Wanawake wana haraka kuliko miaka 60 ya Uhuru

Wanawake wana haraka kuliko miaka 60 ya Uhuru

kavulata

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2012
Posts
13,778
Reaction score
14,214
Unapouliza mapungufu kwenye masuala ya demokrasia yetu nchini ni rahisi sana kusikia kuwa demokrasia yetu bado ni changa sana ukilinganisha Na nchi za marekani Na ulaya, hivyo bado tunajifunza polepole ili tufike kwa wenzetu wenye zaidi ya miaka 200 na kuombwa tusijilinganishe nao.

Uchanga huu wa miaka 60 unatumika kuhalisha mapungufu yaliyoko kwenye demokrasia Na maendeleo nchini. Hata hivyo kasi tuliyonayo kwenye haki za wanawake kwenye uongozi kuelekea 50/50 ni kubwa kuliko nchi ya Marekani, Uchina, India, Uarabuni Na Ulaya zenye zaidi ya miaka 200 ya kujitawala. Hadi leo Marekani haijawahi kuwa Na Rais mwanamke, hawajafikia 50/50 kwa wabunge Na mawaziri. Hapa kwetu tunataka kuaminishwa kuwa kwa miaka 60 wanawake walionewa sana na wanaume hivyo tumechelewa sana kufikia 50/50.

Hebu tufanye utafiti kutoka kwa wenzetu wenye zaidi ya miaka 200 ya Uhuru Na demokrasia ni kwanini wanawake sio 50/50 kwenye ofisi zote hadi Leo. Hii itatusaidia tusijekuharibu nchi yetu au kutengeneza shida ambayo itakuwa ngumu kuitatua huko mbeleni. Lazima majibu wanayo.

Kwanini kuna wakati tunaona miaka 60 ni michache lakini kwa wanawake tunaiona ni mingi mno?
 
Wao wazungu ni wajanja. Wanatuletea mambo meusi ili tuzidi kuwa masikini. Mambo ya 50/50 ni upumbavu. Watu wapewe uongozi kulingana na uwezo walionao haijalishi jinsia.

Mfano wanawake wamejazana bungeni kwa mgongo wa 50/50 na hawana impact yoyote zaidi ya kutuchelewesha. Wafanye kazi wenye uwezo nazo sio kujazana bungeni kama kwaya ya wasabato.
 
Wao wazungu ni wajanja. Wanatuletea mambo meusi ili tuzidi kuwa masikini. Mambo ya 50/50 ni upumbavu. Watu wapewe uongozi kulingana na uwezo walionao haijalishi jinsia.

Mfano wanawake wamejazana bungeni kwa mgongo wa 50/50 na hawana impact yoyote zaidi ya kutuchelewesha. Wafanye kazi wenye uwezo nazo sio kujazana bungeni kama kwaya ya wasabato.
Miaka 60 inatosha sana kuwa Na tume huru ya uchaguzi, katiba inayotokana Na watu, Uhuru wa habari Na wakisiasa. Miaka 60 ni michache sana kwa wanawake kuona wamechelewa sana. Kifupi tufanye utafiti ili kuona kama ni kweli miaka 60 ni michache sana kuwa Na demokrasia inayokubalika kwa vyama Na watu wote, ama ni mingi sana kwa wanawake kuwa hivyo walivyo sasa.
 
Kuwa na Kiongozi Mwanamke ni dalili za sikuza mwisho.
Wanawake kutembea Uchi,Fashion shows ni dalili ya zama za mwisho.
Wanawake kudai talaka na kzaa na wanaume bila kuolewa ni dalili ya zama za Mwisho.
Kudai Haki sawa na wanaume katika mirathi ,ajira, na mengineyo ni dalili ya zama za mwisho.
MWISHO NDIO HUU UMESHADHIRI
TUNGOJE KUREJEA KWA YESU
NA JUA KUCHOMOZA UPANDE WA MAGHARIBI
 
Kuwa na Kiongozi Mwanamke ni dalili za sikuza mwisho.
Wanawake kutembea Uchi,Fashion shows ni dalili ya zama za mwisho.
Wanawake kudai talaka na kzaa na wanaume bila kuolewa ni dalili ya zama za Mwisho.
Kudai Haki sawa na wanaume katika mirathi ,ajira, na mengineyo ni dalili ya zama za mwisho.
MWISHO NDIO HUU UMESHADHIRI
TUNGOJE KUREJEA KWA YESU
NA JUA KUCHOMOZA UPANDE WA MAGHARIBI
Tujiulize maswali wenyewe ni kwanini mataifa makubwa yenye uchumi mkubwa Na ustaarabu wa miaka mingi kama vile Uingereza, Marekani, France, German, Uchina, Urusi, Spain, Saudi Arabia, Dubai, nk hawajafika mbali sana kwenye 50/50? Kwanini Tanzania maskini Na miaka 60 tu inaonekana kama mama, bibi, shangazi, dada, Na watoto zetu hatuwapendi, tunawaonea, Na kuwanyima kila kitu?

Tatizo kubwa linakuja, tujiandae nalo.
 
Tujiulize maswali wenyewe ni kwanini mataifa makubwa yenye uchumi mkubwa Na ustaarabu wa miaka mingi kama vile Uingereza, Marekani, France, German, Uchina, Urusi, Spain, Saudi Arabia, Dubai, nk hawajafika mbali sana kwenye 50/50? Kwanini Tanzania maskini Na miaka 60 tu inaonekana kama mama, bibi, shangazi, dada, Na watoto zetu hatuwapendi, tunawaonea, Na kuwanyima kila kitu?

Tatizo kubwa linakuja, tujiandae nalo.
Tunatafuta sifa itakayotutafuna Kwa muda mrefu sana,na kama kawaida hatutajua tatizo limeanzia wapi.

Sent from my Nokia 5.1 Plus using JamiiForums mobile app
 
Hili swala umeongea hapa ni swala mtambuka na fikirishi sana. Ni kama mbinu mkakati ya mataifa ya nje katika kutudhoofisha kiintelijensia.

Naona kama sasa hivi mdororo wa uchumi umeongezeka na ufanisi wa kiutendaji serikalini umezidi kushuka kwa kasi sana sababu ya ongezeko la watendaji wasio na umeme unaotakiwa kuweka mambo sawa.

Familia kwasasa sio tena nguzo imara ya taifa sababu hakuna akina mama kwenye familia bali kuna wanawake kwenye familia. Familia hazipo imara tena kama miaka ile ya awali bali familia zimekuwa ni changamoto.

Pesa nyingi inakwenda kuratibisha haya maswala ya kijinsia ya kike ambayo hupewa majina mbali mbali ya kiupendeleo.

Tanzania na mifumo yake wanalenga nini siku zijazo?! Hadi sasa tufanye tathimini kama hii miaka 60 ya kupigia domo na kukurukakara hizi ajenda za kijinsia tumepata mafanikio gani na hasara gani!


Kuna ukakasi mwingi sana kwenye hili jambo ......!
 
Tunatafuta sifa itakayotutafuna Kwa muda mrefu sana,na kama kawaida hatutajua tatizo limeanzia wapi.

Sent from my Nokia 5.1 Plus using JamiiForums mobile app
Wanawake tuliolazimisha wawe wabunge
Tunatafuta sifa itakayotutafuna Kwa muda mrefu sana,na kama kawaida hatutajua tatizo limeanzia wapi.

Sent from my Nokia 5.1 Plus using JamiiForums mobile app
Kama tunaamua kukimbia basi tukimbie hata kwenye mambo yetu yote yakiwemo yale ya haki za watu, utawala bora, demokrasia, na wanawake. Sio tuwe navrangi mbili kama kidonge kwa tetracycline, upande tuko miaka 60 na upande tuko miaka 300.

Kunawanawake tulilazimisha wawe wabunge, mawaziri, DC, RC, na wawakilishi kwenye serikali za mitaa, lakini hawana tofauti na wanaume katika kuwasaidia wanawake wenzao, tena wanaume wanasaidia wanawake kuliko wanawake wenzao.

Kule Kilimanjaro na Moshi kuna wanawake wengi waliosaoma, wabunge, na viongozi mbalimbali lakini wanawake wenzao hadi kesho hawamiliki ardhi, wananyimwa haki ya kumiliki ardhi ya wazazi wao, kama wanawake wasaomi hawawezi kuwasaidia wezao kwenye kudai haki yao ya kumiliki ardhi kwenye kabila lao tu je wataweza kwa nchi nzima?
 
Msichoelewa ni kuwa hao wanawake mnaopigia makelele ni sehemu ya mpango wa wafadhili na lengo kubwa hasa ni kuweza ku penetrate na kujichotea rasilimali tu. Wanajua mtavurugana tu mnyukano wenu wao kwao ni furaha maana kutakuwa na less supervision.

Dalili zinaonesha dili mbovu nyingi zitafanyika chini ya utawala huu and trust me ni dhahiri ufanisi wa kitendaji umeshuka sana katika kipindi kifupi tu toka tufanye transition toka kwa JPM. Najua mashabiki mandazi wa mama mtakuja kunishambulia ila vitu viko dhahiri kwenye ground za kitaa.
 
Hili swala umeongea hapa ni swala mtambuka na fikirishi sana. Ni kama mbinu mkakati ya mataifa ya nje katika kutudhoofisha kiintelijensia.

Naona kama sasa hivi mdororo wa uchumi umeongezeka na ufanisi wa kiutendaji serikalini umezidi kushuka kwa kasi sana sababu ya ongezeko la watendaji wasio na umeme unaotakiwa kuweka mambo sawa.

Familia kwasasa sio tena nguzo imara ya taifa sababu hakuna akina mama kwenye familia bali kuna wanawake kwenye familia. Familia hazipo imara tena kama miaka ile ya awali bali familia zimekuwa ni changamoto.

Pesa nyingi inakwenda kuratibisha haya maswala ya kijinsia ya kike ambayo hupewa majina mbali mbali ya kiupendeleo.

Tanzania na mifumo yake wanalenga nini siku zijazo?! Hadi sasa tufanye tathimini kama hii miaka 60 ya kupigia domo na kukurukakara hizi ajenda za kijinsia tumepata mafanikio gani na hasara gani!


Kuna ukakasi mwingi sana kwenye hili jambo ......!
Hatuna muda wa kujiuliza ni kwanini mataifa makubwa yote duniani kote yanakwenda mwendo wa kinyonga kwenye haki za wanawake wakati wao wamesoma sana na wameendelea sana na wana demokrasia pana na wana mahakama imara na wanawake wengi wamesoma sana?

Nadhani tunachofanya sisi sio kile kinachotakiwa. Kinachotakiwa ni kuondoa vikwazo vyote kwa wanawake katika mambo yote ya elimu, siasa, uchumi na ajira ili mwanamke na mwanamke wawe na fursa sawa kwenye kupata elimu, haki, afya, uchumi, ajira, kumiliki ardhi na uongozi kwa kutumia vigezo. Yaani uwanja wa kumbilia kati ya mwanamke na mwanaume uwe sawa bila kusaidia (manipulate) upande wowote, yaani survival of the fittest katika kila sector. Mwenye sifa zaidi ataonekana na kuchaguliwa sio kwa kutumia huruma, upendeleo nabutashi wa ni mwanamke au mwanaume. Hiki ndicho wanachokifanya mataifa makubwa.
 
Viti maalum vya ubunge vifutwe, wabunge wote wapatikane kwa kupigiwa kura na wananchi. Nchi inaingia gharama kubwa kuwa na idadi kubwa ya viongozi wasiongeza tija yoyote.
Utakuta ni mbunge wa viti maalumu bungeni lakini wanawake wa kibila lake hawamiliki ardhi kwao, ni wakimbizi. Anasaidia nini sasa huko bungeni na kwenye kabila.
 
Msichoelewa ni kuwa hao wanawake mnaopigia makelele ni sehemu ya mpango wa wafadhili na lengo kubwa hasa ni kuweza ku penetrate na kujichotea rasilimali tu. Wanajua mtavurugana tu mnyukano wenu wao kwao ni furaha maana kutakuwa na less supervision.

Dalili zinaonesha dili mbovu nyingi zitafanyika chini ya utawala huu and trust me ni dhahiri ufanisi wa kitendaji umeshuka sana katika kipindi kifupi tu toka tufanye transition toka kwa JPM. Najua mashabiki mandazi wa mama mtakuja kunishambulia ila vitu viko dhahiri kwenye ground za kitaa.
Toa mfano.
 
Toa mfano.
Mfano gani unaotaka mkuu?

Kama msimamizi wa nidhamu ataamua kubembeleza wanafunzi wachomekee mashati badala ya ku impose adhabu kali kwa ambaye hatachomekea unatarajia mabadiliko ya tabia kweli?

“Tufanye kazi jamani sote ni watu wazima hamna haja ya kutumbuana.”
Umwambie mfanyakazi wa kitanzania hivi unatarajia mabadiliko kweli?
 
Viti maalum vya ubunge vifutwe, wabunge wote wapatikane kwa kupigiwa kura na wananchi. Nchi inaingia gharama kubwa kuwa na idadi kubwa ya viongozi wasiongeza tija yoyote.
Kule Marekani mpaka leo hii kazi moja hiyohoyo mwanaume anapata mshahara mkubwa kuliko mwanaume. Nikamuuliza mtu kwanini iwe hivyo, akaniambia hata ufanye nini kwa siku 30 za mwezi kuna masaa mengi ya kazi ambayo mwanamke atayatumia kwa kazi/shida zake binafsi na familia na muda ataomba msaada au ushauri kutoka kwa mwanaume ili kufanikisha kazi za mwajili wake.

Wazungu wamefanya utafiti kuwa wanawake ni watu wanaoomba na kutegemea ushauri zaidi kabla ya kuamua. Hivyo kufanya vizuri au kukosea kunategemea nani amemshauri kwenye jambo husika. Hii ndiyo tabia pekee wanayoiogopa wazungu kwa wanawake. Ili mwanamke afanye vizuri lazima awekewe very strong watu wa kumshauri.
 
Mfano gani unaotaka mkuu?

Kama msimamizi wa nidhamu ataamua kubembeleza wanafunzi wachomekee mashati badala ya ku impose adhabu kali kwa ambaye hatachomekea unatarajia mabadiliko ya tabia kweli?

“Tufanye kazi jamani sote ni watu wazima hamna haja ya kutumbuana.”
Umwambie mfanyakazi wa kitanzania hivi unatarajia mabadiliko kweli?
Hiyo kweli, 87% ya watoto waliosoma na kumaliza vyuo vikuu vizuri ni watoto wa baba wakali sana.
 
Hiyo kweli, 87% ya watoto waliosoma na kumaliza vyuo vikuu vizuri ni watoto wa baba wakali sana.
Na sikuzote baba huonekana katili hadi pale utapofanikiwa ndio utaona kumbe mzee alikuwa jembe.
 
Back
Top Bottom