kmbwembwe
JF-Expert Member
- Aug 16, 2012
- 10,892
- 7,780
Hivi jamani vazi la taifa hua linatafutwa au linakuepo tu?
Mimi naamini watanzania kama taifa hatuna vazi ila tuna mavazi ya jadi kwa makabila mbalimbali ya nchi yetu. Mavazi ambayo wala hatuyavai tena isipokua kwa makabila machache kama wamasai. Wao hadi leo wameweza kudumisha uvaaji wa vazi lao la kiasili.
Kuna waziri mmoja wa utamatuni awamu ya nne alianzisha mradi wa kutafuta au kubuni vazi la taifa. Hela nyingi ikatumika mwisho wake wala vazi lilobuniwa halikukubalika na umma wa wananchi.
Nionavyo mimi mawaziri wa utamaduni waache huu mchongo wa kutafuta vazi la taifa.
Sasa waziri wa utamaduni kaanzisha tena upya eti mradi wa kutafuta au kubuni vazi la taifa. Matokeo yatakua yaleyale ya mwanzo wasanii kupewa riziki isiyokua na tija yoyote zaidi ya kua ni ubadhilifu tu.
Vazi la taifa sio kitu cha kubuniwa na wabunifu wa mavazi. Ni vazi la jadi linalotokana na utamaduni wa watu uliyojengeka kwa karne kadhaa sawa na lugha wanayoongea watu hao.
Tanzania tutambue tu mavazi ya jadi ya makabila yetu na pia ya waswahili wa pwani ya nchi yetu kama urithi wetu kimavazi. Tuachane na mradi wa kuwapa wasanii wa ubunifu ulaji huku tukijua kila watakapotuletea vazi hatutakubaliana nalo kama ndio vazi la taifa.
Mimi naamini watanzania kama taifa hatuna vazi ila tuna mavazi ya jadi kwa makabila mbalimbali ya nchi yetu. Mavazi ambayo wala hatuyavai tena isipokua kwa makabila machache kama wamasai. Wao hadi leo wameweza kudumisha uvaaji wa vazi lao la kiasili.
Kuna waziri mmoja wa utamatuni awamu ya nne alianzisha mradi wa kutafuta au kubuni vazi la taifa. Hela nyingi ikatumika mwisho wake wala vazi lilobuniwa halikukubalika na umma wa wananchi.
Nionavyo mimi mawaziri wa utamaduni waache huu mchongo wa kutafuta vazi la taifa.
Sasa waziri wa utamaduni kaanzisha tena upya eti mradi wa kutafuta au kubuni vazi la taifa. Matokeo yatakua yaleyale ya mwanzo wasanii kupewa riziki isiyokua na tija yoyote zaidi ya kua ni ubadhilifu tu.
Vazi la taifa sio kitu cha kubuniwa na wabunifu wa mavazi. Ni vazi la jadi linalotokana na utamaduni wa watu uliyojengeka kwa karne kadhaa sawa na lugha wanayoongea watu hao.
Tanzania tutambue tu mavazi ya jadi ya makabila yetu na pia ya waswahili wa pwani ya nchi yetu kama urithi wetu kimavazi. Tuachane na mradi wa kuwapa wasanii wa ubunifu ulaji huku tukijua kila watakapotuletea vazi hatutakubaliana nalo kama ndio vazi la taifa.