Wanaume: Mnapokosea kudhani mnawaelewa wanawake………!


Umenena sawia!!!
 
Nikweli kabisa GUSTAVO, wanahitaji kusikilizwa,kuthaminiwa na kupendwa....!

Anaposema kazi nyingi siyo kama anataka mwanaume amsaidie baadhi ya kazi za nyumbani.lol!

Kwani upendo husaidia, huheshim,huvumilia hauhesabu mabaya wal haujivuni.
 
Mtambuzi, hongea sana kwa kutuletea makala yenye somo zuri sana.

Kwa mtazamo wangu mimi na uzoefu juu ya nini wanawake wengi wanataka sitofautiani sana na wewe ila nitalelezea kwa namna ya tofauti kidogo.

Kitu ambacho mwanamke anakitaka kutoka kwa mwanaume ni kimoja tu nacho ni upendo. na huu Mungu mwenyewe alibainisha. Upendo huu ukiwa ni wa kweli(dhati), kutoka kwa mumewe basi utakuwa umebeba silaha za huruma na kujali.

utakapo mpenda mwanamke kisha ukamjali ni wazi kuwa, utayafanya hayo kwa hali na mali. Kadhalika utakapo mpenda na ukamuhurumia basi utayafanya hayo kwa kukivaa kiatu chake na hivyo hutapenda umuone amekosa raha au anaumia kwa sababu ya kitu fulan iwe ni kimwili au kihisia tu.

mfano- mnapotoka kazini wote wawili jioni kisha mkarudi nyumbani ndani ya gari moja, kwa mwanamke anayejua wajibu wake ataingia ndani baada ya kuoga, atarudi jikon kuangalia nini kinachoendelea, wakati huyu mama anayafanya hayo pasi hata kulalamika kuwa amechoka basi ilimpasa mumewe kwa sababu anao upendo wa dhati juu ya mkewe ambembeleze kwa pole mke wangu, haya ma swtlo ni kusaidie nini au hata amfuate jikon akambusu kidogo. ukifanya hivi tu bila hata kusema neno jingine utashangaa sura ya huyu mwanamke imebadilika tabasamu limejaa usoni na hata menu anayo andaa ikawa na mvuto.( huu ni mfano tu)

so wanawake wanapenda zaidi kujalia kisaikolojia wa upendo wa dhati basi. material giving kwao siyo ishu kubwa sana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…