Wanaume wa siku hizi

mankachara

JF-Expert Member
Joined
Sep 27, 2013
Posts
6,152
Reaction score
3,473
Mwanaume mmoja aliwatongoza wanawake watatu tofauti na nia yake ni kufanya upembuzi yakinifu ili mmoja wao awe mkewe. Hivyo jamaa aliamua kuwapa jaribio kwa kuwapa Tsh. 500,000/= kila mmoja huku akitaka kujua ni namna gani watazitumia.

Mwanamke wa kwanza alitumia pesa yote kununua vipodozi. Alitembelea duka la vipodozi na urembo akajikwatua sawa sawa! Alivyorudi kwa mchumba wake akamwambia,

"nimeamua kutumia pesa yote kwa ajili ya kujipamba ili nizidi kukupendeza

machoni pako na kukuvutia maana nakupenda sana."

Hakika yule mwanaume akapendezwa sana na mpenzi wake.

Mwanamke wa pili alinunua zawadi kwa ajili ya bwana wake. Alinunua simu janja mpya kwa ajili ya bwana wake, saa ya kisasa, nguo na viatu vizuri. Alivyofika kwa bwana wake alimwambia,

"pesa yote nimeitumia kununua hizi zawadi zako maana nina kupenda sana."

Jamaa akafarijika sana

Mwanamke wa tatu aliwekeza zile pesa kwenye soko la hisa na baada ya muda fulani alipata faida ya shilingi 2,000,000/=. Mwanamke yule aliamua kumrudishia bwana wake ile pesa aliyokuwa amepewa yaani laki 5 na pesa iliyokuwa imebakia alifungua akaunti ya pamoja na bwana wake. Kisha yule mwanamke akamwambia yule jamaa,

"nahitaji kuwekeza na kuhifadhi kesho yetu kwa sababu nakupenda sana."

Hakika yule mwanamke alimfurahisha sana jamaa.

Jamaa akatafakari sana yale ambayo yalikuwa yamefanywa na wale wanawake baada ya kupewa laki 5. Lakini mwisho wa siku jamaa aliamua kumwoa mwanamke mwenye makalio makubwa! Wanaume watabakia kuwa wanaume tu!
 
Du......kumbe alikuwa na kigezo chake tayari
 
maisha hayana formula mkuu, ulivyo sivyo utakavyokuwa kesho, ingawa hilo halikuzuii kuandaa kesho yako kila upatapo nafasi
 
Huyo mwenye makalio makubwa ni miongoni mwa hao watatu au?
 
Hahahaaha dah
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…