Mpira ni mchezo wa kiuungwana. Kitendo alichofanya Frank Domayo ni cha makusudi. Amekuwa akitumika hivi kila mara. Alishafanya kwa mchezaji wenu mwingine John Boko.
Nadhani mnapaswa mseme naye kuwa huo sio mchezo. Hii michezo ya kihuni sisi wapenda mpira wa miguu hatuitaki. Hata kama mimi si Simba, lakini naamini kuna siku mhuni mmoja atafanya hivyo kwa mchezaji wa team yangu.
Nashauri mashabiki wa Simba msiliache jambo hili kiwepesi. Semeni na Frank Domayo nadhani anaweza wasikiliza na wachezaji wengine wenye tabia za kihuni watajifunza pia.