Pre GE2025 Wanawake Dar kuandaa tukio kusherekea mafanikio ya Rais Samia

Pre GE2025 Wanawake Dar kuandaa tukio kusherekea mafanikio ya Rais Samia

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Cute Wife

JF-Expert Member
Joined
Nov 17, 2023
Posts
1,906
Reaction score
5,000
Wakuu,

Wanawake Dar mmeamua haya na mi sijui, kuna watu wana siri...nimelia sana:BearLaugh::BearLaugh::BearLaugh:

=====



Wanawake wa jijini Dar es Salaam, kwa kushirikiana na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam wanatarajia kuandaa tukio maalum la kumpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa mafanikio yake katika nyanja mbalimbali za maendeleo. Tukio hilo linatarajiwa kufanyika katika siku zijazo, likilenga kuonyesha mshikamano na kuunga mkono juhudi za Rais katika kuleta maendeleo nchini.

Kupata taarifa na matukio yanayojiri kuelekea uchaguzi mkuu kwa kila mkoa ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025

Katika hafla hiyo, wanawake hao wataelezea furaha yao na kutambua juhudi za Rais Samia, ambaye hivi karibuni alichaguliwa tena na chama tawala cha CCM kugombea nafasi ya urais katika uchaguzi mkuu wa mwaka huu2025. Wanawake hao wamesema kuwa Rais Samia amekuwa kielelezo cha uongozi bora na amekuwa akifanya kazi kwa karibu na jamii katika kutatua changamoto mbalimbali zinazowakabili wananchi.

Tukio hili linakuja wakati ambapo nchi inajiandaa kwa uchaguzi mkuu, na wanawake wa Dar es Salaam wanatarajia kuwa sehemu ya mabadiliko chanya yanayoletwa na uongozi wa Rais Samia. Wanawake hao wanatumai kuwa tukio hili litakuwa fursa ya kuimarisha umoja na kuhamasisha wanawake wengine kushiriki katika siasa na maendeleo ya nchi.

Pia soma: Pre GE2025 - Kipindi hiki cha Uchaguzi wanawake wanapata nafasi ya kutosha kushiriki kwenye masuala ya uchaguzi?
 
Huu Mwaka naupite tu

Ukigeuka huku Mama kafanya haya

Kule Mama kafanya lile

Huku Mama katenda lile

Nchi nzima ni Mama Mama Mama ......

Kama mambo yatakuwa hivi, akija Mgeni Kwa mara ya Kwanza Nchini anaweza kuhisi hii Nchi haina Wababa 🙌
 
Hongereni wanawake wa JF, hongera Mello kwa kuwapa fursa wanawake wa JF
 
Huu Mwaka naupite tu

Ukigeuka huku Mama kafanya haya

Kule Mama kafanya lile

Huku Mama katenda lile

Nchi nzima ni Mama Mama Mama ......

Kama mambo yatakuwa hivi, akija Mgeni Kwa mara ya Kwanza Nchini anaweza kuhisi hii Nchi haina Wababa 🙌
Nilifikiri pia kutakuwa na mikakati ya kukabiliana na athari tarajiwa ya kusita misaaada ya baadhi ya taasisi za kimataifa?
 
Nilifikiri pia kutakuwa na mikakati ya kukabiliana na athari tarajiwa ya kusita misaaada ya baadhi ya taasisi za kimataifa?
Hayo mambo ya maana huwa hatuna interest nayo isipokuwa mambo ya kusifu na uchawa
 
Huu Mwaka naupite tu

Ukigeuka huku Mama kafanya haya

Kule Mama kafanya lile

Huku Mama katenda lile

Nchi nzima ni Mama Mama Mama ......

Kama mambo yatakuwa hivi, akija Mgeni Kwa mara ya Kwanza Nchini anaweza kuhisi hii Nchi haina Wababa 🙌
Ngoma inamelizwa sana.
 
Hivi huu ujinga wa uchawa aliuleta nani. Kwa nini wananchi wa Watanganyka kila kinachofanywa na viongozi waliowachagua wanaona ni hisani kwao kutoka kwa viongozi na siyo wajibu wao. Najiuliza sana,

Je ugumu wa maisha ndiyo umeleta ujinga huu?

Je ukosefu wa ajira ndo umeleta ujinga huu?

Je ukosefu wa elimu ndiyo umeleta ujinga huu?

Je wanaofamya ujinga huu ni kwa manufaa binafsi au taifa?

Je Taifa limegawanyika? Wasiopenda huu ujinga na wanaopenda huu ujinga?

Ni ujinga sababu km ni jambo jema kwa nini wasiwe wanawafanyia wazazi wao kwa kuwashukuru kuwaleta duniani, kuwalea na kuwasomesha?

"Illiteracy and ignorance are eating Africa". With regard to the above descriptions discuss this contention with reference to Tanzanian citizens (50 marks). 😃😃
 
Aisee wanawake Akili zenu ni fupi mno...Acha trump aendelee kubana pesa yake
 
Wakitoka hapo sherehe ili ikamilike wanaenda kumalizia kwa wanaume.
 
Back
Top Bottom