Nchi ngumu sana hii! Watu wanapiga hela za walipa kodi, walipa kodi wenyewe wanataka majibu ya kwa nini wanawake huvaa kanga wakati wa kupiga deki.
Tena kwa msisitizo, mlipa kodi anataka majibu! Na siyo maelezo!!
Mabuti ya kijeshi uyaone mafupi mepesi/
Yani kama vile simple toka nduki toka lesi/
Ka risasi ya bunduki au jeti/
No kunyuti no kuketi, wape nafasi wakushoot/
Kama Malcolm X usikubali kubaki/
Uwe pimbi upewe kesi/
Ikibidi jitose ndani ya dimbwi la kinyesi/
Sio suala la uoga,kuogopa ukunguru/
Ila Bora kurogwa kuliko kukosa uhuru/
Wapi Shemponda wapi Jenerali Komba/
Siri Kali Sera Kali cheza mbali na wajomba/
Kimbiaa, mitihani imevuja nyie hamjasikia!?/
Yanini kusoma huku elimu inanunuliwa/
Kimbiaa, Nchi imeshauzwa hii hamna kusikilizia/
TANESCO, Madini Hadi Air Tanzania/
Watoto wa uswazi hawana matumaini/
Ndoto zao ujambazi sababu ya umaskini/
Matapeli wenye shahada kila hatua tatu/
Makahaba wa miaka kumi na tatu/
Maskani kamsitu, vicheche na machatu/
Usipite pekupeku bila kuvaa viatu/
Aaaah Kimbiaaaaaaaa
Rest Easy LANGA (RIP)