Mtawaonea tu wanasheria bure,
>>kazi ya uanasheria si lelemama kama wengi wafikiriavyo, inahitaji moyo mgumu na commitment,
>>wengi wamesomeshwa na fedha za wazazi wao (hakuna mtu anayesoma bure Tz)
>>mtu anatumia gharama nyingi sana na muda mwingi mpaka kuja kuwa mwanasheria,
>>kuendesha kesi ni gharama pia na muda unatumika pia kuandaa hiyo kesi
>>mwanasheria ni mtu kama watu wengine mwenye majukumu kama yako
>>mwanasheria analipa kodi kama mfanyabiashara mwingine, ana TIN na Business License
>>analipia leseni ya uendeshaji wa huduma zake (practising license) kila mwaka
>>analipia huduma nyingine za kuendesha ofisi yake na wafanyakazi
>>wakati mwingine anakutana na kesi ambayo inaweza hatarisha amani ya maisha yake
>>kazi ya uanasheria siyo ya lazima kutoa huduma kwa jamii bure
>>Tanganyika Law Society inatoa msaada (Pro bono) kwa watu ambao hawana uwezo wa kifedha kwa kuwapa mawakili
kwahiyo mtu unapokuja hapa na kuanza kutoa lawama kana kwamba hii hudumu ni ya bure fikiria kwanza hayo hapo juu, yaani ni sawa uende dukani kwa mtu akupe huduma bure wakati yeye ameigharamia, pamoja na kwamba wanasheria wanatoa huduma mbalimbali bure (msaada wa sheria) kupitia vituo mbalimbali nchini na vipo vingi sana kila wilaya pamoja na kujitangaza kwenye vyombo mbalimbali vya habari, na kwenye mitandao ya kijamii, ni watu wachache sana wanaothubutu kwenda kuomba msaada wa sheria bure.
sasa najiuliza mlitaka wanasheria wawafate nyumbani kwenu mkiwa na matatizo ya kisheria wawasaidie?, au watembelee sehemu zenye migogoro ya ardhi ndo wawasaidie kutatua?, matatizo ya kikaktiba ni mengi sana yametatuliwa na wanasheria hata juzi tumeona la wakili Jebra Kambole khs ndoa za utotoni, suala la Mtikila lilikuwa ni personal interest wala si public interest, yeye alikuwa na masilahi yake binafsi so huwezisema eti hakuna watu ambao wanantetea katiba ama wananchi, kumekuwa na vipindi vingi sana kwenye vyombo vya habari kwa ajili ya kutoa elimu ya sheria, (tatizo hamfuatilii)
waTanzania mnataka hata katiba mje mfundishwe majumbani kwenu, na bado mmekuwa wabishi sana, hao hao wanasheria wakitaka kuwaelimisha pamoja na kutoa vielelezo ninyi ndo mnageuka kuwa wanasheria, humu jamii forums, pamoja na kejeli mnazotoa kwa wanasheria, lakini bado misaada ya kisheria inatolewa.
kumbukeni msaada wa sheria ni hiari ya mtu, sheria ni kazi kama kazi nyingine, ukitaka msaada nenda kamuone wakili ofisini kwake, lipa ada, uone kama hujapewa huduma.
halafu huduma ya sheria haitangazwi.