Hivi inakuwaje Mwanamke mwenye elimu tu nzuri anatumia Medicated soap kuogea??..Medicated soap ni kama tetmosol,dettol n.k
Hizi sabuni ni kwa ajili ya kuulia bacteria na zinatumika tu pale ambapo mtu unakuwa exposed kwenye mazingira machafu sana
Unapotumia hizi sabuni frequently zinaenda kuua normal flora wa kwenye ngozi na pia wale wa kwenye uke..matokeo yake mtu unapata mashambulizi,,fungus kama candida wanatake over na kusababisha candidiasis na pia magonjwa mengine kama UTI yanafwata
Na kwa wanaume sio nzuri pia ila madhara ni makubwa kwa wanawake kutokana na maumbile yao
Ndugu changamoto kubwa ya Wasomi wetu wanaenda shule kupata Elimu (Vyeti) na sio kupata Akili (Kukuza Uelewa) jambo linafanya washindwe hata kuwa na uelewa wa mambo ya Msingi katika uhalisia wa Maisha.