Wanawake wanajishtukia hawataki tena uchumba

Peter Mwaihola

JF-Expert Member
Joined
Jun 23, 2022
Posts
276
Reaction score
460
Ni ukweli wala sio utani kwamba baadhi ya wanawake ambao bado hawajaolewa hawavutiwi tena na hatua ya uchumba kabla ya ndoa.

Utafiti mdogo uliofanyika unaonyesha kuwa wanawake wamechoshwa na uchumba sugu, kudanganywa na wanaume wanao ahidi kuwaoa kisha kutelekezwa baada ya muda fulani kupita.

Aidha wanawake wengi wanaona sulihisho la tatizo hili ni kukataa kukaa kwenye hatua ya uchumba kwa muda mrefu na wanaume wanaojitokeza kuwapenda ili kupunguza uwezekano wa kuachwa solemba.

Miongoni mwa wanawake walioguswa na utafiti huu wanasema hawawezi kuingia kwenye uhusiano na mwanaume ambae hana nia ya kuoa hivi karibuni.

"Kama mwanaume ananipenda basi anatakiwa aende nyumbani ajitambulishe kisha afuate taratibu atakazoambiwa ili anione" anasema Taji ambaye ni mwanafunzi wa shahada ya sheria moja ya chuo kikuu nchini Tanzania.

Anasema wanaume wengi wamekuwa waongo kwa wanaweke wengine huwazalisha na kutokomea kusiko julikana na kukwamisha ndoto za wanaweke.

Hata hivyo wanaume nao wana msimamo wao kuwa hawawezi kuoa mwanamke wasiyemjua vizuri tabia, na mwenendo hivyo ni vema kupitia hatua ya uchumba kabla ya ndoa ili kupata muda wa kumsoma vizuri na kujua namna ya kuishi nae katika ndoa.

Aidha wanaume wanaeleza kuwa baadhi ya wanawake hatawataki uchumba kwa sababu ya tabia zao mbaya ili zisiijulikane mapema hivyo wanatafuta mwanaume atakae waoa kwa haraka bila kuwachunguza jambo ambalo ni kama kuuziwa mbuzi kwenye gunia.

Sababu nyingine zilizobainika kupelekea baadhi wanawake kutotaka uchumba ni kuepusha shinikizo la wazazi na jamii katika kuvuruga uhusiano wa wahusika kabla ya kufikia ndoa.

Je wewe una mtazamo gani kuhusu kuingia kwenye uchumba kabla ya ndoa?.

(Imeandikwa na Peter Mwaihola)
 
Kama mlifanya utafiti kwa mifano ya huyo mwanafunzi wa chuo basi huo utafiti hamjaufanya kwa kina, kwasababu mmefanya tafiti kwa mabinti ambao hawajaingia hata mtaani na hawajui nini maana ya ndoa.

Mmefanya utafiti kwa wanafunzi ambao bado hawajawahi hata kujitegemea, na hawajui hata upweke unavyo tafuna ukiachilia ndoa.
 
Wanaume nao wanahofu ya kuachwa uchumbani. Unakuta mdada ana wachumba mia, anachekecha wa kumuoa, wengine wanamuonjea mpiko na hawamuoi. Zamani ilikuwa haiwezekani kufikisha wanaume watatu wanaotaka kuoa, wanawake walioolewa fasta na wa kwanza aliyejitokeza.
 
Sasa mtu hauna bikra, umeliwa na wanaume tofuti zaidi ya 10 halafu unademand mimi nije kwenu kwanza kuomba ridhaa ya wazazi wako, ridhaa gani hiyo ninayokuja kuomba? Kama ridhaa ni kitu muhimu ni kwann haukuzingatia kujitunza mwili wako usiguswe hata na nzi ili nikija kuomba ridhaa nijue nakuja kutunukiwa usichana wako ambao uliutunza for the "One".

Me nadhani ifike muda wadada waanze kutumia akili sawa sawa. Kama unaweza kuoga vizuri, ukajiremba, na kufanya mambo mengine kama mwanadamu na sio nyani then hili ni dogo sana kukushinda.

Huwezi shindwa kuelewa tofauti yako na bikra, wewe hauna hadhi au ile heshima ya mke mwema, wewe ni wale wanaochezewa. Ukitaka kujiweka nafasi nzuri anza kujishusha na kutambua kuwa wanaume watakithamini kwa mchango wako kwenye maisha yao sio wewe kudemand ufanyiwe vitu special kufurahisha akili yako wakati umri unasogea.

Wanawake hawaambiani ukweli hata siku moja. Wakikutana wanafarijiana kuwa wapo wanaume watakuja kuwaoa na kuwapa hadhi ya mke, ila hawaambiani ukweli kuwa hawana hadhi ya mke sababu walishatumika nani anataka kuoa mwanamke ambaye ameshatembea na wanaume kadhaa, hivi unajiskiaje unakutana na mshikaji wanasalimiana na mkeo halafu unakuja ambiwa huyu mwana alikuwa ni boyfriend wa mkeo kipindi wapo chuo walikulana sana na waliishi geto, hayo mapenzi ya kuendelea kumpenda yanatoka wapi hapo.

Waacheni waendelee kuweka masharti na standards za kibwegebwege wakitarajia kuwa miaka hii kuna wanaume wa sampuli ile ya mwaka 1947. Hii breed ya wanaume wa kisasa hawa ndio ya kuiwekea masharti hii?

Kama wanapiga kibuti mwanamke bikra halafu wewe uje na masharti lukuki na bikra hujui ulidondosha wapi huko.

Kila la heri ukisubiria wakukulipia mahari na hautaki kuishi nae kinyumba ile hali "body count yako inasoma 15 Men.
 
So what?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…