Rorscharch
JF-Expert Member
- Jul 22, 2013
- 878
- 2,014
Wanawake wenu na watoto wenu wanaharibika, si kwa sababu yao pekee, bali kwa sababu nyinyi ni watu wa hovyo! Mmesahau majukumu yenu kama viongozi wa familia na jamii, mmekaa kimya mkiona kila kitu kinaporomoka huku mkijifanya hamuoni! Mmegeuka wanaume wa mzaha—watu wa starehe, watu wa mizinga, watu wa kufuata mkumbo! Mmeacha majukumu yenu na kuwa mashabiki wa maisha badala ya kuwa wahusika wakuu. Leo hii, baba ni jina tu—heshima yake haipo, mamlaka yake haipo, sauti yake haina nguvu!
Na msiwaelekezee lawama wazee wenu—kweli waliteleza kwa namna moja au nyingine, lakini angalau wao walijitahidi kuweka mfumo fulani wa jamii. Nyinyi je? Mko bize na maisha ya hovyo—michepuko, pombe, mziki, mitandaoni kupiga soga! Vikao vya kimila na kitamaduni vilikuwa maeneo ya wanaume kukaa chini na kupanga mustakabali wa familia na jamii zao. Leo hii, Watanzania wanajikusanya kwa makundi makubwa si kwa masuala muhimu, bali kwa ujinga! Kama si mpira, ni siasa za kijinga, au starehe zisizo na mbele wala nyuma!
Viko wapi vikao vya tafakari na maamuzi mazito? Vikao vya wanaume waliotulia, wanaume wenye heshima, wanaume wenye akili timamu, wanaume wanaojiuliza:
"Kwa nini watoto wetu wa kike wanajirahisisha ovyo mitaani?"
"Kwa nini kesi za ustawi wa jamii zinazidi kutufedhehesha?"
"Kwa nini nyumba tunazopangisha zinakuwa makazi ya ushoga na tabia za ajabu?"
"Kwa nini watoto wetu wanakua bila adabu wala heshima kwa wazazi?"
Lakini nyinyi hamuwezi hata kuwa na mazungumzo yenye maana. Mmekuwa wanaume wa kulindana kwenye ujinga! Leo hii mtu ana mshikaji anayejisifia kuzalisha wanawake kila kona bila kuwajibika, na badala ya kumkaripia, mnacheka! Mnacheka? Unacheka na mwanaume anayeharibu maisha ya wanawake na watoto? Unacheka na mwanaume anayekataa majukumu yake? Hili ni tatizo kubwa!
Miaka 20 iliyopita, mwanaume wa heshima alikuwa na mipaka thabiti: mtoto wa kike alikuwa ndani saa 12 jioni, akitoka basi ni kwa sababu maalum au ameolewa! Leo hii, mtoto wako wa kike anakuletea wajukuu ovyoovyo, baba zao huwajui, na maisha yanaendelea kana kwamba hakuna kilichoharibika!
Tumeiangusha jamii kwa kuwa na vipaumbele vya kipuuzi —starehe kwanza, mengine baadaye. Tumekuwa wanaume wa anasa na udhaifu! Hatuna tena msimamo, hatuna tena heshima, hatuna tena mamlaka! Na hata pale tunapokutana kwa ajili ya mambo ya maana, bado tunajifanyia maigizo! Misibani tumejaa unafiki, na kwenye maharusi ni maigizo ya maisha yasiyo halisi—kuoneshana mali badala ya kujenga msingi wa maisha ya baadaye!
Lakini msidhani wanawake nyinyi ni watakatifu—hapana! Nanyi lazima niwaweke on red notice! Mna damu kwenye mikono yenu! Wanaume wanaowazalisha hovyo na kuwatelekeza—it's not all their fault! Mna mategemeo makubwa sana ya jinsi wanaume wanavyotakiwa kuwa, wakati ninyi wenyewe hamjui hata majukumu yenu! Mumewasusia jukumu la furaha zenu na mahitaji yenu! Mnategemea wanaume wawatengenezee maisha, wawajengee mazingira bora, wawafurahishe, wawajibike kwa kila kitu, ilhali ninyi hamchukui hata hatua moja kujenga misingi thabiti ya mahusiano na familia.
Siku hizi mahusiano yamegeuka biashara—mwanaume anahitajika kutoa, kutoa, kutoa, huku mwanamke akiwa mnufaika pekee. Msipopewa, mnalalamika kwamba "wanaume wa siku hizi hawatoshi," ilhali tatizo ni kwamba mmeacha kuwa sehemu ya suluhisho na kubaki kuwa sehemu ya tatizo!
Haya ni maangamizi! Tunakwenda wapi? Ni hivi tunavyotaka vizazi vyetu vikue? Tunataka watoto wetu waje kuwa wanaume wa hovyo kama tulivyo sasa? Tunataka mabinti zetu waendelee kuwa wake wa wanaume wasiowajibika kwa sababu jamii haina mifumo thabiti?
Ni wakati wa kurejea kwenye nafasi yetu ya uongozi! Hakuna kusubiri, hakuna kujificha! Wanaume, tuamke! Wanawake, badilikeni! Tusemane! Tuchukuliane hatua! Acha mchezo, acheni starehe, rudisheni heshima ya familia, jamii, na kizazi chetu!
Na msiwaelekezee lawama wazee wenu—kweli waliteleza kwa namna moja au nyingine, lakini angalau wao walijitahidi kuweka mfumo fulani wa jamii. Nyinyi je? Mko bize na maisha ya hovyo—michepuko, pombe, mziki, mitandaoni kupiga soga! Vikao vya kimila na kitamaduni vilikuwa maeneo ya wanaume kukaa chini na kupanga mustakabali wa familia na jamii zao. Leo hii, Watanzania wanajikusanya kwa makundi makubwa si kwa masuala muhimu, bali kwa ujinga! Kama si mpira, ni siasa za kijinga, au starehe zisizo na mbele wala nyuma!
Viko wapi vikao vya tafakari na maamuzi mazito? Vikao vya wanaume waliotulia, wanaume wenye heshima, wanaume wenye akili timamu, wanaume wanaojiuliza:
"Kwa nini watoto wetu wa kike wanajirahisisha ovyo mitaani?"
"Kwa nini kesi za ustawi wa jamii zinazidi kutufedhehesha?"
"Kwa nini nyumba tunazopangisha zinakuwa makazi ya ushoga na tabia za ajabu?"
"Kwa nini watoto wetu wanakua bila adabu wala heshima kwa wazazi?"
Lakini nyinyi hamuwezi hata kuwa na mazungumzo yenye maana. Mmekuwa wanaume wa kulindana kwenye ujinga! Leo hii mtu ana mshikaji anayejisifia kuzalisha wanawake kila kona bila kuwajibika, na badala ya kumkaripia, mnacheka! Mnacheka? Unacheka na mwanaume anayeharibu maisha ya wanawake na watoto? Unacheka na mwanaume anayekataa majukumu yake? Hili ni tatizo kubwa!
Miaka 20 iliyopita, mwanaume wa heshima alikuwa na mipaka thabiti: mtoto wa kike alikuwa ndani saa 12 jioni, akitoka basi ni kwa sababu maalum au ameolewa! Leo hii, mtoto wako wa kike anakuletea wajukuu ovyoovyo, baba zao huwajui, na maisha yanaendelea kana kwamba hakuna kilichoharibika!
Tumeiangusha jamii kwa kuwa na vipaumbele vya kipuuzi —starehe kwanza, mengine baadaye. Tumekuwa wanaume wa anasa na udhaifu! Hatuna tena msimamo, hatuna tena heshima, hatuna tena mamlaka! Na hata pale tunapokutana kwa ajili ya mambo ya maana, bado tunajifanyia maigizo! Misibani tumejaa unafiki, na kwenye maharusi ni maigizo ya maisha yasiyo halisi—kuoneshana mali badala ya kujenga msingi wa maisha ya baadaye!
Lakini msidhani wanawake nyinyi ni watakatifu—hapana! Nanyi lazima niwaweke on red notice! Mna damu kwenye mikono yenu! Wanaume wanaowazalisha hovyo na kuwatelekeza—it's not all their fault! Mna mategemeo makubwa sana ya jinsi wanaume wanavyotakiwa kuwa, wakati ninyi wenyewe hamjui hata majukumu yenu! Mumewasusia jukumu la furaha zenu na mahitaji yenu! Mnategemea wanaume wawatengenezee maisha, wawajengee mazingira bora, wawafurahishe, wawajibike kwa kila kitu, ilhali ninyi hamchukui hata hatua moja kujenga misingi thabiti ya mahusiano na familia.
Siku hizi mahusiano yamegeuka biashara—mwanaume anahitajika kutoa, kutoa, kutoa, huku mwanamke akiwa mnufaika pekee. Msipopewa, mnalalamika kwamba "wanaume wa siku hizi hawatoshi," ilhali tatizo ni kwamba mmeacha kuwa sehemu ya suluhisho na kubaki kuwa sehemu ya tatizo!
Haya ni maangamizi! Tunakwenda wapi? Ni hivi tunavyotaka vizazi vyetu vikue? Tunataka watoto wetu waje kuwa wanaume wa hovyo kama tulivyo sasa? Tunataka mabinti zetu waendelee kuwa wake wa wanaume wasiowajibika kwa sababu jamii haina mifumo thabiti?
Ni wakati wa kurejea kwenye nafasi yetu ya uongozi! Hakuna kusubiri, hakuna kujificha! Wanaume, tuamke! Wanawake, badilikeni! Tusemane! Tuchukuliane hatua! Acha mchezo, acheni starehe, rudisheni heshima ya familia, jamii, na kizazi chetu!