#COVID19 Wanasayansi wanatengeneza Chanjo ya Corona inayoweza kuliwa kwenye Nyanya

#COVID19 Wanasayansi wanatengeneza Chanjo ya Corona inayoweza kuliwa kwenye Nyanya

Sam Gidori

Senior Member
Joined
Sep 7, 2020
Posts
165
Reaction score
417
Wanasayansi nchini Uzbekistan wanatengeneza chanjo dhidi ya virusi vya corona inayoweza kuliwa ndani ya nyanya, Wizara ya Ubunifu ya nchi hiyo imeeleza.

Wanasayansi kutoka Chuo cha Sayansi wamefanikiwa kuweka sehemu ya kirusi hicho ndani ya seli ya nyanya ambapo seli hiyo imegeuka kuwa chanjo dhidi ya virusi hivyo.

Jaribio hilo linatarajiwa kukamilika baada ya kukuza nyanya kwa miezi miwili ambapo watu watakaokula nyanya hizo watatengeneza kinga ya mwili dhidi ya virusi vya corona.

Msemaji wa Chuo hicho ameliambia Shirika la Habari la Uturuki (Anadolu Agency) kuwa majaribio ya chanjo hiyo yalianza mwezi Januari na kuwa chanjo hiyo kwa sasa inajaribiwa kwa wanyama.

Hatua ya kwanza ya majaribio ya chanjo kwa binadamu itaanza mara tu majaribio kwa wanyama yatakapokamilika.

Chanzo: AA

1630317445678.png
 
Uzbekistan inatakiwa kupongezwa sana kwa hatua iliyofikia. Japan nchi ambayo mimi ninaishangaa sana Nchi ya 3 kwa Uchumi mkubwa lakini mpaka leo wanategemea Chanjo kutoka America. Ni aibu kwa taifa la Japan
 
Ule mpango wa kukwepa chapa ya mnyama ndio umefikia hitimisho🤣
Tutakula mboga ambazo hazijaungwa na nyanya mkuu! Afu si tutalima nyanya zetu kwa mbegu zetu sio lazima kuagiza huko..

Ila wakiweka kwenye bia au sigara hachomoki mtu.. Make unakuta hata kama huvuti fegi ila ule moshi wa anaevuta naww ukivuta wa pembeni tayari unakua umepata kinga 😎😎
 
Nasubiria waweke kwenye viazi na mayai ili tuone wanaume wa dar wanavyoteketea
But ni mtizamo tyu, wajumbe msijenge chuki
 
Back
Top Bottom