Wanaume tukubali tu, no way out! Jinsia si kigezo tena cha kuwa Kichwa cha familia!

Wanaume tukubali tu, no way out! Jinsia si kigezo tena cha kuwa Kichwa cha familia!

Weakman

JF-Expert Member
Joined
Jul 23, 2021
Posts
995
Reaction score
1,607
Duuh yaani hata kabla sijafafanua hoja, mnaanza kunifokea!?

Anyway, ukweli ni kwamba dunia hapo kale ilimtambua mume kuwa Kichwa Cha familia! Kiukweli kwa uhalisia wa nyakati zile Ilikuwa sahihi kwa 100%

Mwanamume alibeba sifa zote tatu za msingi za kuwa mkuu wa familia, ambazo ni umiliki wa uchumi, umiliki wa akili pevu, na nguvu za mwili.

Nyakati zile haikuwezekana katu mwanamke kumiliki uchumi wowote. Hakumiliki mifugo Wala shamba, hakuruhusiwa kufanya kazi za biashara Wala ufundi, na kamwe hakuruhusiwa kwenda kuwinda nguchiro, swala hata kutega mitego ya kanga Wala kware shambani.

Kwa hali hio mwanamke asingeweza kamwe kutunza familia wala kujitunza mwenyewe!

Wanawake hawa walikuwa wakifiwa na waume wao, huishi maisha magumu Sana na Hadi manabii nyakati zile wakaleta maandiko ya kuhimiza kusaidia wajane, maandiko ambayo kwa Sasa ni outdated!

Kuhusu akili pevu, kwa mwanamke nyakati zile haikuwa Jambo rahisi kutokea!
Akili hujengwa na kuimarishwa kulingana na mfumo wa maisha ambao mwanadamu hupitia!
Maisha ya mwanamke nyakati zile hayakufungamana na Harakati za utatuzi wa changamoto za maisha.

Jamii ilimsuka mume kuwa mpambanaji wa changamoto, hivyo akili yake ikawa inapevuka kila siku.
Mwanamume alikaa kutafakari ufugaji, kilimo, biashara, uwindaji, utawala hadi mapambano ya Vita.
Mwanamke aliwekwa pembeni, na akawa mlezi wa watoto.

Yeye ni kuishi utoto na vitoto nyumbani hivyo akili ya mwanamke ikawe haipevuki.
Hapo nyumbani ikitokea hitilafu yoyote ataitwa baba haraka.

Baba ndio afikiri kupata ufumbuzi wa tatizo. Hii Hali iliendeleza kudumaza ubongo wa mwanamke

Kuhusu nguvu za mwili, pia mifumo ya maisha ilimnyima mke kujiimarisha. Wanawake hawakuruhusiwa kazi za nguvu zilizowapa tija waume kujenga miili yao!

Hata hivyo ingawa hoja hii ipo kibaiolojia zaidi, lakini ukosefu wa majukumu ya nguvu yalizidisha ulegevu kwa mke, ingawa kibaiolojia asingeweza kuwa juu ya mwanaume kwa ulinganifu wa mabavu!

Leo hii dunia imeshahama huko, tupo mbele maili nyingi Sana!
Kichwa Cha familia Leo hii si issue ya jinsia Tena, Bali sifa tatu nilizoainisha, ambazo nyakati zile zilikuwa sifa za kiume na hivyo mume kuwa Kichwa Cha familia bila kupingwa!

Kutunza familia kunahitaji nguvu ya uchumi. Leo hii uchumi unamilikiwa na yeyote.
Mke anaweza kuwa Bora kiuchumi Mara kumi ya mwanaume.

Mke aweza kujenga nyumba, kununua na kuendesha kilimo, kufanya biashara, kuendesha ofisi za serikali ama binafsi.
Katika mazingira hayo mume unapata wapi uhalali wa kujitangaza kuwa Kichwa Cha familia? Huna haya?

Maisha Leo hii yanaibua na kupevusha akili za mwanamke pia. Mtoto wa kike Leo hii anashiriki nyanya mbalimbali za maisha zinazomfanya kuimarisha akili yake. Uwezo wa kufikiri Leo hii ni kwa jinsia zote. Mwanaume Hana hati miliki Tena ya Akili.

Mume upo na mke mwenye uwezo wa kufikiri Mambo zaidi yako, unatoa wapi nguvu ya kujitangaza kuwa wewe ni kichwa Cha familia?

Kuhusu nguvu za mwili, si tena factor ya msingi kwa ujenzi na utunzaji wa familia. Nguvu itabaki kuwa sehemu ya kipaji Cha kazi za shamba, au vibarua barabarani au viwandani

Hivi, jamani, madam wetu president, madam speaker na wanawake wengine wa kaliba yao, mume anapata wapi nguvu za kutangaza ukuu wake hapo ndani?

Kwenye nyumba Kama hio wewe mwanamume ni Nani hasa? Provider, planning officer, family guide, family security officer,? who are you to declare the head of family?

Waume lazima tukubali, status zetu za kiuchumi na intelligence ndizo zitaamua kwenye ndoa zetu tuwe kichwa ktk familia, au mwenza ktk familia.

Kuna wanaotoa ushauri humu ndani kuwa mwanaume asioe mke aliyomzidi uchumi au akili. Ni kweli iwapo objective ya kuoa ni kuwa Kichwa Cha familia.

Ukimuoa mke amekuzidi, uwe submissive tu. Hakuna shida, ilimradi bidada yupo tayari kukufanya mwenza wa maisha.

Shida yetu waume ni kukariri kuwa sisi haki yetu ni uboss kwenye nyumba. Ukitaka uboss oa yule ambaye kweli utaonesha uboss wako kiuchumi na kiakili.

Mwisho wa siku, Mimi niseme kwamba,
1)Dunia ya leo Kichwa Cha familia ni yeyote anayestahili

2) "Mwanaume ni provider" ni outdated philosophy!
Yeyote ni provider wa familia, iwe baba pekeyake, iwe mama pekeyake au kwa ushirikiano wao kwa viwango sawa au visivyosawa kutegemeana na hali zao.

3) Mahari zifutwe! Ndoa iwe muungano wa hiari wa kujenga familia.
Mahari bado inabeba dhana kuwa mume Ni kichwa, na kwamba yeye ndiye anakwenda kuiendesha familia, na mke anawajibika kwake kwa utiifu wote kitu ambacho hakipo.

Wanawake si watiifu Tena, na possibility ya mume kuwa Kichwa Cha familia ni ndogo Sana.
Misingi ya ndoa za kale imevunjika vipande vipande.

4)Mwanaume kwa Sasa oa kwa ajili ya familia na sio kwa ajili ya mke. Jenga ngome ya ukuu wako na si kuamini kuwa umezaliwa kuwa mkuu wa familia.

Hakuna mke anamheshimu mume kwa sababu ya uanaume wake. Bali utaheshimiwa kwa uchumi wako na akili zako.
Uchumi na akili ndio nyenzo ya kuwa Kichwa Cha familia!

5) Zipo familia nyingi tu, mke ndio kichwa Cha familia!!
 
Leo hii dunia imeshahama huko, tupo mbele maili nyingi Sana!
Mkuu tuanze na huu mstari. Tukifanya ulinganisho wa mmong'onyoko wa ustawi wa jamii uko zamani na sasa hivi, je tupo mbele au tumerudi nyuma? Hivi kuwa mbele ni nini? Ni matekeo chanya ya mfumo au mabadiliko yoyote tu hata kama ni mabovu ukilinganisha na hali ya mwanzo?

Hii mifumo ya feminism na 50/50 tuliyoipokea bila kuifanyia review iendane na mazingira yetu imetuletea anguko la ustawi wa jamii. Infact hata hao wazungu tuliowageza mifumo hii imewqsababishia matatizo makubwa sana. Sasa tutasemaje tupo mbele?

Kwa mentality yako wewe hata ukioa bila shaka mkeo atakua ndie mume ndani ya nyumba.
 
Kitendo cha mwanaume kujiita 'weak' hapo kuna shida kubwa....
 
Mwanaume kujiita ni weak ni uzoba na inaonekana mke wako amekutawala na wewe umekubali kutawaliwa .wanaume tumebaki wa Kanda Ile ya makamanda kwingine hamna kitu.
 
Daima mwanaume ndio kiongozi wa familia, iwe mwanamke ndio ana ukwasi zaidi, iwe ana maarifa zaidi ya mume, etc.. Mwanaume ni mwanaume tu, busara kubwa kabisa ni masikilizano, mnayajenga pamoja..

Ni kipindi gani hicho wanawake hawakuwa wafanyabiashara!?
 
  • Thanks
Reactions: 2v1
🌈 endeleeni kupambana ila hamtoshinda kamwe,hii vita ngumu kuliko mnavyo fikiri
 
Unataka tuwe weak kama wewe ndani ya nyumba? Mwanamke hakuzaliwa kuwa kichwa hata awe trilionea, hawana akili ya kusimamia na kuongoza. Nyumba nyingi ambazo mwanamke ni kichwa migogoro haiishi. Pole sana kwa kukubali kuwa mwanaume suruali.
 
Wazungu walianza hivi hivi kama mtoa mada kabla ya matokeo ambayo tunayaona kwao,
Wanajutia kwa kukosea lakini hawawezi kutwambia. Huwezi ku dictate nature.

Kivyovyote vile, awe kasoma awe na uchumi jitahidi mke awe chini yako na hata wao ndicho kitu wanapenda.
 
Wanajutia kwa kukosea lakini hawawezi kutwambia.
Na ukishaona mzungu anakuletea ideology yake ujue imeshamsababishia matatizo.

We jiulize kwanini wanatupa biblia bure lakini kamwe hawawezi kutuletea sayansi ya kutengeneza ndege bure.
 
Shida kubwa Tulio nayo Ni Kuwaelekeza Wanaume Wapumbavu(Simps) pia Wanawake Wajinga(Feminists).

Juhudi zetu zinakuwa Ngumu kwa Uwepo wa Wanaume Wapumbavu kama Hawa.

Wakipata mishangazi inawalea au Kifeminist Chenye makalio makubwa Basi simp anaukataa Uanaume na Yeye anakuwa Mwanamke.

Siku ambayo Mwanamke atakuwa More Muscular than man na Atakuwa haingii period hadi anaumwa. Basi ndio uje useme Mambo yamebadilika.
 
Duuh yaani hata kabla sijafafanua hoja, mnaanza kunifokea!?

Anyway, ukweli ni kwamba dunia hapo kale ilimtambua mume kuwa Kichwa Cha familia! Kiukweli kwa uhalisia wa nyakati zile Ilikuwa sahihi kwa 100%

Mwanamume alibeba sifa zote tatu za msingi za kuwa mkuu wa familia, ambazo ni umiliki wa uchumi, umiliki wa akili pevu, na nguvu za mwili.

Nyakati zile haikuwezekana katu mwanamke kumiliki uchumi wowote. Hakumiliki mifugo Wala shamba, hakuruhusiwa kufanya kazi za biashara Wala ufundi, na kamwe hakuruhusiwa kwenda kuwinda nguchiro, swala hata kutega mitego ya kanga Wala kware shambani.

Kwa hali hio mwanamke asingeweza kamwe kutunza familia wala kujitunza mwenyewe!

Wanawake hawa walikuwa wakifiwa na waume wao, huishi maisha magumu Sana na Hadi manabii nyakati zile wakaleta maandiko ya kuhimiza kusaidia wajane, maandiko ambayo kwa Sasa ni outdated!

Kuhusu akili pevu, kwa mwanamke nyakati zile haikuwa Jambo rahisi kutokea!
Akili hujengwa na kuimarishwa kulingana na mfumo wa maisha ambao mwanadamu hupitia!
Maisha ya mwanamke nyakati zile hayakufungamana na Harakati za utatuzi wa changamoto za maisha.

Jamii ilimsuka mume kuwa mpambanaji wa changamoto, hivyo akili yake ikawa inapevuka kila siku.
Mwanamume alikaa kutafakari ufugaji, kilimo, biashara, uwindaji, utawala hadi mapambano ya Vita.
Mwanamke aliwekwa pembeni, na akawa mlezi wa watoto.

Yeye ni kuishi utoto na vitoto nyumbani hivyo akili ya mwanamke ikawe haipevuki.
Hapo nyumbani ikitokea hitilafu yoyote ataitwa baba haraka.

Baba ndio afikiri kupata ufumbuzi wa tatizo. Hii Hali iliendeleza kudumaza ubongo wa mwanamke

Kuhusu nguvu za mwili, pia mifumo ya maisha ilimnyima mke kujiimarisha. Wanawake hawakuruhusiwa kazi za nguvu zilizowapa tija waume kujenga miili yao!

Hata hivyo ingawa hoja hii ipo kibaiolojia zaidi, lakini ukosefu wa majukumu ya nguvu yalizidisha ulegevu kwa mke, ingawa kibaiolojia asingeweza kuwa juu ya mwanaume kwa ulinganifu wa mabavu!

Leo hii dunia imeshahama huko, tupo mbele maili nyingi Sana!
Kichwa Cha familia Leo hii si issue ya jinsia Tena, Bali sifa tatu nilizoainisha, ambazo nyakati zile zilikuwa sifa za kiume na hivyo mume kuwa Kichwa Cha familia bila kupingwa!

Kutunza familia kunahitaji nguvu ya uchumi. Leo hii uchumi unamilikiwa na yeyote.
Mke anaweza kuwa Bora kiuchumi Mara kumi ya mwanaume.

Mke aweza kujenga nyumba, kununua na kuendesha kilimo, kufanya biashara, kuendesha ofisi za serikali ama binafsi.
Katika mazingira hayo mume unapata wapi uhalali wa kujitangaza kuwa Kichwa Cha familia? Huna haya?

Maisha Leo hii yanaibua na kupevusha akili za mwanamke pia. Mtoto wa kike Leo hii anashiriki nyanya mbalimbali za maisha zinazomfanya kuimarisha akili yake. Uwezo wa kufikiri Leo hii ni kwa jinsia zote. Mwanaume Hana hati miliki Tena ya Akili.

Mume upo na mke mwenye uwezo wa kufikiri Mambo zaidi yako, unatoa wapi nguvu ya kujitangaza kuwa wewe ni kichwa Cha familia?

Kuhusu nguvu za mwili, si tena factor ya msingi kwa ujenzi na utunzaji wa familia. Nguvu itabaki kuwa sehemu ya kipaji Cha kazi za shamba, au vibarua barabarani au viwandani

Hivi, jamani, madam wetu president, madam speaker na wanawake wengine wa kaliba yao, mume anapata wapi nguvu za kutangaza ukuu wake hapo ndani?

Kwenye nyumba Kama hio wewe mwanamume ni Nani hasa? Provider, planning officer, family guide, family security officer,? who are you to declare the head of family?

Waume lazima tukubali, status zetu za kiuchumi na intelligence ndizo zitaamua kwenye ndoa zetu tuwe kichwa ktk familia, au mwenza ktk familia.

Kuna wanaotoa ushauri humu ndani kuwa mwanaume asioe mke aliyomzidi uchumi au akili. Ni kweli iwapo objective ya kuoa ni kuwa Kichwa Cha familia.

Ukimuoa mke amekuzidi, uwe submissive tu. Hakuna shida, ilimradi bidada yupo tayari kukufanya mwenza wa maisha.

Shida yetu waume ni kukariri kuwa sisi haki yetu ni uboss kwenye nyumba. Ukitaka uboss oa yule ambaye kweli utaonesha uboss wako kiuchumi na kiakili.

Mwisho wa siku, Mimi niseme kwamba,
1)Dunia ya leo Kichwa Cha familia ni yeyote anayestahili

2) "Mwanaume ni provider" ni outdated philosophy!
Yeyote ni provider wa familia, iwe baba pekeyake, iwe mama pekeyake au kwa ushirikiano wao kwa viwango sawa au visivyosawa kutegemeana na hali zao.

3) Mahari zifutwe! Ndoa iwe muungano wa hiari wa kujenga familia.
Mahari bado inabeba dhana kuwa mume Ni kichwa, na kwamba yeye ndiye anakwenda kuiendesha familia, na mke anawajibika kwake kwa utiifu wote kitu ambacho hakipo.

Wanawake si watiifu Tena, na possibility ya mume kuwa Kichwa Cha familia ni ndogo Sana.
Misingi ya ndoa za kale imevunjika vipande vipande.

4)Mwanaume kwa Sasa oa kwa ajili ya familia na sio kwa ajili ya mke. Jenga ngome ya ukuu wako na si kuamini kuwa umezaliwa kuwa mkuu wa familia.

Hakuna mke anamheshimu mume kwa sababu ya uanaume wake. Bali utaheshimiwa kwa uchumi wako na akili zako.
Uchumi na akili ndio nyenzo ya kuwa Kichwa Cha familia!

5) Zipo familia nyingi tu, mke ndio kichwa Cha familia!!
Hizi ni dhana za kidini ambazo wengine hatujawahi kuzikubali kama dhana za uhalisia nje ya muktadha wa dini.
 
Utakuwa mwanamke mwenye mwonekano wa kiume, samahani lakini kama nimetumia neno gumu
 
Back
Top Bottom