Matatizo ya kuamini mtu haraka....jamani miezi mitatu ya mapenzi unamkubalia ombi kubwa kiasi hicho? Na umefunguka mapema sana yaelekea binti alitoa siri \zake zote kuwa ana uwezo wa kupata huo mtaji au mkaka alikuwa anamlia timing..................................duh kweli kuna haja ya kumshirikisha MUNGU katika kuchagua wenzi wetu!!
OMG................6 milllion,mwanaume wa miezi mitatu???? tena unamchukulia mkopo kazini?? ni mume au baba wa watoto wake???
Kweli maisha ni shule ngumu sana....naomba umpe pole,kupitia yeye na sisi tunazidi kujifunza kuhusu viumbe wazito hawa....hakuna haja ya kulipiza ubaya,manake huyu mwanaume ni jambazi,ana roho isiyoshindwa ubaya wowote.....atulie,avumilie,milioni sita inalipika...akumbatie tu kazi yake sasa.....zaidi,Mwenyenzi Mungu namuomba ampe nguvu,hekima na akili katika kukabiliana na haya yaliyomkuta.....!!!God Forbid!!
mkome na nyie..ndo maana hata JK anawaambia mna viherehere...
wangechukua hamsini ingekuwa vizuri,millioni sita?? Wanaume wengine jamani!!! kweli wanatisha....nafurahi haya maneno yanapotoka kwa mwanaume....Bwana Yesu Rudi tu!!!
Inasikitisha sana, mpe pole shoga yako lkn na sisi wadada tuwe tunajifunza asilimia kubwa ya wanaume ni matapeli na tena wanapenda sana kutumiaa mapenz kuwatapeli wadada so tuwe makini tusipende kuwaamini sana hao sio ndugu zetu, kuna mfanya kazi mwenzagu aliwahi kutapeliwa na mtu aliyekuwa akijiita mpenzi wake kumbe alikuwa anamzuga dada wawatu waliweza kuwa wote kwa mda wa miezi kama minne yule kaka aliigiza anampenda kweli hadi yule dada kafikia hatua ya kumpa yule kaka kadi yake ya benki yule mkaka, yule kaka alichofanya alisubiri yule dada kaenda kazini kaenda benki kakomba milioni tisa na kutoroka siku hiyohiyo na namba ya simu aliyokuwa anaitumia haikupatikana tena yule dada alichoambulia ni kuugua ugojwa ambao haujulikana alikuwa kama kichaa fulani hadi sasa akili yake haijarudi ktk hali yake ya kawaida
Hayo mapenzi motomoto ndo yapi,mpaka utoe milioni sita....Mungu pitisha mbali,hata kama ni matamu namna gani sitaki kitu cha kuniondolea uwezo wa kufikiri....khaaaaaaaaaaaaaa!
Safina my dear,nampa pole sana huyo rafikiyo thoug naona makosa yako upande wake.Three months kweli anatoa all that amount?Hata kama ni ndogo kwake haoni watoto yatima kwenye orphanage centres na mabarabarani?Au yeye mwenyewe haoni viwanja vinavyouzwa?Kama anavyo si angeanza ujenzi basi.Hayo alitakiwa akayafanye kwa mume na si wanaume wa sasa tena in a very short time like that!
Siku hizi kuna wanaume machangudoa na huyo ni mfano wao,alimfuata akiwa na full data hivyo alijipanga kikazi zaidi.Alikuwa very efficient and strategic kuhakikisha anafikia malengo yake while rafikiyo akiamini jamaa kapagawa naye.
Ila pia nimewahi sikia kuwa wapo wanaume same as above ila wao maeenda extra miles.Wanatumia madawa kama yale wanayotumiaga matapeli wanaoiba kupitia kwa mahausigeli,wengine wanakuaga na gold bandia n.k.Ni kwamba usiombe akakutarget,utaamini kila akwambiacho na utampa kila atakacho in a very short period of time.Mara nyingi wanatesha mingo kwenye vituo vya daladala.
Jamani kina dada/mabinti/wanawake tuwe makini,kuna vyangudoa wanaume nao wanatafuta pesa kwa njia hiyo kwa uvivu wa kufikiri.Yaani bongo zao zipo kwenye fuvu kujaza nafasi tu!
Mpelekee pole zake ila isijekuwa ni wewe unatumia kigezo cha "rafiki yangu" si ndio style ya kuripoti matukio hapa JF? Pole sana
Habari za mchana wana jamvi.
Hebu sikilizeni kisa hiki, huwa nina ki-grocery changu, sasa hapa huwa nina mashoga zangu kibao, kila mtu anakuja na la kwakwe kuhusu kutendwa, mengine naona ya kawaida lakini hili jamani!!!!! Limenichosha nimeona niwashirikishe.
Huyu shoga yangu kaja hapa mchana huu analia. Kuna jamaa alijifanya anampenda kwa dhati ya moyo wake, katika kukaa, kaa kwenye hilo penzi lao kwa takribani miezi mitatu kwa jamaa kuonyesha mapenzi mazito haswa mpaka wenzake wakawa wanaona mamsapu kapata bwana wa ukweli. Kumbe jamaa alikuwa na yake kichwani, kamdanganya dada wa watu, eti kuna biashara huwa anafanya lakini amekwama, hivyo anamwomba mdada amkopeshe shilingi 6m. Mdada hakuwa nazo, jamaa akamwambia kwa sababu umeajiriwa naomba unikopee ofisini kwako nitakuwa nikirudisha kidogo, kidogo, mdada wa watu kakopa kampa jamaa. Jamaa baada ya kushika kitita mkononi, kidogo kidogo mapenzi yakaanza kupungua na mwisho yakaisha kabisa, kwani hivi sasa dada akimpigia simu hapokei, akipokea akiulizwa mbona siku hizi hauonekani anasema yuko bize. Mdada si akaamua kujitoa fahamu kumfuata huko nyumbani kwake, akakuta jamaa full shangwe na mwanamke mwingine na deni yeye anaendelea kukatwa kwenye mshahara wake kila mwisho wa mwezi. Mwanaume hajajali kuwa kafumaniwa wala nini? Sana sana alimuuliza unashida gani, binti akamwambia inakuwaje leo hii unaniuliza nimefuata nini wakati mimi ni mpenzi wako jamaa akamwambia una kichaa na maneno mengine mengi ambayo siwezi hata kuendelea kuyaandika. Wanaume jamani, jamani mbona mnatutenda vibaya, vibaya hivi why? Kwanini?
Yaani alimwonyesha mdada mapenzi hasa kumbe hayakuwa mapenzi bali utapeli, alimpa mdada milioni moja ya kufanya shopping. Baada ya muda ndo yeye akaja na gia ya kusema mzigo umekwama na hahui afanye nini? Eti dada tu ndo mtu wake anamhesabu kama mama wa watoto wake, halafu anavyoongeaga kwa upole kaka yule, hata sisi marafiki hatukutegemea. Kweli tumepata somo.
Tapeli wa level nyingine hiyo....mpe pole sana mdada!!
Mkuu sio viherehere, kushikwa na penzi ndo kunasababisha haya. Iko siku deni litaisha, na huyo mhuni hatafika popote na udhulumaji wake.
Aksante kwa ushauri huu. Nipo nae na tunajaribu kumpa moyo sana, mashosti tunataka tumchangie hata kidogo kumrudisha katika hali ya kawaida, maana ukimwona amechanganyikiwa kabisa, lile penzi alilokuwa anapewa halipo, pesa pia hazipo, vyote viwili ni kwa wakati mmoja na jamaa huyo huyo, inauma kwa kweli.
Inasikitisha sana, mpe pole shoga yako lkn na sisi wadada tuwe tunajifunza asilimia kubwa ya wanaume ni matapeli na tena wanapenda sana kutumiaa mapenz kuwatapeli wadada so tuwe makini tusipende kuwaamini sana hao sio ndugu zetu, kuna mfanya kazi mwenzagu aliwahi kutapeliwa na mtu aliyekuwa akijiita mpenzi wake kumbe alikuwa anamzuga dada wawatu waliweza kuwa wote kwa mda wa miezi kama minne yule kaka aliigiza anampenda kweli hadi yule dada kafikia hatua ya kumpa yule kaka kadi yake ya benki yule mkaka, yule kaka alichofanya alisubiri yule dada kaenda kazini kaenda benki kakomba milioni tisa na kutoroka siku hiyohiyo na namba ya simu aliyokuwa anaitumia haikupatikana tena yule dada alichoambulia ni kuugua ugojwa ambao haujulikana alikuwa kama kichaa fulani hadi sasa akili yake haijarudi ktk hali yake ya kawaida