Wanaume wanaongoza kwa kutovaa pete ya ndoa

TIQO

JF-Expert Member
Joined
Jan 8, 2011
Posts
13,786
Reaction score
2,095
Ukiangalia kwa makini kwenye vidole vya wanandoa utagundua kuwa wanaume wengi hawapendelei kuvaa pete za ndoa, huku wanawake wengi wanapendelea kuvaa pete hizo unakuta anazo mbili ya uchumba na ile ya siku yenyewe ya ndoa kwenye kidole.
Je kwa nini wanaume hawapendi kuvaa pete za ndoa?
 


Pete zinamaana kubwa sana katika mahusiano ya wawili wapendanao unapo amua kuiweka pembeni inaashilia nini?
 


Pete zinamaana kubwa sana katika mahusiano ya wawili wapendanao unapo amua kuiweka pembeni inaashilia nini?
naomba unisaidia kuani umhimu wa kuvaa pete...
 
Ni kweli wanaume wengi hawapendi kuvaa pete hususan za ndoa,
Nadhani shauri ya ukware ndo maana huwa hatupendi kuzivaa pete za ndoa na hasahasa vijana, ila kwa watu wazima huzivaa muda wote.
 
mie automatically toka utoto wangu huwa sipendi kuvaa vitu mwilini kama bangili,heleni,pete au kubadilisha nywele kama mtoto wa kiume huwa naona sipo huru nikifanya mambo hayo kikubwa ninahisi wengi wanavua kutokana na either sio waaminifu kwa ndoa zao au hawapendi tu kwasababu wanaona mzigo mwilini


Pete zinamaana kubwa sana katika mahusiano ya wawili wapendanao unapo amua kuiweka pembeni inaashilia nini?
 
Kuvaa pete ni ujinga! Babu yangu na Bibi yangu mpaka wanatangulia mbele ya haki ndoa yao ilikuwa na miaka 70 (sabini), lakini sikuwahi kuwaona wakiwa na pete kwenye vidole vyao!
 

Ndoa ya wawili wapendanao,
ipo moyoni mwao na Mungu Mwenyezi,
pete ni ishara tu mkuu!!!!
 
Ndoa ya wawili wapendanao,
ipo moyoni mwao na Mungu Mwenyezi,
pete ni ishara tu mkuu!!!!

Kwa hiyo hakuna umuhimu wa kuvaa pete?
 
Baibo haizungumzii pete.

Afu hayo mashindano yalifanyikia wapi?
 
Kuna jamaa yangu havai pete, alianza kutovaa baada ya miaka mi2 ya ndoa. kutokana na biashara zake anadai alikua hapati mashilikiano mazuri kwenye maofisi na watu mbalimbali(akina dada) kunasafari alikwenda nje ya nchi aliisahau pete bahati mbaya. mambo yalikuwa tofauti, ndio mwanzo wa yeye kuto kuvaa pete mara nyingi
 
Wengine walitengenezewa mazingira ya kufunga ndoa, hawakupenda kuoa
 
ngoja nikisaidie dada..........pete halisi iko ndani ya moyo wa mtu...hizi za vidoleni wala zisikupe shida........kuna kima dada/mama wameolewa na wanavaa hizo pete lakini wanatoka sana nje ya ndoa....... hali kadhalika kina baba/vijana.kuna wengine hawavai na hawafanyi upuuzi.
 
Ndoa ya wawili wapendanao,
ipo moyoni mwao na Mungu Mwenyezi,
pete ni ishara tu mkuu!!!!

Bacha umesema kweli kabisa,
Kama wewe sio mwaminifu toka moyoni mwako, huwezi kuwa mwaminifu kwa kuvaa pete.
Afterall mbona mtu anakutokea na lipete likubwaaaaa la ndoa,
Wala haogopi pete, vaeni msivae lakini UAMINIFU UTOKE MOYONI(Vaa hiyo pete ya uaminifu moyoni mwako)
 
Kuvaa pete ni ujinga! Babu yangu na Bibi yangu mpaka wanatangulia mbele ya haki ndoa yao ilikuwa na miaka 70 (sabini), lakini sikuwahi kuwaona wakiwa na pete kwenye vidole vyao!


Kula tano Obuntu, ni ujinga na kuiga kusiko na akili. Wala hakuna sehemu yeyote kwenye Bible inayotaka wanandoa wavae pete.
 

umejitahidi sasa hivi umesoma na kuelewa na umechangia vizuri
 
Kwa hiyo hakuna umuhimu wa kuvaa pete?


sisemi watu waache kuvaa pete,
watu waendelee tu kwa amani kuzivaa hizo pete,
kwani ni ishara kuwa yupo kwenye ndoa, (ingawa siku hizi kuna wengine wanavaa pasipo ndoa)
lakini hata wale wasiovaa na wako kwenye ndoa,
mimi binafsi siwezi kuwashangaa, kwani
ndoa ipo moyoni mwa mtu na wala si kwenye pete!!!!!!
 

Bacha wewe umevaa pete ya ndoa?? Kama hujavaa ulipokea ya nini pale kanisani/Kwa RC.

Si ungeiacha hapo kwa padri/mchungaji
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…