Wanaopinga mahakama Kadhi "Intellectual Arguments" only

Status
Not open for further replies.

Topical

JF-Expert Member
Joined
Dec 3, 2010
Posts
5,173
Reaction score
938
Assume wewe ni muislam na una wake watatu na watoto 5:4:3 yaani 12 jumla kwa wake watatu..umefariki

Kwa sheria za ndoa ya 1971; ugawaji wa urithi huo hauwezekani japo muislam huyu aliruhusiwa kuoa kiislam

Kwanini mali yake isigawanywe kiislam?? tunataka kadhi wawasaidie hao wanawake, watoto kuhusu mgawanyiko wa mali ya muumini huyu.. siyo voluntarily iwe sheria kabisa na hukumu itolewe na mahakama..ok

Ndio maana tunataka mahakama ya Kadhi..

NB: Naomba wale wenye hasira na uislam na waislamu watuache kwanza tuseme kwanini tunataka mahakama ya kadhi ili mtuelewe
 
Wewe umekimbia kule thread unakuja huku kuanzisha thread ile ile!!?? Mods funga hii Thread tafadhali inajaza server JF bila sababu za msingi... Bwana Topical nakuomba urudi kule kwenye ile thread ulioikimbia na uwache kuwachanganya Members humu JF.
 
Ingawa hili si jukwaa la dini lakini kwani kuna mtu amewazuia kuanzisha mahakama yenu labda hukumwelewa rais soma hapa

 

yaani mnataka mtandao wa mahakama nchi nzima kwa sababu ya masuala ya urithi tu, halafu hapo hapo mnataka serikali igharamie mahakama, NO HELL NO! wekeni bayana hizo taratibu zenu za urithi na zitaamuliwa na mahakama ya kawaida, mkianza hivyo watakuja wamasai n.k nao watataka mahakama zao, na madhehebu mengine nayo yatadai wana taratibu zao za kutoa haki nao watataka mahakama zao, sasa hapo itakuwa utawala wa sheria au vurugu mechi? Hata hivyo rais jk the 2nd katika baraza la idd liliadhimishwa dodoma kwenye msikiti wa gadaffi alisema ni ruksa mahakama ya kadhi kuanzishwa ila serikali haitokuwa na mkono wake wala kujihusisha katika kugharamia na iwe hiyari kwa atakae si kulazimisha hata kama ni muislam.
 
mahakama ya kadhi ya nini?na sisi wakristo basi tupeni mahakama ya kikristo'badala ya kukaa na kuangalia nchi inapelekwa wapi na wajanja wachache mnaleta mambo ya ovyo'nchi hii haina dini'anzisheni mahakama ya kadhi bila kushirikisha serikali ya wakristo na waislam
 
Ingawa hili si jukwaa la dini lakini kwani kuna mtu amewazuia kuanzisha mahakama yenu labda hukumwelewa rais soma hapa
Mkuu, JK sii Mungu wala Katiba.. tunachofuata ni katiba inasema nini na maadam katiba inatambua sheria za asili kwa nini wasiwe na mahakama inayojali na kutafsiri sheria hizo. Sheria ya nchi itambue ndoa ya wake wanne lakini matatizo ya ndoa hizo yaamuliwe kienyeji wakati sheria zipo? -Ndivyo unavyotaka kusema!
 
We Topical, kama umemsoma Feedback na hujaridhika ukate rufaa, sio kuleta upya mijadala iliyokwishatolewa ufafanuzi wa kina kwa wenye uelewa: Hakuna aliyepinga kuanziswa kwa mahakama yenu, anzisheni kulingana na taratibu za dini yenu.
Msitake kila kitu kuanzishiwa na serikali kwa kodi za wananchi.
Pili kama ulivyosema kuwa suala hili ungependa mjadili ninyi waislamu tu, ni ruksa ila mngeweza kufanya hivyo zaidi msikitini badala ya kuleta hapa JF
 
Kama kweli unataka so called "Intellectual Arguments" basi ungeweka hii mada kwenye jukwaa la sheria ili watu wajadili kisheria sheria na kikatiba katiba. Zaidi ya hapo itakuwa n ihisia na ushasbiki wa kidini. ukichanganywa na siasa.

Mimi comment yangu moja tu kwenye uzi niulize wachangaji wote watakapenda kuchangia na mleta mada

je wewe kama ungekuwa mwanasheria mkuu wa serikali uko tayari kurushu na kumshauri raisi akubali kuingiza rasmi mfumo wa mahakama za mila za wajaruo, wahaya, na makabila mengine kwenye mahakama ya JMT.

NB
Agalizo kuna mila zina utaratibu wao mfano wa mirathi
 

Nimeuliza tatizo lenu nini hasa?
Kama ni fedha serikali inalipa mahakimu sasa kwa kuendesha kesi za waislamu ambazo wanakosea sana hukumu

Kwa hiyo kukiwa kadhi hela hiyo hiyo inayotumika sasa ndio itatumika ok

usiwe na wasiwasi na hela ok..

naomba solution ya mambo haya niloyaeleza hapo juu..
 

ni makosa kulinganisha wahaya na uislam ok..
 
Kama ndoa mliifunga kwa imani ya dini fulani, na kwa imani hiyo mnataka kugawana urithi tatizo lipo wapi kutumia taratibu za dini hiyo mpk mpelekane mahakamani? Ukiona mtu hataki utaratibu wa dini ktk kugawana mirathi basi ina maana haitaki na dini yenyewe. Huu ni utaratibu wa kulazimishana kufanya mambo kwa nguvu.

Mbona ndoa hamfungii mahakamani?
 
ni makosa kulinganisha wahaya na uislam ok..

Kwa mtazamo wako, lkn yote ni makundi tu. Kama wewe unavyodai haki ya dini na wengine watasema wao ndoa zao wanataka ziamuliwe kihaya. Kwa hiyo zianzishwe mahakama za kihaya kwa kuwa zilizopo hazina utaalam wa kuamua mila za kihaya. Au unataka kuleta zipi?
 
Mtoa mada unachekesha kweli yaani mahakama ya kadhi kwa ajili ya ndoa sita saba kumi.....? kwani wewe unapoa zaidi ya mke mmoja tayari ni tatizo kwa nini usijiandae mapema kabla mungu hajafanya maamuzi yake na mahakama ya Jamhuri ya Muungano itawatendea haki uliowaacha nyuma. Jaribu kufanya research kwa nchi zote ambazo zina mahakama ya kadhi kama hao wajane au watoto walipata haki yao baada ya baba/mume kufariki? Next??????!!!!
 

Twende hatua kwa hatua. Hao wake watatu ulifunga nao ndoa mahakamani?
 

Hivi ni vidume vyenye hila tu hakuna lolote. Nia na madhumuni ni kumnyang'anya mjane mali ya mumewe na kuigawa kwa familia nzima. Eti mimi nife leo, mali yangu badala itumike kumpa nguvu mke wangu kulea watoto niliomwachia ianze kugawanywa kwa kaka zangu na vibabu ambavyo si jukumu langu kuvilea. Vitu vingine ni very illogical
 

kudai mahakama ya kaz kwasababu ya urithi ni mawazo finyu na ya kimasikini! Hoja hasa si kwamba mahakama ya kadhi inapingwa, swala ni muundo wa makakama uliopo uliotokana na the magistrate court Act 1962 hauwez ku adapt mahakama ya kadhi. After all kama hoja ni kutimiza matakwa ya kidini, nadhan bado matakwa hayo xanaweza kutimizwa kwa kutumia forum nyingine.
 
Topical anatetea ajira yake jamani, yumo kwenye list ya makadhi pamoja na vile vizee vinavyoshinda kwenye mabao na kahawa na kuoa wake wengi, wanataka warambe ajira serikalini kilaini bila jasho la kufuta umande
 

Kama hawataki kwenda mahakama hizi za kawaida (kwasababu za imani yao na wao ni watanzania) tuwafanyeje?? acha ushabiki nataka intellectual arguments
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…