Wanariadha watatu wa DR Congo wametoweka tangu Jumapili siku ya mwisho ya michezo ya 33 ya Olimpiki

Wanariadha watatu wa DR Congo wametoweka tangu Jumapili siku ya mwisho ya michezo ya 33 ya Olimpiki

Mkalukungone mwamba

JF-Expert Member
Joined
Aug 29, 2022
Posts
862
Reaction score
1,755

Screenshot 2024-08-13 094459.png

Wakati sherehe za kufunga michezo ya Olimpiki zikifanyika mjini Paris, wanariadha watatu wa DR Congo wametoweka tangu Jumapili hii, siku ya mwisho ya michezo ya 33 ya Olimpiki.

Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo ilishiriki katika matukio manne (Judo, kuogelea, riadha na ndondi) nchi hiyo ikikumbwa na ushiriki duni na kumaliza mashindano bila kutwaa Medali.

Soma Pia: Olympic 2024 France: Maonesho ya Ufunguzi yashutumiwa kuonesha viashiria vya ushetani na upinga Kristo

Wakongo waliofanya vizuri ni Dominique Lasconi aliyetolewa katika raundi ya kwanza katika mbio za mita 100 kwa wanaume akimaliza katika nafasi ya 7 baada ya kufanikiwa kumaliza wa tatu katika awamu ya awali kwa muda wa 10’54

Matukio hayo yanaongeza doa kwa DRC huku Didier Budimbu, Waziri wa Michezo akiondoka Kinshasa kwenda Paris kushiriki katika kufungwa kwa michezo hiyo ya Paris. Kwenye tovuti ya Paris, mabondia Marcelat Sakobi, Brigitte Mbabi na muogeleaji Divine Miansadi wamesalia kuwa wanariadha pekee wa DR Congo ambao walishiriki gwaride la kuhitimisha mashindano ya Olimpiki.
 
Dadeki, ukisia one mistake one goal ndio hiyo sasa😃😃
 

Wakati sherehe za kufunga michezo ya Olimpiki zikifanyika mjini Paris, wanariadha watatu wa DR Congo wametoweka tangu Jumapili hii, siku ya mwisho ya michezo ya 33 ya Olimpiki.

Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo ilishiriki katika matukio manne (Judo, kuogelea, riadha na ndondi) nchi hiyo ikikumbwa na ushiriki duni na kumaliza mashindano bila kutwaa Medali.

Soma Pia: Olympic 2024 France: Maonesho ya Ufunguzi yashutumiwa kuonesha viashiria vya ushetani na upinga Kristo

Wakongo waliofanya vizuri ni Dominique Lasconi aliyetolewa katika raundi ya kwanza katika mbio za mita 100 kwa wanaume akimaliza katika nafasi ya 7 baada ya kufanikiwa kumaliza wa tatu katika awamu ya awali kwa muda wa 10’54

Matukio hayo yanaongeza doa kwa DRC huku Didier Budimbu, Waziri wa Michezo akiondoka Kinshasa kwenda Paris kushiriki katika kufungwa kwa michezo hiyo ya Paris. Kwenye tovuti ya Paris, mabondia Marcelat Sakobi, Brigitte Mbabi na muogeleaji Divine Miansadi wamesalia kuwa wanariadha pekee wa DR Congo ambao walishiriki gwaride la kuhitimisha mashindano ya Olimpiki.
Huko wanandugu zao kama wote
 
Wanamichezo waTZ walishazamiaga Australia 🇦🇺 alikuwa bondia na mwenzie

Sio mambo mageni sana
 
Mcongo tena usitumie chance ya Pariiii,,utakua boya jamaa hawajafanya makosa
 
Vijana wameamua wakapambane na changamoto za Paris, walitoroka mahujaji sembuse hao
 
Back
Top Bottom