‘Wanaotawaliwa’ na wake zao huishiwa nguvu za kiume………………!

Mtambuzi

Platinum Member
Joined
Oct 29, 2008
Posts
8,809
Reaction score
15,421
Ugunduzi mpya unaonyesha kwamba, wale wanaume ambao huwa ni watu wa kukubali kila jambo wanaloambiwa na wake zao, huja kufikia mahali ambapo uwezo katika tendo la ndoa huisha ambapo hushindwa kabisa kushiriki jambo hilo au kulishiriki kwa taabu sana. Tatizo la uwezo wa nguvu za kiume ambalo hufahamika kitaalamu kama erectile dysfunction, huwa linawakumba zaidi wanaume ambao wametawaliwa na wake zao kuliko wale wanaume wenye kauli ya mwisho kwenye nyumba zao. Utafiti wa kitaalamu unaonyesha kwamba zaidi ya nusu ya watu wenye umri kuanzia umri wa miaka 45 huwa wanakabiliwa na tatizo hili.

Takwimu zitokanazo na tafiti mbalimbali kuhusu suala hili zinaonyesha kwamba, kati ya hao nusu ya watu wote wenye umri kuanzia miaka 45, wengi ni wale ambao hawana kauli mbele ya wake zao. Pamoja na kuwa ni tatizo linaloambatana na umri, suala la mwanaume ‘kukaliwa' na mkewe limeonyesha kuwa na athari zake. Sababu zinazotajwa kuwaweka wanaume wanaotawaliwa na wake zao kwenye hatari ya kuishiwa na nguvu za kiume ni zile za kisaikolojia. Kati ya kila wanaume kumi wanaoishiwa na nguvu za kiume kutokana na sababu za kisaikolojia, sita ni kutokana na kutawaliwa na wake zao. Unaweza kushangaa ni kwa kiasi gani kiwango ni cha juu sana.

Mwanaume ambaye hana kauli kwa mkewe mara nyingi anajiamini anaposhiriki tendo na huwa hana wasiwasi, hali ambayo humuongezea uimara katika suala hilo tofauti na yule ambaye ametawaliwa. Anayetawaliwa huwa na hofu na wasiwasi kutokana na kutojiamini. "Bwanae mbona unafanya kama bata, unanichafua tu hapa………." Wanawake wanaowatawala waume zao ni rahisi kutoa kauli kama hizi wakati wanapokuwa kwenye tendo la ndoa na waume zao, kauli ambazo huwaua waume zao kisaikolojia.

Kwa hiyo wale wanawake ambao wanaona fahari kuwatawala waume zao inabidi wajue kwamba, kitendo hicho huwasababisia waume hao matatizo makubwa katika tendo. Mbaya zaidi ni kwamba wanawake hao mwanapoona waume zao ni ‘wachovu' hukimbilia nje haraka na waume hao huzidi kudhalilika.
 
.....vp na wale wanawake ambao wao kufika kilele kwao ni ndoto....hata upige masaa 3...
Wao nao tatizo lao nn "wa..kutambua"...?
 
.....vp na wale wanawake ambao wao kufika kilele kwao ni ndoto....hata upige masaa 3...
Wao nao tatizo lao nn "wa..kutambua"...?

Hili swali ingeuwa vizuri kama wakijbu wanawake wenyewe...........................
 
Kwahiyo ukimtawala mwanamke mvua ya magoli itamshukia?
OTIS
 
wanaolishwa limbwata je??????
Maana kuna mmoja nimempalimbwata kilo 50, asije akawa yuzilesi bure.
 
Ndo mana baba Kanumba alisusia mazishi kuepusha hayo yote.
Yeye alipanga mwanae azikwe Kwao, Mama akaamrisha azikwe Dar.
 
Wanawake wanapata Tatizo hili kutokana na 'kukaliwa' na wanaume


.....vp na wale wanawake ambao wao kufika kilele kwao ni ndoto....hata upige masaa 3...
Wao nao tatizo lao nn "wa..kutambua"...?
 
kuna male menopause msianza usingizia wanawake kwa matatizo yenu! tafuteni chanzo kwa nini siku hizi wanaume wana hiyo shida sana maana wengine hata hawajaoa na hawana nguvu za kiume!,,
 
Wanaoishi na wanaume wababe na wasio treat wake zao kama equal partners hawafiki kileleni.

Nyumba Kubwa
Nemo says thank you for this useful post, especially the bolded part.

Mtambuzi
Personally mimi sielewe why partners cant share responsibilities in their relationship, instead of having either above the other!!!!
 
Ndo mana baba Kanumba alisusia mazishi kuepusha hayo yote.
Yeye alipanga mwanae azikwe Kwao, Mama akaamrisha azikwe Dar.

Kakajambazi
Excuse me, I beg to differ Kususia msiba of your own kid for any reason, let alone such a dumb reason has got not to do with female domination but rather akili finyu of a stupid small minded male!!!!!!
 
.....vp na wale wanawake ambao wao kufika kilele kwao ni ndoto....hata upige masaa 3...
Wao nao tatizo lao nn "wa..kutambua"...?
Kupiga masaa mengi siyo tija ,tija unapiga vipi!

Mwanamke akiwa hana mood ya kungonoka anaweza kukuachia mpaka utoe hewa yy wala anakusikilizia tu.

Mimi kwa masikio yangu nilimsikia mama mmoja akiwasimulia wenzake kwamba anaporudi nyumbani mara nyingi anakuwa amechoka na mumewe akitaka yy anamwachia lakini anakuwa hayupo kihisia jamaa anakula mzigo akimaliza analala, nilichogundua wawili hao hawapo katika mahusiano mazuri==Mwanaume hajitumi kutimiza majukumu ya familia.
 
Nakubaliana nawe, wanawake waliowakalia waume zao wanaGUBU sana, ile shughuli inahitaji utulivu wa kiakili, ukiambiwa neno linalokera stimu zinapotea na kila wakati unapotaka kuanza ukikumbuka hisia zinapaa tena.

Kuna jamaa ndoa yake imevunjika kwa sababu ya Gubu la mkewe lililosababisha jamaa akawa hawezi shughuli kabisa, si akamua kuchepuka ili kupima km kweli uwezo wake umepunga dah ufanisi ukawa 100% basi akawa anaponea huko huko, siku wamegombana na mkewe akamwambia ananisema kila wakati sina uwezo mbona kwa wanawake wengine naweza!, hiyo tafrani ilikuwa kali na mwanamke akaanza mbele.
 
inawezekana, kwa sabau inaonekana familia nyingi ambazo wanaume wako under-control ya mwanamke watot huzaliwa wa kike(jaribu kutafiti utaona) sijajua kwanini lakini nafikiri ni kwa sababu mbegu za kiume huhitaji utulivu na amani na za kike ni weak but fast!!! so ni possible ulichokisema mkuu
 
du wee toghocho hatari,najaribu kuwaza kama ina ukweli vile!
 

fanya research yako vizuri kwa hiyo wanaume waliozaa boys ni wababe? mbona si kweli!
 

fanya research yako vizuri kwa hiyo wanaume waliozaa boys ni wababe? mbona si kweli! kwa hiyo kama firstborn ni girl baba alikaliwa secondborn akiwa boy baba alikuwa mbabe loooh!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…