Wanavyuo waambiwa watoe taarifa za viashiria vya vitendo vya ukatili wa Kijinsia na unyanyasaji

Wanavyuo waambiwa watoe taarifa za viashiria vya vitendo vya ukatili wa Kijinsia na unyanyasaji

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
WhatsApp Image 2024-09-25 at 19.04.56_de7dcfe8.jpg

WhatsApp Image 2024-09-25 at 19.04.57_aec86030.jpg
Wanafunzi wa Shule za Sekondari, Vyuo vya Kati na Vyuo Vikuu Mkoani Mbeya wamehimizwa kutoa taarifa za viashiria vya vitendo vya ukatili wa kijinsia na unyanyasaji.

Akizungumza katika uzinduzi wa kampeni ya "Tuwaambie kabla hawajaharibiwa" iliyofanyika Septemba 25, 2024 katika uwanja wa Ruanda Nzovwe Jijini Mbeya, Mkuu wa Wilaya ya Mbeya Mhe Beno Malisa kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa huo Mhe Juma Homera amewataka wanafunzi kutosita kutoa taarifa za ukatili ili ziweze kufanyiwa kazi.
WhatsApp Image 2024-09-25 at 19.04.58_73b8f37b.jpg

WhatsApp Image 2024-09-25 at 19.04.57_b6d4b3f3.jpg
Aidha, Malisa ameeleza kuwa lengo la kampeni hiyo ya Jeshi la Polisi nchini kupitia kitengo cha Dawati la Jinsia na Watoto ni kuwatahadharisha Wanafunzi wa Sekondari, Vyuo vya kati na vyuo vikuu kuhusu hatari iliyopo mbele yao kutokana na utandawazi na mmomonyoko wa maadili.

Aliongeza kuwa, kampeni hii inakwenda kuwakumbusha wazazi na walezi wajibu wao kwa watoto wao wa kutoa malezi bora ikiwa ni pamoja na kufuatilia mienendo na tabia za watoto wao ili kubaini mabadiliko mbalimbali wanayopitia na endapo kama kuna vitendo vibaya wanavyofanyiwa waweze kubaini na kuchukua hatua.

"Kampeni hii imelenga kutoa elimu ya kupinga ukatili kwa Wanafunzi wa Shule za Msingi, Sekondari na Vyuo vikuu na vya kati ili kuwajengea uwezo na uelewa wa kujitambua na kujua thamani yao katika jamii" alisema Malisa.
WhatsApp Image 2024-09-25 at 19.04.59_f493107b.jpg

WhatsApp Image 2024-09-25 at 19.04.58_b5b97833.jpg
Naye, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Benjamin Kuzaga ameeleza kuwa Jeshi la Polisi kupitia Dawati la Jinsia na Watoto litahakikisha linawafikia wanafunzi wote wa Shule za Msingi na Sekondari, Vyuo vikuu na vya Kati kwa kuwatumia Maafisa Polisi Jamii na Wakaguzi na Polisi Kata waliopo kila Kata.

Kwa upande wake Mkuu wa Dawati la Jinsia na Watoto Mkoa wa Mbeya Mrakibu Msaidizi wa Polisi (ASP) Veronica Ponera amewataka wanafunzi wa Shule za Msingi na Sekondari kushirikiana na Jeshi la Polisi, Wazazi na Walimu kwa kutoa taarifa za viashiria vya ukatili bila kuogopa ili wasiharibiwe na kupelekea kutofikia ndoto zao za kimaisha.

Kampeni ya Tuwaambie kabla hawajaharibiwa kitaifa ilizinduliwa Agosti 29, 2024 Mkoani Njombe na Mkuu wa Mkoa huo Mhe Anthony Mtaka ikilenga kutoa elimu ya kujitambua kwa Wanafunzi ili kuwaepusha dhidi ya uharibifu unaosababishwa na utandawazi na kuiga matendo mabaya kama vile ulevi, matumizi ya dawa za kulevya na mapenzi ya jinsia moja (ushoga).
 
Back
Top Bottom