. Waswahili wanasema tenda wema uende zako ila me nakuongezea tenda wema uwavute watu wema kwako na wema ukufuate popote uendapo.

Nikaketi.katika siku nilijiona shujaa ni siku ile. Abiria walikuwa wote wakizungumza na kumlaumu konda kwa kuleta taharuki isiyo ya lazima na pia kufedhehesha mtu ambaye hamjui na badala ya kusaidia akaishia kumuongezea hasira kwa kumjibu shombo. Upande mwingine walifurahishwa na kitendo cha mimi kumpisha yule dada ambae simfahamu na kujali hali yake ya kupanic kumsaidia kupata haki yake kitu ambacho hata yy muhusika hakukitegemea hata kidogo.

I hope yule dada alijifunza kitu siku ile. I hope anapokutana na mtu ambaye anaweza msaidia basi hatosubiri kuombwa ila atajitoa kumsaidia bila kuangalia yeye binafsi atapata nini.

Hii siku huwa siisahau nikikumbuka namba yule dada alipokuwa anaongea na konda kwa maumivu halafu konda anamjibu kwa kumpuuza na kumtibua zaidi halafu baadae akaamua kukaa kimya na kuugulia maumivu akijua tayari alichotarajia kimefeli na siku yake imeshakuwa mbaya.
 
Kwa nini upande daladala? Nunua hata ka baiskeli ili uwe na usafiri wako yaani hutabishana na mtu awaye yote, ukiwa na ka baby walker ama ist utagombana na watu pia hasa wauza mafuta 😂
 
Watu huwa wana hasira zao, kuna mmoja jana kanijibu, umeona unikalie kabisa, nikamwambia sogea hataki. Ikabidi nihame siti
 
Ukweli mtupu, yani jana tu kuna mama mmoja alimshukia kama mwewe Konda kisa nauli imepanda, alifoka gari zima anasikika yeye nilibaki nacheka...
 
Nimenunua hii ili nikwepe gharama za mafuta kipindi hiki naambiwa eti ni baiskeli ya watoto...mimi mzee kijana sifai kuendesha?

IMG_0199.jpg
 
Back
Top Bottom