Dr Akili
JF-Expert Member
- Aug 21, 2011
- 5,119
- 4,569
Nilishindwa kupata jibu la kisayansi la kile kilichowapata baadhi ya vijana waliokuwa kwenye mkusanyiko mkubwa wa watu eneo la wazi huko Tanga (tena karibu na fukwe ya bahari la Hindi), kuishiwa pumuzi na kuzimia kutokana na upungufu wa hewa ya oxygen iliyosababishwa na uwingi na msongamano wa watu katika eneo hilo la wazi!
Vijana hawa walianguka na kulala chini wakigalagala kwa ukosefu wa hewa ya oxygen kama tulivyowaona kwenye luninga. Kitendo cha kuweza kulala chini kilimaanisha kwamba angalao kulikuwa na nafasi (space) kati ya mtu na mtu ya kutosha mtu kulala lakini Oxygen imevutwa yote na kuacha vacuum!
Kwa madaktari na wanasayansi naomba mtujuze kama hili linawezekana kweli. Yaani kwa mfano kule mbuga ya Serengeti hayo makundi makubwa ya nyumbu ambayo huwa yanajikusanya kwa ajili ya 'Great Migration' huwa baadhi yanakufa kwa kumalizika hewa ya oxygen? Kwenye closed space kama kumbi za maholi ni jambo la kawaida hasa kama madirisha yamefungwa au hayatoshi, na dawa yake huwa ni kutoka nje kwenye eneo la wazi ambalo lina unlimited amount of air 30% of which is oxygen!
Wanasayansi/ madaktari tupeni jibu.
Vijana hawa walianguka na kulala chini wakigalagala kwa ukosefu wa hewa ya oxygen kama tulivyowaona kwenye luninga. Kitendo cha kuweza kulala chini kilimaanisha kwamba angalao kulikuwa na nafasi (space) kati ya mtu na mtu ya kutosha mtu kulala lakini Oxygen imevutwa yote na kuacha vacuum!
Kwa madaktari na wanasayansi naomba mtujuze kama hili linawezekana kweli. Yaani kwa mfano kule mbuga ya Serengeti hayo makundi makubwa ya nyumbu ambayo huwa yanajikusanya kwa ajili ya 'Great Migration' huwa baadhi yanakufa kwa kumalizika hewa ya oxygen? Kwenye closed space kama kumbi za maholi ni jambo la kawaida hasa kama madirisha yamefungwa au hayatoshi, na dawa yake huwa ni kutoka nje kwenye eneo la wazi ambalo lina unlimited amount of air 30% of which is oxygen!
Wanasayansi/ madaktari tupeni jibu.