Wanawake Kanuni Za Ndoa.

Hassan Ibungu

Member
Joined
Jul 15, 2018
Posts
5
Reaction score
2
Madhumuni ya ndoa

Ndoa ni haja ya kawaida kwa kila mwanadamu. Inayo manufaa mengi na mazuri, baadhi ya hayo manufaa mengi na mazuri yaliyo muhimu ni haya: Ujengaji wa familia ambayo kwayo mtu anaweza kupata usalama na utulivu wa akili. Mtu ambaye hakuoa au kuolewa hufanana na ndege asiye na kiota. Ndoa hutoa huduma ya hifadhi kwa kila mtu anayehisi amepotea kwenye maisha yasiyo na mpango; mtu anaweza kupata mwenzi wa maisha ambaye anaweza kushirikiana naye katika furaha na huzuni.

Matamanio ya kawaida ya kijinsia yana nguvu na yenye maana. Kila mtu anatakiwa kuwa na mwenzi kwa lengo la kujitosheleza kijinsia kwenye mazingira yaliyo salama na tulivu. Kila mtu anapaswa kufaidi raha mustarehe ya kijinsia katika namna iliyo sahihi na inayostahiki. Wale wanao jiepusha na ndoa mara kwa mara husumbuliwa na maradhi ya kimwili na kisaikolojia.

Maradhi hayo na matatizo fulani ya jamii ni matokeo ya moja kwa moja ya vijana kujiepusha na ndoa.

Uzazi: Kupitia kwenye ndoa, binadamu wanaendelea kuzaana. Watoto ni matokeo ya ndoa na ni vipengele muhimu katika kuimarisha misingi ya familia na halikadhalika kama chanzo cha furaha kwa wazazi wao. Msisimko mkubwa sana umebainishwa kwenye Qur’ani Tukufu na Hadith kuhusu ndoa na kupata watoto. Mwenyezi Mungu Mweza wa yote anasema kwenye Qur’ani Tukufu:

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…