Wanawake wana haraka kuliko miaka 60 ya Uhuru

50/50 ni scam

Taifa na uchumi wa nchi hujengwa na wanaume !!?
Tafsiri yetu ya kujenga uchumi sio sawa. Kuna watu wanaodhani ili mama aonekane anafanyakazi lazima nae aache watoto na nyumba akashinde kazini apewe mshahara. Uchumi mzuri ni ule ambao unasababisha watoto, baba na mama wana afya, elimu na maendeleo ya kiuchumi. Uchumi wa mwanamke kushinda kazini pia ni uchumi unaosababisha watoto wasiwe na usimamizi majumbani na baba na mama wasielewane, jioni baba na mama wote wamechoka na kusubiri wapewe ripoti kuhusu watoto wao kutoka kwa house girl, majirani na ndugu walioshinda na watoto wao.

Familia ambazo baba na mama wote hawashindi nyumbani inazalisha watoto watoro shuleni wanaofeli masomo, makahaba, mashoga, na watumia dawa za kulenya. Vinginevyo baba lazima awe mkali sana kwa watoto. Mama siku zote sio mkali na wqtoto hawaogopi mama.
 
Mwanamke mwenye uwezo na shupavu ni yule anaeamua vizuri au vibaya cha kufanya yeye mwenyewe zaidi bila kutegemea ushauri na msaada or approval kutoka kwa wanaume au wanawake. Anakosea na kupatia yeye mwenye. Yaani anaweza kumuadhibu vikali mtoto wake mwenyewe bila kumsubiri baba aje kumuadhibu. Wanawake wengi wanaadhibu watoto wa kambo na kushindwa kuwaadhibu wale wa kwao wenyewe.

Wanawake shupavu ni kama akina Magreth Thatcher aliyekuwa wqziri mkuu wa uingereza. Akina mama wa hivyo hawazaliwi wengi, mimi ninae mtoto mmoja tu. Ushujaa kama huu unaanzia utotoni, shuleni, vyuoni na kazini. Yaani mwanamke anasoma na kupata marks zake mwenyewe, anaweza kusema YES kwa anachokubaliana nacho au NO kwa asichokikubali kwa mtu yeyote bila kujali consequences, na anaweza kushuhulika na matokeo yake.

Mtu aliyesaidiwa kufaulu hawezi kuwa kiongozi mzuri hata awe ni mwanaume.
 
Sisi hiyo ilitokea bahati mbaya hakuchaguliwa
 
Point yako ni nzuri ila umeboronga hapo mwishoni,au kuna tenda ya kuprint t-shirt walikunyima?
 
ppl
50/50 ni scam

Taifa na uchumi wa nchi hujengwa na wanaume !!?
Nionavyo mimi tanzania hatuna tatizo la demokrasia wala jinsia bali tuna tatizo la wizi wa kura na kupika matokeo, wizi na ubadhilifu wa mali ya umma, ukwepaji kodi, rushwa na ukosefu wa huduma za msingi kwa wananchi, baaaasi. Tutumie rasilimali katika kurebisha haya sio demokrasia wala jinsia. Kurekibisha hakuhitaji pesa hata kidogo, ni wananchi kusema acheni wizi kusanyeni kodi, ondokeni, nk.
 
Haya maoni yako yamekaa kiimani zaidi.
 
Inaweza isiwe mwisho wa dunia, maana walikuwepo akina Cleopatra huko nyuma pia. Tunachosema tusikimbilie kujaza wanawake kwenye uongozi kama revenge, fidia, na huruma tu, bali wachukuliwe wale kweli wanaojitokeza kwenye jamii na kuonekana wana uwezo, wana tabia ya kuweza mambo, wenye tabia ya kufanya maamuzi wenyewe tangu kwenye masomo yao shuleni na vyuoni, kazini na kwenye jamii. Wanawake wa hivi (Iron ladies) sio wengi ndani ya jamii duniani. Ndiyo maana hata ulaya na marekani wanalega kwenye 50/50. Tusifanye zoazoa tukalidhuru taifa. Na shida kubwa iko kwenye kurubuniwa na wanaume (maadui na wezi) kutoka ng'ambo.

Hii ya kurubuniwa ndio sababu kuu iliyosababisha makabila mengi kuwanyima urithi wa ardhi wanawake kwa kuogopa wasije wakarubuniwa na wanaume wao na kuiuza ardhi ya ukoo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…