GENTAMYCINE
JF-Expert Member
- Jul 13, 2013
- 60,660
- 121,325
Kila siku tunalalamika tu kwamba Tanzania haina Wakimbiaji wazuri wa Marathon ili waweze kutuwakilisha vyema katika mashindano mbalimbali huko Ulaya na hata hapa Afrika hivyo basi nina uhakika Siku ya Kesho tarehe 26 April, 2018 katika maeneo mbalimbali ya Miji nchini Tanzania tunaweza kuwapata akina Filbert Bayi na Juma Ikangaa wengi na huwezi jua hata Mrithi wa Usain Bolt kwani nina uhakika kutakuwa na mbio ndefu na fupi za ' Kutukuka ' ambazo hata Olympic hazijawahi kuwepo.
GENTAMYCINE nitakita Kambi yangu Dar es Salaam ili kuvivumbua hivyo nitaomba na Members wengine pia waliopo sehemu mbalimbali za mijini huko Mikoani nanyi Kesho mnisaidie kuvivumbua Vipaji vingine huko ili baada ya Siku ya Kesho tukaviwakilishe katika Shirikisho za Mbio za Ridhaa na Kulipwa nchini Tanzania kusudi viweze kutumika kuiletea ' Medali ' Tanzania katika mashindano makubwa yajayo.
Nawasilisha.
GENTAMYCINE nitakita Kambi yangu Dar es Salaam ili kuvivumbua hivyo nitaomba na Members wengine pia waliopo sehemu mbalimbali za mijini huko Mikoani nanyi Kesho mnisaidie kuvivumbua Vipaji vingine huko ili baada ya Siku ya Kesho tukaviwakilishe katika Shirikisho za Mbio za Ridhaa na Kulipwa nchini Tanzania kusudi viweze kutumika kuiletea ' Medali ' Tanzania katika mashindano makubwa yajayo.
Nawasilisha.