Wanatupotosha tena, wanaokufa na Corona wakiwa na magonjwa mengine hawafi na Corona

Wanatupotosha tena, wanaokufa na Corona wakiwa na magonjwa mengine hawafi na Corona

Masi Lambo

JF-Expert Member
Joined
Apr 8, 2020
Posts
532
Reaction score
360
Wanadai wagonjwa wa magonjwa mengine wakipata korona wanakufa na magonjwa hayo siyo korona, kama kisukari, moyo, saratani n.k. Lakini duniani kuna hata watoto walio fit bila magonjwa mengine, wamekufa na korona, kuna watu wazima wenye Afya zao wamekufa na korona.

Kwa madai yao wanatupotosha kufikiri korona haiuwi kama rais alivyodai mwanzo na kuonyesha hana ujuzi wowote wa hili na anaongea pumba tu, maana watu wengi hata TZ wamekufa na korona.

Pia wanatupotosha kwa kutotangaza idadi ya visa vya korona wakati dunia nzima inaona umuhimu wake katika kupambana nayo, hili jambo linatufanya tufikiri korona haipo au haijasambaa.

Namuunga mkono rais kwa ugunduzi wake wa uitilafu wa mashine za kupima, lakini maelezo yake ni finyu yasiyoeleweka kufanya wengi wafikiri korona sio kweli na haipo. Zaidi angalia video hii,-

 
Saizi ukipeleka mgonjwa hospitali yoyote wanapima korona baada ya hapo unaambiwa subiri majibu ,wakati huo huo mgonjwa anaumwa figo hivyo watamwachaaaaaaaa mpakaaaa yaani ni shida
 
Wanadai wagonjwa wa magonjwa mengine wakipata korona wanakufa na magonjwa hayo siyo korona, kama kisukari, moyo, saratani n.k. Lakini duniani kuna hata watoto walio fit bila magonjwa mengine, wamekufa na korona, kuna watu wazima wenye Afya zao wamekufa na korona. Kwa madai yao wanatupotosha kufikiri korona haiuwi kama rais alivyodai mwanzo na kuonyesha hana ujuzi wowote wa hili na anaongea pumba tu, maana watu wengi hata TZ wamekufa na korona.

Pia wanatupotosha kwa kutotangaza idadi ya visa vya korona wakati dunia nzima inaona umuhimu wake katika kupambana nayo, hili jambo linatufanya tufikiri korona haipo au haijasambaa.

Namuunga mkono rais kwa ugunduzi wake wa uitilafu wa mashine za kupima, lakini maelezo yake ni finyu yasiyoeleweka kufanya wengi wafikiri korona sio kweli na haipo. Zaidi angalia video hii,-

Kama sio Corona kuua hao wenye sukari na magonjwa yaisyoambukizwa mbona hapo nyuma walikuwa hawafi kama kuku wa kideri? kwa sasa corona inaua hata watoto. Hapa muhimu tafuteni tu tiba hayo mengine ni blah blah tu,pia ongezeni vifaa vya kufanya test kwa watu ,kuwe na vituo vingi vya kufanya test,kazania elimu kwa mfano serikali ingepiga marufuku watu kutembea bila kuvaa barakoa.
 
Hujitambui wewe, sasa ujue na wasio ugonjwa nao wanakufa pia.

Muhimu hata ukiwa na magonjwa ni kujikaza haswa na kuondoa hofu
 
Back
Top Bottom