Zipo sababu kama tatu hivi;
1. Wengine hupenda ili nyeti zao zisipanuke, wachache kukwepa maumivu
2. Watu wengi hatuna mazoezi, kazi tunazofanya hazichangamshi misuli hivyo kukosa pumzi. Hii humuwia ngumu mwanamke kupushi pindi ajifunguapo. Ulishaona swala/mbuzi anashindwa kujifungua?
3. Kula vyakula vya protini na mafuta, hivyo mtoto kuwa mkubwa awapo tumboni. Sasa mtoto akiwa mkubwa plus mdada hana pumzi kwa kukosa zoezi, lazima tu apitie kisu. Wazee zamani walikuwa na falsafa zenye akili; kwa mjamzito nyama za ndani ni mwiko, akila mayai mtoto atanyonyoka nywele, etc. Iliwasaidia mama zetu