JF-Expert Member
- May 27, 2014
- 2,118
- 4,863
Nimekaa hapa nakula mvinyo kuna bajaji kapita kakuta mabinti wawili wanapita kasimamisha kauliza “mnaenda” wakamjibu “hatuendi” , bajaji kakomaa “mnaenda wapi” wamemjibu tumefika. Bajaji kakomaa “twendeni basi niwasogeze”. Mabinti wamepanda bure.
Ukute bajaji hili hili liwapite madume wenzie uone linavyowakazia. Kuna kidemu nilikua nakipa lift kitoto cha jirani leo kimepata kazi kimenunua gari kimenipita mahala nilikua nanyoosha zangu miguu hata kuniuliza kama nafanya mazoezi.
Inashangaza sana wanawake ambao ndiyo wachoyo wa kutoa lifti kwa wanaume, ila sisi wanaume ndiyo tunajikomba kuwapa lift lakini tunawafungia vioo vidume wenzetu kwenye maswala ya lift.
Ukute bajaji hili hili liwapite madume wenzie uone linavyowakazia. Kuna kidemu nilikua nakipa lift kitoto cha jirani leo kimepata kazi kimenunua gari kimenipita mahala nilikua nanyoosha zangu miguu hata kuniuliza kama nafanya mazoezi.
Inashangaza sana wanawake ambao ndiyo wachoyo wa kutoa lifti kwa wanaume, ila sisi wanaume ndiyo tunajikomba kuwapa lift lakini tunawafungia vioo vidume wenzetu kwenye maswala ya lift.