"Wanawake/wanaume weusi wanajidharau sana"... je nikweli?

Imany John

JF-Expert Member
Joined
Jul 30, 2011
Posts
2,935
Reaction score
1,185
Wanajamvi natumaini mu wazima wa Afya!<br />
Nimekuwa nikifiria sana kwa muda mrefu na nikaona ni vizuri kushirikiana mawazo,<br />
Ndugu yangu MKESHAJI AMEWEKA CLEAR MAWAZO yangu kwa thread Yake ndo mana nimeuliza hivi.<br />
<br />
Kwa upande wa pili wanawake/wanaume waeusi kwa ngozi zao wanajidharau(they feel inferior) just kwa weusi wa Ngozi zao na hili linathibitishwa dhahiri kwa wimbi kubwa la wadada/wakaka weusi wanavyohaha kujichubua nyuso zao ili wawe weupe.<br />
<br />
Je ni kweli Wanawake/wanaume weusi wanajidharau??<br />
<br />
Note.:sio wanawake na wanaume wote.
 
Umesema TAYARI IMETHIBITISHWA alafu unarudi kuuliza KAMA NI KWELI?!

Wewe ndio utuambie....
 
Umesema TAYARI IMETHIBITISHWA alafu unarudi kuuliza KAMA NI KWELI?!<br />
<br />
Wewe ndio utuambie....
<br />
<br />
Kama unakubali unga mkono my sis lizzy.
 
zaidi ya wanaume wa Congo zijaona wanaume wengi wanajichubua na nadhani sometimes its just going with fashion... kwa kipindi hicho doing something extra does not necessarily mean kwamba mtu hataki alichonacho....

Wazungu wengi wanafanya tanning in order to appear darker...., its just an iconic thing...., ingawa if the community perceives something as beautiful obvious someone who lacks that might have some inferiority complex that she is not beautiful na hii kitu sio sana kwenye ngozi bali ni kwenye size ya mtu btn european countries na African countries

Au Size ya bottom kwa Brazillian Countries..., Size of the chest kwa some european countries... (its all how the community perceives) lakini what matters its how the person appreciates him/herself
 
kama unavyosema sio wote,na wengi wanao kua hivyo sababu hawajiamini ukijiamini.
 
zaidi ya wanaume wa Congo zijaona wanaume wengi wanajichubua na nadhani sometimes its just going with fashion... kwa kipindi hicho doing something extra does not necessarily mean kwamba mtu hataki alichonacho....
<br />
<br />
Only congolies??

Usiwatetee wanaume na wake wa KiTZ.
 
Mimi nijuavyo (Haijathibitishwa) wanaume wenye light skin (weupe) huwa kidogo hawana confidence kama waliyonayo weusi!.
<br />
<br />
So unataka kusema ni sababu za kiurembo tu?
Na sio kujidharau?
 
<br />
<br />
Only congolies??

Usiwatetee wanaume na wake wa KiTZ.

Mkuu most Congo men.., na kuthibitisha kwamba hii ni fashion na perceive ya community mambo ya mkorogo yamepungua siku hizi sio kama zamani... uongo au kweli..???

Zamani mwanambe bila nywele ndefu alikuwa anajiona kama amepungukiwa sana lakini siku hizi unaona wanawake wengi tu wanakata nywele zao fupi na wanaonekana wamependeza/na wanaona wanapendeza....

So its all about fashion na kipindi cha wakati fulani am sure baada ya miaka unaweza kuona watu wanajipaka rangi ili wawe wa blue kama at that time being blue utaonekana ipo cool ni kama kipindi fulani watu walikuwa wanaweka curry kwenye nywele sio kwamba hawapendi nywele zao bali its just the time was like that...

Hivi sasa mkorogo unaonekana kama ni ushamba fulani (au uongo...???)
 
hapa ishu ni kwamba mawazo yako naya fananisha na ya fid q anavyokuambia da mwajuma uswahilini anavyojichubua sio kwamba anakimbia uafrika..

hapa kwa hilo sidhani na walio wengi ni wakutoka uswahilini ndo wanaitikadi hizo..
 
mmhhh
Hatujidharau sababu ya ngozi zetu ..(individual {mtu binafsi})
Bali kuna ambao wanatudharau(saa nyingine wenyewe kwa wenyewe tunadharauliana)
na kuna wengi wanaichukulia hilo dharau kutoka kwa wengine vibaya
ndo maaina wanaishia kujichubua..

kuna mambo mengine yanayochangia pia....
advertisement, peer pressure , media ,
environment ect... ......
 
<br />
<br />
So unataka kusema ni sababu za kiurembo tu?
Na sio kujidharau?

Sio kujidharau LittleX........siamini katika binadamu kujidharau....ukisema kutojiamini yes nitakuunga mkono but not kujidharau.....kujidharau inamaanisha ni kujiona hufai kabisa hata ufanye nini, but kutojiamini ina maana huamini kama unaweza unless uwe na sifa nyingine so unatafuta cha kucompensate............... mf. Mwanaume mweupe anaweza asijiamini mbele ya wanawake kama atakuwa na wanaume wenzie weusi UNLESS aongezee mapompas, avae smart, anukie utajiri n.k (zaidi ya rangi au uasili wake) but kama anajidharau it means atashy away kabisa na kuondoka.
 
Aisee!Mimi ni kijana wa kitanzania,mwafrika,japokua sio mweusi kivile ila najivunia jinsi nilivyo,pia kama nikija kutaka mahusiano nitamuhitaji ambae yuko "natural"!
 
Aisee!Mimi ni kijana wa kitanzania,mwafrika,japokua sio mweusi kivile ila najivunia jinsi nilivyo,pia kama nikija kutaka mahusiano nitamuhitaji ambae yuko &quot;natural&quot;!
<br />
<br />
A gud say paw.
 
Mzuri pesa tu,sura kutambuana kama ndug nyumban kwen,kwa ss vibab ndo vinakul madem w ukwel.so whatever u a b proud an think v ur lyf
 
Mungu katuumba wanadamu na kutupatia akili kumiliki na kutawala viumbe vyote vilivyopo ardhini. Mwanadamu katika uumbaji alikuwa mwa mwisho na baadae Mungu akapumzika na kuangalia vitu vyake vilivyo vyema machoni pake. Uumbaji huu wa aina yake, wa kufanana na yeye aliye juu umetukuka na yeye Mungu akaona vyema na akasema zaeni mkaongezeke mkaiijaze dunia.

Sasa cha kushangaza tunachokiona hapa duniani sasa hivi, wanadada wengi na wakak pia, wanabadilisha ngozi zao zilizoumbwa na mwenyezii Mungu kwa kemikali za kujipaka kwa hiari,wamezifanya ngozi zao kupauka na kuzifanya nyeupe si nyeupe, nyekundu si nyekundu ilimradi tu ni vichekesho huku mishipa ya damu ikionekena bayana. Loh Mungu wangu tuhurumie.

Kutokana na mikorogo, ngozi zao zimebadilika, ngozi ya kenge si kenge ni mabaka mabaka tu mwili mzima, tazama paji la uso jeupe,macho meusi mithili ya miwani ya jua, vifundo vya mikono na miguu vyeusi, ili mradi ni mikorogo tu ya rangi. Eti kisa ni mwenyezi Mungu kakosea kuwapa hao rangi nyeusi.

Achana na ngozi, nywele nazo kazi ni moja tu, unamwangalia msichana au mvulana inakuwa kama ni kichekesho, nyani si nyani, komba si komba, mbega si mbega, basi ilimradi yupoyupo tu. Watu wanahangaika na maisha, kwao mwenyezi Mungu amekosea.

Na ukiwaambia jamani mikorogo hii ina madhara kubwa kwa afya zao, hapo ndipo utapomjua mwanamke wa kibongo/mwanaume..."mwanga we, unanionea wivu we. Kama umefulia, tulia, na kwanza unikome kabisa" Watu hawa sasa hivi wamevuka mipaka na maadili.

sasa hivi wanatafuta uzuri eti wafanane na malaika wa Mungu, wanatumia vidonge na sindano, na hata kemikali za kukuza matiti na makalio..'toba' walah, hivi tunakwenda wapi jamani?? Yale waliyojaliwa hawaridhiki nayo, Mi naona kama wanamtusi Muumba wao.

Sasa maumbile yao yamewageuka na yanakuwa hayana tofauti na matairi ya nyuma ya trekta, yanakuwa ndembendembe, yanakuwa kama kinyago cha m-makonde uchwara.

Sasa hembu sikiliza hii ya firauni, baadhi ya wanaume wa kibongo licha tu ya mavazi yao ya kuvalia nguo mapajani a.k.a kata K-almaarufu, wao sasa wapo wanataka kujibadili ili wawe kama wasichana kimuonekano na nina uhakika kwamba wakipata fursa watatamani kuwa wanadada kamili.

Kuna wanakaka wengi licha ya nywele tu, wanapaka wanja na lipstick, na wengine kuchonga nyusi achilia mbali kubadili sauti na kutembea mithili ya kinyonga kama watoto wa kike.

Ili kujulisha ukweli huu wamedhihirisha kwa kujiita "MASHAROBARO". Hii ni nomino maana yake halisi ni msichana MREMBO. Anajipenda na kujisikia huku akitafuta kwa hamu KUPENDWA KWA HALI NA MALI. Hawa ni masharobaro wa kiume na si wa kike. Bora wangejiita MABAROBARO, Hali kidogo ingekuwa shwari.

Sasa cha kujiuliza uasi huu unatokana na nini?? Ee wabongo, ni ufinyu wa fahamu juu ya kile wanachokitenda ama?? Huu ni ulimbukeni wa kuiga hata visivyoigika, ni kasumba ya kuthamini vya wenzetu kuliko vyetu, ni ukosefu wa uzalendo, ni lack of confidence, ni utovu wa maadili na ushenzi uliopiliza.

Hii sio kazi ya shetani , ni utashi wa matunda ya wabongo wenyewe kwa jinsi maisha yanavyotubadilikia. Ni ukosefu wa shukrani kwa Mungu dhidi ya uumbaji wake. Ni dhambi na ni kufuru ya wabongo. hatujui tulitendalo.

WABONGO TUBADILIKE. wIKEND NJEMA!!
 
<br /> <br / KWELIII
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…