Wanaume tumeharibika. Wanawake na watoto wanaporomoka kwa sababu hatuwajibiki. Tuamke na tufanye mabadiliko sasa!

Wanaume tumeharibika. Wanawake na watoto wanaporomoka kwa sababu hatuwajibiki. Tuamke na tufanye mabadiliko sasa!

Rorscharch

JF-Expert Member
Joined
Jul 22, 2013
Posts
878
Reaction score
2,014
Wanawake wenu na watoto wenu wanaharibika, si kwa sababu yao pekee, bali kwa sababu nyinyi ni watu wa hovyo! Mmesahau majukumu yenu kama viongozi wa familia na jamii, mmekaa kimya mkiona kila kitu kinaporomoka huku mkijifanya hamuoni! Mmegeuka wanaume wa mzaha—watu wa starehe, watu wa mizinga, watu wa kufuata mkumbo! Mmeacha majukumu yenu na kuwa mashabiki wa maisha badala ya kuwa wahusika wakuu. Leo hii, baba ni jina tu—heshima yake haipo, mamlaka yake haipo, sauti yake haina nguvu!

Na msiwaelekezee lawama wazee wenu—kweli waliteleza kwa namna moja au nyingine, lakini angalau wao walijitahidi kuweka mfumo fulani wa jamii. Nyinyi je? Mko bize na maisha ya hovyo—michepuko, pombe, mziki, mitandaoni kupiga soga! Vikao vya kimila na kitamaduni vilikuwa maeneo ya wanaume kukaa chini na kupanga mustakabali wa familia na jamii zao. Leo hii, Watanzania wanajikusanya kwa makundi makubwa si kwa masuala muhimu, bali kwa ujinga! Kama si mpira, ni siasa za kijinga, au starehe zisizo na mbele wala nyuma!

Viko wapi vikao vya tafakari na maamuzi mazito? Vikao vya wanaume waliotulia, wanaume wenye heshima, wanaume wenye akili timamu, wanaume wanaojiuliza:

"Kwa nini watoto wetu wa kike wanajirahisisha ovyo mitaani?"

"Kwa nini kesi za ustawi wa jamii zinazidi kutufedhehesha?"

"Kwa nini nyumba tunazopangisha zinakuwa makazi ya ushoga na tabia za ajabu?"

"Kwa nini watoto wetu wanakua bila adabu wala heshima kwa wazazi?"



Lakini nyinyi hamuwezi hata kuwa na mazungumzo yenye maana. Mmekuwa wanaume wa kulindana kwenye ujinga! Leo hii mtu ana mshikaji anayejisifia kuzalisha wanawake kila kona bila kuwajibika, na badala ya kumkaripia, mnacheka! Mnacheka? Unacheka na mwanaume anayeharibu maisha ya wanawake na watoto? Unacheka na mwanaume anayekataa majukumu yake? Hili ni tatizo kubwa!

Miaka 20 iliyopita, mwanaume wa heshima alikuwa na mipaka thabiti: mtoto wa kike alikuwa ndani saa 12 jioni, akitoka basi ni kwa sababu maalum au ameolewa! Leo hii, mtoto wako wa kike anakuletea wajukuu ovyoovyo, baba zao huwajui, na maisha yanaendelea kana kwamba hakuna kilichoharibika!

Tumeiangusha jamii kwa kuwa na vipaumbele vya kipuuzi —starehe kwanza, mengine baadaye. Tumekuwa wanaume wa anasa na udhaifu! Hatuna tena msimamo, hatuna tena heshima, hatuna tena mamlaka! Na hata pale tunapokutana kwa ajili ya mambo ya maana, bado tunajifanyia maigizo! Misibani tumejaa unafiki, na kwenye maharusi ni maigizo ya maisha yasiyo halisi—kuoneshana mali badala ya kujenga msingi wa maisha ya baadaye!

Lakini msidhani wanawake nyinyi ni watakatifu—hapana! Nanyi lazima niwaweke on red notice! Mna damu kwenye mikono yenu! Wanaume wanaowazalisha hovyo na kuwatelekeza—it's not all their fault! Mna mategemeo makubwa sana ya jinsi wanaume wanavyotakiwa kuwa, wakati ninyi wenyewe hamjui hata majukumu yenu! Mumewasusia jukumu la furaha zenu na mahitaji yenu! Mnategemea wanaume wawatengenezee maisha, wawajengee mazingira bora, wawafurahishe, wawajibike kwa kila kitu, ilhali ninyi hamchukui hata hatua moja kujenga misingi thabiti ya mahusiano na familia.

Siku hizi mahusiano yamegeuka biashara—mwanaume anahitajika kutoa, kutoa, kutoa, huku mwanamke akiwa mnufaika pekee. Msipopewa, mnalalamika kwamba "wanaume wa siku hizi hawatoshi," ilhali tatizo ni kwamba mmeacha kuwa sehemu ya suluhisho na kubaki kuwa sehemu ya tatizo!

Haya ni maangamizi! Tunakwenda wapi? Ni hivi tunavyotaka vizazi vyetu vikue? Tunataka watoto wetu waje kuwa wanaume wa hovyo kama tulivyo sasa? Tunataka mabinti zetu waendelee kuwa wake wa wanaume wasiowajibika kwa sababu jamii haina mifumo thabiti?

Ni wakati wa kurejea kwenye nafasi yetu ya uongozi! Hakuna kusubiri, hakuna kujificha! Wanaume, tuamke! Wanawake, badilikeni! Tusemane! Tuchukuliane hatua! Acha mchezo, acheni starehe, rudisheni heshima ya familia, jamii, na kizazi chetu!
 
📌📌📌📌
giphy.gif
 
Mnawaonea sana wanaume..mnawatwisha mizigo mizito sana na sheria zinawakandamiza.
Mnawanyima fursa na bado mnataka watimize majukumu yao kama kawaida.
Kwakifupi jamii inamtumia na kumsurubisha sana mwanaume huku kampenu za usawa na jinsia zikiwabeba mnoo jinsia pinzani.

Acheni waishi wanavyoona wao inafaa, msitupangie, otherwise rekebishen mlipokosea mbona iko wazi???
 
mwanaume utafute hela, kazi, nyumba, lakini bado una kuja kudharaurika na kusalitiwa.

Au utafute hela kwa mbinde, kisa hawa mabinti wa TikTok, Instagram au fb nah

KATAA NDOA LINDA MAISHA YAKO
KATAA NDOA LINDA UCHUMI WAKO
KATAA NDOA LINDA UHURU WAKO
 
Daaah mazito mengine haya ,
Mwanamke huyu huyu wa kizazi hiki useme nae neno akusikilize au
Si kwamba majukumu yetu hatuyajui lahasha tunayajua kweli kweli na tunaweza kutimiza haswa ila kuna haya machache

1. Mwanamke wasasa hana heshima
Maandiko yanafundisha vizuri sana mwanamke anapaswa amuheshimu mumewe ukiwa na maan kuwa. Maagizo nitakayotoa yatimizwe mara kadhaa tunashuhudia visa vya kuuliwa kwa wanawake ukifatilia kisa ni dharau .

2. Mwanamke sasa amejikita katika
Kutafuta maisha na sio ulezi kama awali , mfanyakazi anamalezi gani ya uchungu kwa mtoto wa mtu kwa mfano embu nipate jawabu....?
Mama yupo siku moja nyumbn jmpl tu na hio anakua na mambo yake bado unataka mwanaume alaumiwe ktk malezi ,kila kazi wao wanahitaji kufanya kujiringanisha na wanaume vyombo vya habari virekodi sifa zijae kedede kedede kumbe mototo anaumia. Matukio mangapi unyanyaji wa watoto kwa dada na kaka wakazi .

3.Tamaa iliopitiliza
Hiii kwa Hawa ambao wao hawakuumbiwa kutafuta kwa jashoo
Baba anatafuta analeta nyumbn yeye huyo vikobani lengo aonekane nae anacheza mwishowe anapoteza hata mwelekeo na familia anakimbia kwa zama hizo ilikua jambo la kawaida sana mama kubaki na mtoto baba kakimbia lakini sasa mama kakimbia kaacha watoto kisa vikoba mbaya hii sana mtoto anabaki na malezi pande moja lakn Leo unatusema hujui tumekimbiwa na wake zetu .

4.uwepo wa maisha bandia nje na wazazi
Unatambua kabisa dunia imeendelea mno tofauti na ilee ya miaka ile hata vikao hivyo vya malezi sio kukaa katk miti tenha ila Whatsapp video , telegram conference au google meeting sasa kutokana na hii Hali unatoa maelekezo haya kwa mama na mtoto lakn kuna malezi huru huko duniani ktk mitandao ambako ww hujui kama mtu kajifunza mpya unaona mtoto anabadilika tu mwisho ukija kujua umechelewa fuatilia baadhi ya visa mtoto amejifunza tabia flan akiulizwa katoa mtandaoni

5.Malezi mabovu ya kiroho
Mtoto anaweza kuwa Bora tu akikulia misingi ya Iman kwa ulimwengu huu ila kilichopo sasa wachungaji wanatoa maombi tu na miujiza nakutaka sadaka hawakuzi Hawa watoto wadogo katika hofu ya Mungu ifike wakati katk makanisa watoto wawe na madarasa ya kusoma na kujifunza tabia zinazo faaa



Mapendekezo
1.Malezi ya mtoto sio ya mtu mmoja sio mama baba pekee ijumuishwe jamii yaan tuseme malezi yawe ya jamii akikosea wa mwenzako aadhibiwe Kwan akioza wajirani basi na wako kaoza Kwan ataambatana nae tu .

2.Mambo yanayo husisha starehe ikiwezekana yafanywe usiku tu na mavazi Yao yasivaliwe hadharani
...binadamu anajifunza kwa kuona hata Hawa tunao walaumu sisi watu wazima chanzo tunafanya yasio faa mbele zao tunabaki na kauli moja watoto wasiku hizi wanaju kila kitu.

3.Matumizi ya program / aplikesheni baguzi
Yaan natambua sasa haziepukiki sasa kuokoa hili jaazi kuwepo program za ubaguzi kwa kuzingatia umri ,simu ikinunuliwa unapowasha iulize maswali haya
°umri wa mtumiaji -- akiwa na miaka chini ya mtu mzima aplikesheni simu itachagua piah
Na kuchagua program ambazo zinafaa kwa umri wake na sio kua na uhuru ikiwa na maan kwa alie chini miaka 18 playstore hatakuwa anaweza kuingia Wala hakuna website ambayo inamaudhui yakiutu uzima atapaswa kuingia .

4.Nguvu ya dini
Sasa turudi katika malezi ya kiroho makanisani waache tamaa ya pesa tu waajenge na jamii ilonahofu na Mungu .
 
Back
Top Bottom