Wanawake mnapenda gari za aina gani?

Simplicity.

JF-Expert Member
Joined
Dec 19, 2013
Posts
2,636
Reaction score
1,662
Wakuu, nafuata ule msemo kuwa kama una silaha, hata bomu la maangamizi na adui anakusumbua, wewe tumia tu, kwa hiyo ni ujinga kuwa na ulimbo lakini ndege wanakusumbua na wewe unawaangalia.

Sasa naona wanawake wamepanda tena daraja, hasa hawa wa mjini Dar, kuna vigari vyetu hivi kama corolla, vits, etc., naona siku hizi wanaviona kama maguta tu, nani kawafundisha, sijui! Duh, hali ni mbaya.

Mwezi uliopita nilikuwa sehemu mjini kwenye mkutano, sasa ikawa mida ya jioni mkutano umeisha ndio tunatawanyika. Kuna mdada mmoja, nikaona anahaha namna gani ataenda nyumbani, mie nikawa msamaria mwema kwa kumwambia, si tunaenda njia moja, twende nikupe lift, duh, akajibu "kwa usafiri gani, aku", huyo akawa ameishia, mara akaenda kupanda gari ya jamaa mwingine! Kwa sababu nilipata kizunguzungu kutokana na jibu lake hata sikujua alipanda gari ya aina gani.

Sasa wanawake wa mjini naona kila siku mnapanda bei, mnapenda gari gani? Ili nami ninunue tuheshimiane.
 
Lengo lako la kununua gari ni ili uwape wanawake lift?
Hii ndio shida ya kutokuwa na vipao mbele ktk maisha, anyway ngoja waje wenyewe watakujibu ipasavyo.
 
Lengo lako la kununua gari ni ili uwape wanawake lift?
Hii ndio shida ya kutokuwa na vipao mbele ktk maisha, anyway ngoja waje wenyewe watakujibu ipasavyo.

Mkuu hizo dharau wewe unaona sawa? Yaani mwanamke mpaka anakacha lift ya gari, sio kabisa.
 
Ukiishi kwa kuwafurahisha wengine, Amini nakuambia hutaendelea kamwe.
 
Ukiishi kwa kuwafurahisha wengine, Amini nakuambia hutaendelea kamwe.

Mkuu nyie wenyewe sasa hamtaki wanaume wasio na hela wala gari, bora nitafute mnachotaka ili msinisumbue.
 
Ingekua heshima ni gari mafundi garage wangeongoza kuheshimiwa...

Kumbe huna taarifa, jinsi mafundi wanavyoiba wake za watu mjini. Hao jamaa ukiwaachia gari wakutengenezee, mwisho wa siku lazima wapige nayo misele town kabla hujaenda kuichukua, na hata ukikutana naye anaiendesha atakuambia nilikuwa naitest kama ishakuwa poa.
 
Hatari sana wenzio tunawapandisha bodaboda watoto wakati hadi basi
 
Kuna jamaa alikuwa analalamikia makalio yake, au ndio hizi gari za akina wema? Sio Murano kweli? Siigusi.
 

mkuu tunaongelea heshima sio kuiba wake za watu

Hata mimi ninayeuza dawa za mende,kunguni,viroboto mbona naiba sana wake za watu na sina gari?!
 
Hahaha! Aisee! Hii dar ishakuwa sheedar! Wacha nihame!!
 
Mi napanda ule mgari mkuubwaa semi trela !yani nkiwa mule naskia burudani walah!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…